masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Friday, October 26, 2012

Watoto wauawa kwenye mapigano Sudan



Jeshi la Sudan limesema watato wawili wameuawa kufuatia mashambulio mapya ya mabomu yaliyotekelezwa na waasi katika mji mkuu wa jimbo la Kordofan ya Kusini.

Msemaji wa jeshi la nchini hiyo amesema kuwa raia wanane walijeruhiwa wakati wa shambulio hilo mjini Kadugli.

Kundi la waasi wa SPLM-North nchini Sudan limesema lilikuwa likijibu mashambulio ya siku kadhaa yaliyotekelezwa dhidi yao na wanajeshi wa serikali

Umoja wa mataifa unakadiria kuwa maelfu ya watu wamehama makwao na wengine wengi kuathirika kutokana na mapigano hayo katika eneo la Kordofan ya Kusini, tangu uasi huo ulipoanza mwaka uliopita wakati Sudan Kusini ilijapatia uhuru wake.




Source:   BBC Swahili

No comments:

Post a Comment