masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Friday, November 16, 2012

Kanisa Katoliki Iringa lanajisiwa

Padre Angelo Burgio akiwa wodini katika hospitali ya Mkoa wa Iringa.

Padre Helman Myala akiwa katika hospitali ya  Mkoa wa Iringa.

Ikiwa ni siku moja tu baada ya Kanisa Katoliki Parokia ya Kihesa Jimbo la Iringa kunajisiwa, Parokia ya Isimani nayo imenajisiwa huku mapdre wawili wakinusurika kuuawa kwa bunduki, nondo, marungu na mapanga usiku wa kuamkia leo na watu wasnaosadikika kuwa ni majambazi.

Padre Angelo Burgio muitaliano wa Parokia ya Isimani amepigwa risasi huku mwenzake Paroko msaidizi Helman Myala akipigwa mapanga kichwani na nondo na virungu sehemu mbalimbali za mwili wake nusura kuuawa na watu hao.

Akizungumza na waandishi wa habari akiwa hospitali ya Mkoa, Padre Angelo Burgio Paroko anayemaliza muda wake, alisema walitokea watu 7 majira ya saa 4:30 usiku wakavunja mageti kisha wakaingia ndani na kuwavamia.

“Ilikuwa majira ya saa 4:30 usiku tulipokuwa tukijiandaa kulala ndipo walipotokea watu 7 wakiwa bunduki, virungu, nondo na mapanga wakatuvamia wakitaka tuwaoneshe pesa zilipo; wakaanza kunipiga kwa virungu huku mmoja akiniwekea bunduki tumboni kisha wakachukua zaidi ya milioni mbili na nusu huku mwenzangu Pd. Myala wakamchukulia shilingi milioni moja na laki tatu (1,300,000/=) pamoja na simu zetu zote” amesema Pd. Burgio.

Hata hivyo amesema hajui mali zingine zilizochukuliwa kwa kuwa baada ya kuvamiwa na kuumizwa hawakupata nguvu tena za kuweza kukagua vitu vingine.

“Kwa kweli sijui uharibifu mwingine kwa sababu baada ya kuvamiwa na kuumizwa hatukupata nguvu tena ya kuweza kukagua vitu vingine ndipo tulipokimbizwa na wasamalia wema hospitalini” amesema.

Kaimu wa Mganga Mkuu wa hospitali ya Mkoa wa Iringa Gwanchele Faustine amekiri kupokea majeruhi hao majira ya saa 7 usiku.

“Tumepokea majeruhi wawili usiku ambao ni Mapadre wa Kanisa katoliki Pd. Angelo Burgio muitaliano na Pd. Helman Myala. Pd. Angelo amepigwa risasi upande wa kushoto na kutokea upande wa kulia lakini kuna risasi zingine zipo kifuani tunamuandaa aingizwe kufanyiwa upasuaji sasa hivi” amesema Faustine.

Hata hivyo alisema pamoja na matibabu wanayoendelea kupata, hali zao zinaendelea vizuri.

Taarifa zinazolifikia gazeti hili tunapoingia mitamboni zilieleza kuwa tayari mtu mmoja ametiwa nguvuni kwa kusadikiwa muwa ni mmoja wa tukio hilo la ujambazi.

Diwani wa Kata ya Kihorogota Costantino Kihwele amesema vijana wameingia kwenye msako kila sehemu na kufanikiwa kumkamata kijana mmoja anayesadikiwa kuwa ni mmoja wa tukio hilo akiwa na bunduki.

“kuna kijana mmoja ametiwa nguvuni mwa vijana wa Isimani ambao waliamua kuingia msituni kufanya msako lakini jina lake nitakwambia kadiri tutakavyokuwa tunaendelea na msako. Usijali jina tutakutajia kwa sabu hatutaki kulitaja sasa hivi” amesema.

Katika hatua nyingine Dkt. Faustine amesema mlinzi wa Kanisa la Kihesa aliyejeruhiwa jana hali yake bado ni mbaya.

“Mlinzi wa Kanisa la Kihesa aliyejeruhiwa na kufikishwa hapa bado hali yake ni mbaya na bado tunaendelea kumhudumia” amesema.

No comments:

Post a Comment