| Askari wa kikosi cha kuzuia ghasia wakiwa wamesambaa mahakamani hapo kuwadhibiti waandishi wa habari. |
| Askari wakiwa wamejipanga mahakamani kuwazuia waandishi wa habari wasimpige picha mtuhumiwa. |
| Mikono ya Posili wakizuia waandishi kupiga picha. |
| Askari wakiwa katika mlango wa gari kumficha mtuhumiwa asipigwe picha. |
| Askari wakitoka mahakamani hapo mara baada ya mtuhumiwa kuondoka. |
Mmiliki wa mtandao huu leo amenusurika kipigo kutoka kwa askari waliokuwa wameweka
ulinzi mzito mahakamani wakizuia waandishi wa habari wasimpige picha mtuhumiwa
wa mauaji ya aliyekuwa mwandishi wa kituo cha televisheni cha Chanel Ten, Daud
Mwangosi.
Hayo yametokea mara
baada ya mtuhumiwa huyo Pasificus Alphonce Simon kufikishwa katika Mahakama ya
Hakimu Mkazi kwa mara ya pili.
Askari mwenye
kitambulisho G.T. Timbuka katika mavazi yake alichukua uamuzi wa kutaka kumpiga mwandishi huyo
baada mwandishi huyo kugundua mbinu iliyotumika kumfikisha mtuhumiwa huyo
mahakamani hapo tofauti na siku ya kwanza alipofikishwa kwa gari la kifahari
lenye namba za usajili T 320 ARC.
Tofauti na siku ya kwanza
alipofikishwa kwa gari la kifahari, mtuhumiwa huyo leo amefikishwa mahakamani
hapo kwa miguu na kupitishwa katika mlango wa nyuma wa mahakama ili waandishi
wasimgundue mapema na kumpiga picha.
Mara baada ya mmiliki
huyo kugundua njia hiyo na kutaka kuingia mahakani hapo alianza kusukumwa na
askari na kupewa amri kuwa ni marufuku kuingia mahakamani hadi watakapotoa
ruhusa ya kuingia.
Alipohoji ni utaratibu
gani unatumika na ni lini umeanza askari aliyekuwa tayari kuanza kipigo aliyetambulika
kwa jina la G.T. Timbuka katika vazi
lake akiwa na kirungu mkononi akiambatana na askari waliovaa kiraia alisikika
akisema “huyu anaonekana mbishi hajui kuwa anaweza kuwa kwenye mstari sasa hivi!”.
Wakati hayo yakiendelea
walitokea askari wengine ambao walikuwa na silaha za moto na kutoa amri kwa
mwandishi huyo kuondoka mapema eneo lile vinginevyo watamshughulikia.
Katika hatua nyingine
mtuhumiwa wa mauaji hayo mwenye namba G 2573 akisomewa shitaka lake mbele ya
Hakimu Mkazi Mwandamizi Dyness Lyimo, mwendesha mashtaka na wakili wa serikali
Lilian Ngilangwa alisema mtuhumiwa huyo anatuhumiwa kwa kumuua Daud Mwangosi
kwa makusudi mnamo tarehe 02.09.2012 katika eneo la kijiji cha Nyololo Wilaya
ya Mufindi Mkoa wa Iringa.
Mtuhumiwa hakutakiwa kujibu
chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kisheria kusikiliza kesi za
mauaji.
Ilielezwa kuwa
upelelezi haujakamilika na kesi ikaahirishwa hadi Oktoba 10, 2012 itakapotajwa
tena mahakamani hapo na mtuhumiwa amerudishwa mahabusu.
Katika hali isiyokuwa
ya kawaida askari wakiwa na magari madogo zaidi ya matatu na gari kubwa moja,
mtuhumiwa huyo mara baada ya kutoka mahakamani alipakiwa katika gari lenye
namba DFP 2175 Land cruiser Pic up.
No comments:
Post a Comment