masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Friday, October 26, 2012

Wasomi wapinga ripoti ya kamati ya Nchimbi > Wasema ni ya kihuni > Wamtaka Kamuhanda aondoke Iringa kwa hiari yake

Baadhi ya wasomi wa vyuo vikuu vya Iringa wakiwa katika viwanja vja bustani ya Manispaa wakati wa kuongea na vyombo vya habari kupinga ripoti ya kamati iliyoundwa na Waziri Emmanuel Nchimbi juu ya mauaji ya Daud Mwangosi










Watanzania wameaswa kutokubali ripoti ya kamati iliyoundwa na Waziri wa Mambo ya ndani Emmanuel Nchimbi juu ya mauaji ya aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo cha runinga cha Channel ten Daudi Mwangosi kwa kuwa haina ukweli wowote na inapingana na katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kauli imetolewa leo na Rose Mayemba mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCO) katika umoja wa wasomi wa vyuo vikuu vya mjini Iringa uliofanyika katika viwanja vya bustani ya Manispaa ya Iringa kwa ajili ya kupinga ripoti hiyo na kulaani vitendo vya uongozi wa Mkoa huo kukaa kimya baada ya tukio la mauaji ya mwanahabari huyo.

Mayemba amesema ripoti iliyotolewa na kamati ya nchimbi ni batili kwa kuwa inalenga kuwaondoa wahusika wa tukio la mauaji hayo  kwa makusudi.

“Ripoti ya Nchimbi ni batili, inalenga kuwakwepesha wahusika wa mauaji yale. Haikuwa na sababu yoyote ya kusomwa kwa kuwa haina ukweli wowote. Inawapasa watanzania kuipuuza na kuilaani kwa kuwa inakiuka haki za binadamu” amesema.

Pia mesem,a serikali kupitia vyombo vya dola hasa polisi iache kuwalazimisha wananchi kufuata sheria zao feki zisizo za haki kwani zinalenga ukandamizaji wa wazi.

“Serikali kupitia polisi acheni kutulazimisha kudfuata sheria zenu feki za kikandamizaji na unyanyasaji kwani zinatunyima haki zetu kwa makusudi. Hata hivyo Nchimbi alitumia sheria gani kuunda tumwe feki ambayo imeleta ripoti feki namna hii” amesema.

Naye Olime Mwakilembe mwanafunzi wa RUCO amewataka serikali kutumia ushahidi wa uhalisia ili kuwapa wananchi matumaini ya kupata haki zao badala ya kupindisha uongo kuiwa ukweli kama ilivyo kwa ripoti ya tume ya Nchimbi.

“Serikali iwe makini na ushahidi wa uhalisia, watumie picha zinazoonesha ukweli badala ya kutumia uongo unaoonekana wazi. Huu ni uonezi na ni udhalilishaji wa haki za binadamu” alisema Mwakilembe.

Amewataka wasomi waungane kwa pamoja katika kuishauri serikali kuwa na ukweli kwa matukio ja kijamii badala ya kutumia mabavu na uongo kwa kuiaminisha jamii uongo usio  na maana.

“Wasomi tuwe na umoja katika kiishauri serikali kuwa na ukweli kwa matukio kama haya ambayo yanatudhalilisha bila sababu. Tunaipinga ripoti ya Nchimbi kwa sababu (1) ina majibu feki, (2) haina uhalisia na (3) polisi wanalinda kibarua chao badala ya kufanya kazi zinazostahili.

Jescar Kishoa mwanafinzi wa RUCO amewataka waandishi kutokubali kulazimishwa kufanya kazi za kihuni kwa ajili ya kuwasafisha wahuni na badala yake wawajibike kwa kufuata maadili yao.

“Waandishi msikubali kulazimishwa kuandika habari za kuwasafisha watu waliojaa kila aina ya hila kwa ajili ya maslahi yao badala yake mfanye kazi kwa kuzingatia maadili yenu kwa ajili ya manufaa ya jamii” amesema.

Vitus Rupeche mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Tumaini amewaasa waandishi kuwa sauti ya wanyonge badala ya kutumika na mafisadi wasiokuwa na huruma kwa wananchi na kufuata nyayo za marehemu Mwangosi wakati wa uhai wake.

“Waandishi msikubali kutumika na mafisadi na badala yake muwe sauti ya wanyonge kama alivyokuwa Mwangosi wakati wa uhai wake. Wanafunzi tulipokuwa tunadai pesa za mikopo, Mwangosi alikuwa ndio sauti yetu na kuhakikisha tunapata mikopo hiyo. Wasaidieni wanyonge” amesema.

Nico Mwakabilikile mwanafunzi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Mkwawa amesema nchi inakoelekea ni kubaya kwa kuwa watu wachache wanaamua kufanya mambo yao kwa maslahi yao binafsi bila kuwajali wengine.

“Nchi inakoelekea si kuzuri. Mauaji yanayoendelea kufanyika yanatugawa wananchi katika matabaka kwa kuonesha upendeleo wa wazi. Alipouawa Mwangosi mwandishi wa habari, serikali haikutoa matamko yoyote lakini alipouawa kamanda wa polisi wa Mwanza, serikali imetoa matamko ya kila aina. Je, Mwangosi hakuwa binadamu kama Liberatus Barlow? Huu ni uonezi na matabaka haya hayafai kabisa” amesema Mwakabilikile.

Hali kadhalika Gofrey Bagamba mwanafunzi wa RUCO alisema mwananchi wa leo si wa miaka ya 77 kwani ana upeo mkubwa wa mabo na kuyaona mambo na kuyaelewa sambamba na kuujua uongo na ukweli.

“Sisi wananchi tunauona ukweli, hatuwezi kulazimishwa kupotoshwa kuamini uongo wakati tunaona kwa macho yetu. Wananchi wa leo ni tofauti na wale wa miaka ya 77 kwani tunayaona mambo na kuayelewa. Katiba ya nchi inavunjwa na wachache wanaolazimisha mabo hasa serikali isiyokuwa na mtizamo wa mbali kwa maslahi ya taifa” amesema Bagamba.

Katika hatua nyingine Oscar Kamayugi mwanafunzai wa Chuo Kikuu kishiriki cha Mkwawa amelaani vikali vitendo vya uongozi wa mkoa wa Iringa kukaa kimya katika tukio la kuuawa kwa Mwangosi kwa kujifanya kama mkoa hauna viongozi.

“Kitendo cha viongozi wa Mkoa kukaa kimya hadi leo katika mauaji ya Mwangosi kilaaniwe kwa hali yoyote ile. Ni dhahiri kwamba serikali inahusika kwa mauaji ya Mwangosi. Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa wilaya na viongozi wengine wote walaaniwe. Ukimya wao unatuonesha wazi kuwa wao ni wahusika wakuu na mauaji hayo waliyapanga kwa manufaa yao” mesema Kamayugi.

Hata hivyo amesema vitendo wanavyoendelea kufanyiwa waandishi wa habari wawapo kazini hasa katika kesi ya mtuhumiwa wa mauaji ya Mwangosi vinafanyiwa kazi.

“Vitendo vya Polisi kupiga na kuwanyanyasa waandishi wa habari waswapo kazini hasa mahakamani wanapoandika habari za mtuhumiwa wa mauaji, sisi tunaviona na tunavifanyia kazi” amesema.

Amesema kuanzia leo watahakikisha waandishi wa habari wanapiga picha za mtuhumiwa huyo kwa uhuru bila kubughudhiwa na mtu vinginevyo patachimbika.

“Kuanzia leo hatutakuwa tayari kuona mtuhumiwa huyo anafunikwa sura anapofikishwa mahakamani na hatutakuwa tayari kuona waandishi wa habari wananyanyaswa wanapowajibika katika kazi zao vinginevyo patachimbika.

Amewataka wanairinga kushirikiana na waandishi wa habari wakati mtuhumiwa huyo akifikishwa mahakamani ili kuhakikisha hafunikwi wala waandishi hawafanyiwi hila yoyote.

“Umefika wakati sasa na sisi wananchi kuonesha machungu yetu. Tuache shughuli zetu wakati mtuhumiwa huyo anapofikishwa mahakamani kushirikiana na waandishi ili kuhakikisha anaonekana sura yake na waandishi wanampiga picha bila bikumbo. Si kwamba hatuwezi, tunauwezo mkubwa sana, kwa nini waandishi wanyanyashwe na sisi tukae kimya?” Tuoneshe nmachungu yetu.

Nicolas Francis amemtaka Kamanda wa polisi Mkoa wa Iringa kwa hiari yake aondoke kwa kuwa wananchi wamechoka kumuona akiendelea kurandaranda ndani ya mkoa huo.

“Nimpe taarifa Kamuhanda kwa hiari yake mwenyewe aondoke Iringa kwa kuwa wananchi hawataki kumuona akiendelea kuzunguka na kurandaranda mkoani hapa. Awaache wananchi wa Iringa warudishe amani yao na waendelee na mahusiano yao mazuri na p;olisi yaliyokuwepo hapo awali. Kamuhanda asiendelee kupandisha hasira za wanairinga kwani asifikiri kwa kuwa wapo kimya wamemsifu kwa kile alichokifanya. Kamuhanda uondoke kwa hiari yako” alisema.

Wasomi hao walipanga kuanza na maandamano kuanzia Kihesa na kuhiotimisha katika viwanja hivyo vya bustani ya Manispaa lakini maandamano hayo yalizuiliwa na Polisi hata hivyo w2asomi hao walifanya harambee kwa ajili ya kumsaidia mjane wa marehemu Mwangosi.


No comments:

Post a Comment