masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Sunday, October 28, 2012

MOHAMED ENTERPRISES YANYANG’ANYWA LESENI NA TFRA


Mohamed Enterprises inayojishughulisha na uuzaji wa pembejeo za kilimo pamoja na bidhaa mbalimbali nchini imenyang’anywa leseni hiyo na mamlaka ya udhibiti wa mbolea nchini - Tanzania Fertilizer Regulator Authority (TFR) iliopo chini ya wizara ya kilimo, chakula na ushirika baada ya kuvunja masharti ya uuzaji wa mbolea.

Akizungumza na mtandao huu hii leo Mkurugenzi mtendaji wa TFRA Dk. Susan Ikerra, amesema hatua hiyo imetokana na kampuni kuvunja taratibu za biashara ya mbolea na hivyo wakulima kuingia hasara kwa kuuziwa pembejeo zilizo mbovu. 

Dk. Ikerra amesema makosa yaliyosababisha kampuni hiyo kunyang’anywa na kufungiwa biashara ya mbolea nchini, ni pamoja na bidhaa hiyo kukutwa ikiwa haina vigezo  huku mbolea ya CAN na DAP kuwa na virutubisho vya Nitrojen 12 kati ya 27 inayotakiwa jambo linaloifanya mbolea hiyo kutofanya kazi inayokusudiwa.

“Kampuni hii imevunja masharti ya uuzaji wa mbolea nchini, anauza mbolea iliyo na ujazo wa kilo 9, hatuna ujazo huu sisi, hiyo haikubaliki, pia mbolea hii imegnda kama aunavyoona, tayari imepoteza ubora wake, kwa hiyo mkulima akinunua mbolea hii haitamsaidia, huu ni uchafu tu, na nimenyang’anya leseni yake kwa sababu hizo, afanye biashara nyingine, lakini siyo ya mbolea,” amesema Dk. Ikerra

Amesema lengo la mamlaka hiyo licha ya kuanza mapema mwaka huu itahakikisha mbole inayouzwa kwa mkulima inakuwa na ubora ili kuboresha sekta ya kilimo, kwa kuondoa uchafu na changamoto zinazowakabili wakulima na kuwapa hasara bada ya kuuziwa mbolea zisizofaa.

“Nimekuja Iringa kuhakiki ubora wa mbolea kwenye magodawn, kwenye maduka,  na kwa mawakala,  ambako huko nimekuta matatizo makubwa kama uwepo wa mbolea zisizo na taarifa maalumu kutengenezwa wala kuisha muda wake, mbolea nyingi zimeganda na tayari nimemjulisha mkurugenzi wa kampuni hii, na amekubaliana nami,” amesema.

Amesema matokeo ya maabara kutoa SUA juu ya mbolea hiyo kutokuwa na ubora tayari yalikabidhiwa kwa Waziri wa kilimo mwenye dhamana  Christopher Chiza, huku naye Mohamed Enterprises akipatiwa taarifa hiyo pamoja na barua ya usitishaji wa biashara hiyo.

Ameutaka uongozi wa kampuni hiyo kutouza mbolea hiyo ya CAN na DAP, kwani amefungiwa rasmi kufanya biashara hiyo, na kuwa jeshi la polisi na Manispaa zitapewa barua ya sitisho la leseni ya uuzaji wa mbolea kote nchini.

Naye ofisa kilimo wa Manispaa ya Iringa Gerald Mwamuhamila amesema baada ya kubaini kampuni hiyo inawauzia wakulima mbolea chafu walifika katika ghara hiyo na kukuta mifuko ya mbolea isiyo na naironi ya ndani, jambo linalosababisha mbolea kupoteza ubora mapema.

Mwamuhamila amesema katika ghara hilo kulikuwa na mbolea zilizokuwa zimeganda, huku kukiwa na mifuko ya mbolea aina ya UREA yenye ujazo wa kilo 9 ambayo haifahamiki, kwani hakuna ujazo huo na kuchukua baadhi ya mifuko hiyo kama ushahidi na kuipeleka polisi.

Mtaslimu (Accountant officer) wa kampuni ya Mohamed Enterprises mkoa wa Iringa Ivan Ole Mganga alikubaliana na hatua hiyo na kuweka saini katika fomu ya usitishwaji wa leseni katika biashara hiyo ya mbolea.

Nao baadhi ya mawakala wa mbolea, walikutwa na zoezi hilo wakikiuka taratibu za utunzaji na uuzaji wa mbole, huku wengi wao wakiwa wameifungua mifuko hiyo ya mbolea jambo lilipunguza ubora na kuyafanya mazao yashindwe kustawi vizuri.

Akitoa sababu za kufanya hivyo mmoja wa wauzaji wa bidhaa hiyo Charles Kamazu alisema hulazimika kufungua mifuko kwa lengo la kupima kwa ujazo wa kilo, kwani baadhi ya wakulima hwana uwezo wa kununu mfuko mzima wenye kilo 50.

Mawakala nao waliiomba serikali kuweka mbolea hiyo pi katika ujazo wa kilo 2 na zaidi ili kuwasaidia wananchi hao, kwani walio wengi wamekuwa wakinunua mbolea kidogo kidogo pasipo kujua madhara yake.

“Hatufahamu kama mfuko ukifunguliwa na kuachwa wazi mbolea inakwisha ubora, lakini tunalazimkka kufany hivyo kwani wateja walio wengi ndiyo wanataka kupimiwa kuanzia kilo moja na kuendelea, serikali ianzie kufunga mbolea kuanzia kilo mbili siyo mbaya,” mesema Kamazu.

Pia waliitaka serikali kutoa elimu zaidi juu ya utunzaji wa pembejeo hizo, ili kuepukana na uharibifu wa bidhaa hiyo, unaosababisha ubora kupungua, na kumsababishia mkulima hasara na hivyo sekta ya kilimo kushindwa kufikia mlengo yake.

Wakati wa uanzishaji wa mamlaka hiyo mapema mwezi wanne, waziri Chiza alisema, TFRA imeanzishwa ili kusimamia masuala yote yahusuyo sekta ya mbolea na ubora wake-Bio, ambapo kutakuwa na utaratibu wa ukaguzi wa mara kwa mara wa bidhaa hiyo.












No comments:

Post a Comment