| Damu ya marehemu Bathlomeo Nzigilwa ilivyotiririka baada ya kuvamiwa na majambavi na kujeruhiwa vibaya akiwa kazini. |
| Bathlomeo Nzigilwa alipokuwa amelazwa katika hospitali ya Mkoa wa Iringa kabla ya kupelekwa katika hospitali ya Taifa ya Mhimbili. |
Nzigilwa amefariki dunia katika hospitali ya Taifa ya Mhimbili alikopelekwa kwa matibabu baada ya kuondolewa katika hospitali ya Mkoa wa Iringa alikokuwa amelazwa baada ya kuvamiwa.
Uvamii uliofanyika kanisani hapo ulikenda sambamba na uharibifu wa mali za Kanisa vikiwemo vyombo vitakatifu vya ibada.
Mavazi ya ibada na
vifaa mbalimbali vya ibada viliharibiwa vibaya, Taberenakulo ndogo nayo
ikiharibiwa, msalaba kuvunjwa pamoja na Hostia Takatifu zikimwagwa kila
mahali pamoja na fedha kadhaa kuibwa..
Bwana ametoa na Bwana ametwa, jina la Bwana lihimidiwe.
Mungu aiweke roho ya marehemu mahala pema mbinguni .... Amina.
No comments:
Post a Comment