masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Thursday, November 15, 2012

Mlinzi wa Kanisa ajeruhiwa nusura kuuawa na Kanisa kuvunjwa

Damu ya mlinzi wa Kanisa ikitiririka baada ya kuumizwa na watu wasiojulikana.



Tabrenakulo ndogo ikiwa imeharibiwa na kulia ni Msalaba uliovunjwa.


Muuguzi mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Iringa Rustica Tung'ombe akitoa taarifa kwa waandishi wa habari juu ya mlinzi aliyeumizwa na kufukishwa hospitalini hapo  leo.

Mlinzi aliyeumizwa na watu wasiojulikana akiwa amelazwa hospitalini.


Kanisa Katoliki Parokia ya Kihesa Jimbo la Iringa limevunjwa na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia leo huku mlinzi wa Kanisa hilo Bathlomeo Nzigilwa akijeruhiwa nusura kuuawa.

Akitolea maelezo juu ya tukio hilo kanisani hapo leo, mhuduma wa Kanisa hilo Sista Lucy Grace Mgata amesema aligungua kuwa kunauvamizi umefanyika alfajiri alipofika kanisani hapo kwa ajili ya kufungua milango ya Kanisa hilo ili kutayarisha vyombo vya Ibada ya Misa ambazo hufanyika kila siku kuanzia saa 12:00 asubuhi.

“Nilifika hapa saa 11:40 alfajiri kwa ajili ya kufungua milango na kufanya maandalizi kwa ajili ya Misa lakini nilipoukaribia mlango huo nikakuta mlinzi amekaa kwenye kiti huku kichwa chake akikiwa kimeinamishwa chini na kufunikwa kofia nikajua amelala lakini milango ikawa wazi. Nilopofika jirani nikaona damu inatiririka chini na mwili wake ukiwa umelowa damu nikaenda kugonga nyumba ya padre kutoa taarifa ndipo walipofika waamini mbalimbali tukasaidia” alisema.

Pamoja na kuvunjwa kwa milango ya Kanisa hilo, ofisi ya parokia nayo imevunjwa huku vitabu, mafaili mbalimbali na pamoj na kumbukumbu zikiwa zimechanwa na kuvurugwa ovyo kiasi cha kutotamanika.

Mavazi ya ibada na vifaa mbalimbali vya ibada vimeharibiwa vibaya, Taberenakulo ndogo nayo ikiharibiwa, msalaba kuvunjwa pamoja na Hostia Takatifu zikimwagwa kila mahali.

Sista Mgata alisema kuwa kuliwa na hela za watumishi wa artare walizokuwa wakichangishana kwa ajili ya matumizi ya umoja wao pamoja na hela za chama cha kitume cha utume wa Fatima zimechukuliwa japo bado hazijajulikana jumla yake japo kuwa funguo za teberenakulo kubwa wanayohifadhia Ekaristi Takatifu hazijulikani zilipo.

“Kulikuwa na hela ambazo watumishi wa artare walikuwa wakichangishana kwa ajili ya matumizi ya umoja wao pamoja na fedha za chama cha kitume cha utume wa Fatima zimechukuliwa ingawa sijajuwa jumla yake mpaka wao wenyewe waje waeleze kulikuwa na kiasi gani pamoja na funguo za taberenakulo kubwa hazionekani” alisema sista Mgata.

Kwa upande wake Katekista Agustino Luhama mhudumu wa ofisi ya Parokia amesema hela anazozikumbuka kwa harakaharaka ambazo zimechukuliwa na wavamizi hao ni zaidi ya shilingi laki tano.

“Hela ninazozikumbuka kwa harakaharaka ambazo zimechukuliwa ni zaidi ya shilingi laki tano lakini zingine sijapata idadi kwa sababu nilikuwa sijazijumlisha na zingine nilizipokea jana kutoka kwa waamini mbalimbali” alisema Kat. Luhama.

Padre Aloyce Mdemu ambaye pia ni Makamu wa Askofu wa jimbo hilo amesema bado ni mapema kujua thamani ya uharibifu uliofanyika kwa kuwa bado wanaendelea na uchunguzi wa vifaa vingine na maeneo mengine ambayo huenda hayajagundulika.

“Ni kweli tukio hili limetokea na limetushtua sana hata kuumizwa nuzura kuuawa mlinzi wetu lakini bado ni mapema sana kujua thamani ya uharibifu wa vitu vyote vilivyoharibiwa kwa sababu tunaendelea na uchunguzi wa vitu vingine na maeneo mengine ambayo huenda nayo yameharibiwa na hayajajulikana. Tutakapokuwa tumekamilisha, taarifa zitatolewa” alisema Pd. Mdemu.

Muuguzi mfawidhi wa hospitali ya Mkoa wa Iringa Rustica Tung’ombe amethibitisha kupokea majeruhi huyo na kusema kuwa hali yake ni mbaya na japo kuwa anaendelea kupata matibabu.

“Ni kweli tumempokea majeruhi Bathlomeo Nzigilwa mlinzi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Kihesa ambaye ni mkazi wa kwa Semtema akiwa na hali mbaya amelazwa chumba namba 9 lakini bado hali yake ni mbaya wala hajapata ufahamu” alisema Tung’ombe.

Hata hivyo, licha ya polisi kutaarifiwa alfajiri kabla ya saa 12 walifika katika eneo la tukio kwa kuchelewa majira ya saa 02:37 asubuhi.

No comments:

Post a Comment