masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Tuesday, October 30, 2012

Mkuu wa Shirika la Consolata Tanzania amezikwa leo: > Usikose kufuatilia matukio haya kwa kina kesho

Picha inayoonekana ni marehemu Padre Salutaris Lello Masawe aliyekuwa Mkuu wa Shirila la Wamisionari wa Consolata Tanzania ambaye amezikwa leo katika makaburi ya Jimbo la Iringa yaliyopo Tosamaganga.




Wakristo Wakatoliki wameshauriwa kujiuliza kuwa wanahusiana na wengine vipi kama ishara ya kujiandaa kuufikia uzima wa milele mbinguni.

Hayo yamezungumzwa leo na Askofu wa Jimbo Katoliki la Iringa Mhashamu Tarcisius Ngalalekumtwa alipokuwa akihubiri wakati wa Misa ya Mazishi ya Padre Salutaris Lello Massawe ilifofanyika katika Kanisa la Moyo Mt. wa Yesu Parokia ya Tosamaganga jimboni humu.

Amesema binadamu hataulizwa endapo alitenda matendo ya upendo bali ataulizwa kama alikuwa na roho ya ubinadamu na haki katika kuwajali wengine.

“Swali la kujiuliza kila wakati katika maisha ni kwamba, umehusiana na watu wangapi wakakubariki? Na tena hatutaulizwa endapo tulitenda upendo bali tutaulizwa kama tulikuwa na roho ya ubinadamu na haki katika kuwajali wengine” amesema

Amesema Mungu ana mzaha katika kuvichukua viumbe wake kwani huchukua muda anaoutaka ambao binadamu haujui lakini jambo la msingi ni kujiandaa kiroho ili kuwa tayari wakati wowote.

“Munu ana mzaha pia. Mzaha wenyewe ni kiama huu ambao kila mtu anajiuliza kwa nini Massawe ameondoka wakati ambao hakutarajiwa? Kila mtu anajiuliza, kwa nini mapema? Kwa nini ghafla? Huo ndiyo mzaha wenyewe ila yeye anajua kila mtu atamchukuaje na kwa wakati gani” amesema.

Akimzungumzia Massawe Mhashamu askofu Ngalalekumtwa amesema alikuwa ni mtu mwenye bidii, uaminifu katika kuwajibika na alikuwa na maneno ya kutia moyo.

“Kazi za kitume alizitenda kwa bidii na kwa uaminifu. Pia alikuwa na maneno ya kutia moyo. Aliadhimisha matendo ya wokovu kwa nidhamu. Tunaimani kabisa kuwa huko alikokwenda ni kuzuri” amesema.

Amewataka Wakristo kuwa ni watu wa kutenda haki na kujituma katika kuwasaidia wanaohitaji msaada kwa kutenda matendo ya upendo wakijua kuwa maisha ya mwanadamu ni safari ya kumtafuta Mungu.

“Tendeni matendo ya haki, matendo ya upendo kwa kuwasaidia wahitaji kwa kujua kuwa safari ya mwanadamu ni kumtafuta Mungu; binadamu kajaliwa moyo mkubwa wa kuweza kumwelekea Mungu” amesema.

Padre Salutaris Lukas Massawe Lello alizaliwa Moshi Julai 8, 1962. Baba yake ni Lukas Victor na Mama, Maria Illuminata Manka.

Alisoma katika shule ya msingi ya Singachini kati mwka 1971 – 1978, akajiunga katika seminari ya Maua ambapo alisoma mpaka 1985, alipohitimu masomo ya sekondari.

Mwaka 1985 alianza masomo ya falsafa na teolojia katika seminari ya Consolata ya Nairobi na kuhitimu mwaka 1988 alipoanza unovisi. Alimaliza unovisi mwaka 1989 na akafunga nadhiri za kwanza 21 Julai 1989 Sagana (Kenya).

23 Oktoba 1992 alifunga nadhiri za milele Nairobi na 28 Novemba 1992 akapewa daraja la ushemasi.

Julai 27, 1993 alipewa daraja la upadre Moshi kwa kuwekewa mikono na Mhashamu Baba Askofu A. Msarika.

Pd. Massawe alifanya kazi ya umisionari katika nchi ya Ethiopia kutoaka 1995 hadi mwaka 2000 baada ya hapo akatumwa Italia akifanya kazi ya uhamasishaji wa roho ya umisionari hadi mwaka 2007 aliporudi Tanzania.

Baada ya kusoma katika Chuo Kikuu cha Mt. Augustino Mwanza, akatumwa Bunju, Dar es Salaam kwa ajili ya shughuli za gazeti la wamisionari wa Consolata “Enendeni. Kutoka Septemba 7, 2011 alikuwa Baba Mkuu wa Shirika la Wamisionari wa Consolata nchini Tanzania.

Pd. Massawe alifariki Oktoba 25, 2012 Bagamoyo kwa ajali ya Maji na kuzikwa Oktoba 30, 2012 katika makaburi ya Jimbo yaliyopo Tosamaganga.

Mazishi hayo yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali na madhehebu ya kidini kutoka ndani na nje ya nchi ambapo jumla maaskofu wanne walihudhuria mazishi hayo.

Maaskofu hao ni pamoja na Mhashamu Desderius Rwoma wa Jimbo Katoliki la Singida, Mhashamu Alfred Maluma wa Njombe, Mhashamu Evaristo Chengula wa Mbeya pamoja na Mhashamu Tarcisius Ngalalekumtwa wa Iringa ambaye pia ni Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania.

No comments:

Post a Comment