| Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Ugele Fredrick P. Assenga akitoa shukrani zake kwa mwakilishi wa Mbunge Rose Mayemba jana ofisini kwake. |
| Mwalimu Mkuu Msaidizi Maurisia Shandu akiwa ofisini hapo. |
| Baadhi ya wanafunzi wa shule uya msingi Ugele wakihijiwa na waandishi wa habari shuleni hapo. |
| Baadhi ya wanafunzi wakiwa na mwakilishi wa Mbunge Rose Mayemba shuleni hapo. |
| Kulia ni mkazi wa Ugele Joyce Mkanila akishuhudia chakula kilichotolewa na Mbunge kikiwa katika ofisi ya Mwalimu Mkuu wa shule hiyo. |
| Mwakilishi wa Mbunge Rose Mayemba akiwa na wanafunzi shuleni hapo. |
| Walimu wa shule ya msingi Ugele wakiwa nje ya ofisi ya Mwalimu Mkuu mara baada ya kupokea chakula. |
Mbunge wa jimbo la Iringa mjini Mch. Peter Msigwa (CHADEMA) ametimiza
ahadi aliyoahidi kwa kutoa chakula katika shule ya msingi Ugele iliyopo katika
kata ya Mtwivila Manispaa ya Iringa.
Kilo 100 za unga wa sembe pamoja na kilo 25 za maharage
vilivyotlewa shuleni hapo vina thamani ya jumla ya shilingi 170,000/= ambapo
shule hiyo ina waalimu wane akiwemo mwalimu wa kike mmoja.
Akikabidhi chakula hicho jana shuleni hapo, mwakilishi wa mbunge Rose Mayemba
alisema huo ni mwanzo katika kuihudumia shule hiyo kwa kuwa yapo mahitaji
mengine ambayo yatapelekwa kwa ajili ya wanafunzi.
“Mbunge amenituma nilete chakula hiki ikiwa ni sehemu ya
ahadi yake kuwawezesha wanafunzi kupata chakula wakati wa masomo ili
wasihangaike na kuhudhuria vipindi darasani kwa urahisi” alisema Mayemba.
Aliwataka waalimu pale linapojitokeza tatizo kuhusiana na
shule hiyo, ofisi ya mbunge iarifiwe ili kupatiwa ufumbuzi.
“Matatizo yatakayo kuwa yanajitokeza yaelezwe kwenye ofisi
ya mbunge ili yapatiwe ufumbuzi; pia iwe ni hamasa kwa wazazi kwa ajili ya
kuwajibika na kutoa ushirikiano kwa Mbunge ili kuleta maendeleo” alisema.
Akipokea chakula hicho shuleni hapo, Mwalimu Mkuu wa shule
hiyo Fredrick Assenga alisema Mbunge Msigwa amekuwa ni kiongozi wa utekelezji
tofauti na viongozi wengine.
“Tumekuwa tukiahidiwa mara nyingi bila kutekelezewa lakini
Mbunge Msigwa amekuwa tofauti na wengine kwa kuwa anaahidi na kutekeleza; hasa
ukiangalia shule hii ambayo iko pembezoni kama huku, kwa kweli tuna kila sababu
ya kumshukuru sana” alisema Assenga.
Aliwaomba watanzania wapende kuchangia kwa kuzisaidia shule
zilizopo pembezoni kwa kuwa zimekuwa zikisahaulika kila wakati na wenye
dhamana.
“Mimi naomba watanzania wapende kuchangia shule zilizo
pembezoni kama hii kwa kuwa zimekuwa zikisahaulika kila wakati na wenye dhamana
ya kutoa huduma hasa viongozi wa serikali. Naamini kuna wadau mbalimbali ambao
wanaweza kuguswa na kusaidia kwa ajili ya maendeleo” alisema.
Naye Joyce Mkanila mkazi wa Ugele alisema wakati umefika kwa
wananchi kuangalia nani muongo na nani mkweli ili waweze kuchukua maamuzi
sahihi wakati wa uchaguzi ukifika.
“Tumekuwa tukilalamika kuwa Mbunge ametudanganya lakini sasa
hatutasema tena. Vile vile nawasihi wananchi wenzangu kuangalia nani muongo na
nani mkweli ili kufanya uamuzi sahihi siku ya uchaguzi ukifika” alisema
Mkanila.
No comments:
Post a Comment