| Wananchi walioamua kutembea kutoka Mafinga hadi Nyololo kwa ajili ya kumuenzi Daud Mwangosi na kulaani vitendo wanavyotendewa waandishi wa habari wakiwa kazini na jeshi la polisi Tanzania |
| Watembezi wakipumzika katika msitu wa Nyololo. |
| Watembezi wanapumzika katika stendi ya Nyololo bara baada ya kuwasili kijijini hapo. |
| Watembezi wakiwa wamesimama chini ya mti katika eneo alilouliwa Daud Mwangosi mara baada ya kupokelewa na wenyeji. |
| Mwenyekiti wa matembezi Mr. Bookshop alitoa ujumbe baada ya kupokelewa na wenyeji katika eneo hilo. |
| Ujumbe unavyosomeka katika fulana za watembezi hao |
| Mtembezi Selina Luhala akishindwa kutembea baada ya kuwasili katika eneo hilo. |
Matembezi ya kumuuenzi aliyekuwa
mwandishi wa habari wa kituo cha Channel Ten na Mwenyekiti wa chama cha waandishi
wa habari Mkoa wa Iringa (IPC) Daud Mwangosi yamefanyika leo kutoka mji mdogo
wa Mafinga hadi Kijiji cha Nyololo alikouliwa.
Matembezi hayo ambayo yalikuwa ni
mahususi kwa ajili ya kulaani vitendo wanavyotendewa waandishi wa habari wawapo
kazini yalikuwa na ujumbe maalumu “WAANDISHI WA HABARI WAHESHIMIWE NA KULINDWA
WANAPOCHUKUA HABARI”.
Kabla ya matembezi hayo watembezi
walisema hakuna haja ya kumsubiri mtu kumuunga mkono kwa kuwa hata wakiwa
wachache wanauwezo wa kufikisha ujumbe kwa jamii.
Matembezi ambayo yalikuwa ni ya
watu watano ambao ni Mr. Bookshop, Rogers Mselu, Zacharia Zaheks, Muinjilisti
Joisen Nyaluke wote wa Mafinga na Selina Luhala maarufu kwa jina la Mama Denis
kutoka Iringa mjini ylipokelewa na Mwenyekiti wa kitongoji cha Ilala Nyololo
njiapanda Shemu Kyando.
Akiongea mara baada ya kupokelewa
kwa matembezi hayo mwenyekiti wa matembezi Mr. Bookshop wa Mafinga alisema wananchi
hawanabudi kuwaaunga mkono waandishi wawapo kazini na kuwapa nguvu zaidi ili
wasiwe na woga wakati wakiwajibika na kazi yao .
“Mwandishi wa habari ni mtu
muhimu kwetu sisi wananchi kwa kuwa ndio watetezi wetu, tuwape nguvu za kutosha
wawapo kazini ili wasiwe na woga wanapowajibika kwa ajili ya taifa letu”
alisema.
Amewataka waandishi wa habari
kutosaitiana katika msimamo wanaojiwekea ili kulinda nidhamu ya taaluma na
heshima yao kwa
jamii.
“Mwandishi ambaye ataonekana
anaendelea kuandika habari za polisi wakati msimamo ni kutoandika habari za
polisi, hatufai sisi wananchi na lazima tumtilie shaka juu yake na jeshi la
polisi” alisema.
Alisema wakati zimebaki siku chache
kufanya kumbukumbu ya kifo cha Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, wananchi
wamekuwa hawana imani na usalama wao kutokana vitendo vichafu wanavyofanyiwa
waandishi wa habari hasa kuuawa kwa Mwangosi na waandishi wa mkoa wa Iringa
kuendelea kunyanyaswa na jeshi la polisi wanapowajibika kazini.
“Sioni haja ya kufanya kumbukumbu
ya Mwalimu kwa sababu itakuwa ni kumdhalilisha tu. Yeye alipenda amani lakini
amani hii imetoweka kwa vitendo vichafu, vya kinyama na vya kidhalimu
vinavyofanywa na jeshi la polisi dhidi ya waandishi wa habari hususani
waandishi wa Mkoa wa Iringa” alisema.
Watembezi hao waliotembea
kilometa 41 wakati wakuwasilisha ujumbe huo, watembezi walioneshwa masalio ya
nyama ya mwandishi huyo aliyeuawa kwa kufyatuliwa bomu Septemba 2, 2012.
No comments:
Post a Comment