| Hezlon Lusapi Mwenyekiti wa wanafunzi wa vyuo vikuu kutoka Wilaya ya Kilolo akiwahutubia wananchi katika kijiji cha Utengule |
| Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Utengule wakisikiliza maelezo ya wanafunzi. |
| Mmoja wa wananchi wa akitoa rambirambi ya Mwangosi. |
Wananchi wa Kijiji cha Utengule Wilaya ya Kilolo Mkoa wa
Iringa wanaendelea kumlilia marehemu Daud Mwangosi kwa kutoa rambirambi ya
shilingi 15,000 kwa ajili ya kusaidia mjane na watoto wake.
Hayo yalifanyika juzi katika mkutanao wa Chama cha
Democrasia na Maendeleo CHADEMA uliofanyika na kijijini hapo na umoja wa
wanafunzi wa vyuo vikuu wanaotoka katika Wilaya hiyo.
Akiwahutubia wananchi wa kijiji katika mkutano huo,
mwenyekiti wa wanafunzi hao wilaya Hezlon Lusapi aliwataka wananchi kutokubali
kuruzwa na viongozi wasiopenda haki na
kutumia nafasi zao kwa kuwaonea wengine.
“Msikubali kuwa watumwa wa viongozi wasio waadilifu na
kuwatumia ninyi kama watumwa kwa ajili ya maslahi yao binafsi; hojini haki zenu
bila woga ili muweze kupata ukweli wa jambo lolote” alisema Lusapi.
Alisema wapo baadhi ya viomgozi wanatoa amri kuwataka
wananchi kuto michango bila kutolea maelezo juu y uhalali wa michango hiyo na
matumizi yake.
“Kuweni na utamaduni wa kuhoji ukweli wa mambo, msikubali
kuendeshwa kama magari mabovu kwa kuwa mna haki zenu za kujua kila
kinachoendelea katika nchi na maeneo yenu kwa ajili ya maendeleo ya umma. Kuweni
ni watu wa kuhoji na kujua uhalisia wa mambo” alisema.
Alisema wananchi wana jukumu la kutoa ushirikiano kwa waandishi
wa habari wawapo kazini kwa kuhakikisha wanawajibika kwa manufaa ya umma.
“Kuuawa, kupigwa na kunyanyaswa kwa waandishi wa habari
kunatokana na kukosa uongozi bora. Jamii tunajukumu la kutoa ushirikiano wa
dhati kwa waandishi wanapowajibika kwa kazi zetu ili wawe salama kwa wakati
wote” alisema.
Naye Oscar Ndale mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Ruaha RUCO
anayesoma kitivo cha sheria mwaka wa nne alisema ili kulijenga taifa la
Tanzania, wananchi wasiwe kama wakimbizi ndani yao.
“Msikubali kuishi kama wakimbizi ndani ya nchi yenu, tunajua
kuwa wapo baadhi ya viongozi wa wanaowajengea wananchi mazingira ya kuwa kama
wakimbizi ili mradi wanyenyekewe kama watemi na kutowapa wananchi nafasi ya
kuhoji. Wafichueni viongozi wa namna hiyo ili waweze kuwajibishwa” alisema
Ndale.
No comments:
Post a Comment