| Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) Profesa Iblahim Lipumba |
| Mbunge wa Iringa mjini Mch. Peter Msigwa akiwahutubia wananchi wa Iringa. |
| Bamba Juju Mjumbe wa Kamati Kuu Taifa ya NCCR Mageuzi |
| Maelfu ya wananchi wa Iringa wakiwa mwenye mkutano wa Ukawa jana. |
RAIS Jakaya Kikwete ametajwa kuwa ni msaliti namba moja
kutokana nakujidai kuunda kamati ya kukusanya maoni ya katiba mpya na badala
yake ameikana tume hiyo na kuidhalilisha kwa watanzania.
Aidha Rais Kikwete ametajwa kuwa mchochezi namba moja na ana
nia ya kulifanya taifa kutokuwa na umoja, Amani, utulivu kutokana na kauli za
uchochezi ambazo anazitoa mwenyewe pamoja na viongozi ndani ya serikali yake
bila kuchukuliwa hatua kali.
Kauli hiyo ilitolewa mjini Iringa na Makamu Mwenyekiti wa
Umoja wa katiba ya Wananchi (UKAWA) Profesa Iblahim Lipumba alipokuwa
akihutubia katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Mwembetogwa.
Mkutano huo ambao lengo lao kubwa ni kuhakikisha wanatoa ufafanuzi
ni kwa nini umoja huo umesusia kuendelea na vikao vya Bunge Maalum la Katiba na kutoka nje.
Profesa Lipumba alisema kuwa kitendo cha Rais wa nchi kudai
kuwa iwapo serikali tatu zitapita jeshi litachukua nchi ni uchochezi mkubwa.
Prof Lipumba alisema kuwa imeonekana wazi kuwa Rais Kikwete
pamoja na wanachama wa CCM hawakuwa na nia njema ya kutungwa kwa katiba japo
Rais Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM kukubali kuunda tume ya kukusanya
maoni huku akijua kuwa tume hiyo
inatumia fedha nyingi ya walipa kodi.
Kiongozi huyo alisema kilichowafanya wana Ukawa kutoka nje
ya Bunge Maalum la Katiba ni kutokana na
wajumbe wa bunge hilo kuonesha wazi kutokuwa na nia njema ya kuwa na katiba
mpya ambayo ni dira ya maendeleo kwa watanzania.
Aidha Profesa Lipumba alisema kuwa alichokifanya rais Kikwete
cha kutaka kuwepo kwa Katiba mpya ni kiini macho na kuwalaghai watanzania.
Alisema Rais Kikwete anatakiwa kuwaomba radhi watanzania
pamoja na kuiomba radhi tume ya Jaji Warioba kwa kutumia muda wao mwingi
kukusanya maoni ya wananchi kwa uaminifu lakini kutokana na ufisadi wa chama
cha mapinduzi Kikwete ameamua kuwadhalilisha viongozi hao ambao wana heshima
kubwa ndani ya nchi.
Akihutubia katika mkutano huo pia alisema kuwa nia kubwa ya
CCM kutaka kukwamisha mchakato wa katiba ni kutokana na hali yao ya ufisadi.
“Ndugu zangu wote mnajua kuwa katiba ni Roho ya nchi na Katiba
ikiwa nzuri vitendo vya wizi wa mali ya Umma vitakomeshwa.
“Lakini CCM haitaki kuwepo kwa katiba mpya hivyo wanafanya
kila liwezekanalo ili kuendeleza vitendo vyao vya kuhujumu nchi huku
wakiendeleza ufisadi ambao umeliingiza taifa katika hali ya umasikini” alisema
Prof Lipumba.
Mbali na hilo Profesa Lipumba alisema kuwa kwa sasa nchi
inaendeshwa kisanii kwani Rais Kikwete ana tofauti na Vasco Dagama ambaye
alikuwa ni mtu ambaye muda wake wote alikuwa akiwaza kutalii katika maeneo
mbalimbali.
“Ndugu zangu wana Iringa kwa sasa nchi yetu inaendeshwa na
Vasco Dagama wa karne ya 21 kwani muda wake wote anapenda kutalii, anatumia
fedha nyingi kwenda nchi za nje na anatumia fedha za walipa kodi jambo ambalo
ni hatari kwa taifa masikini kama hili.
“Tumekosa kiongozi
shupavu na mwenye fikra za kuona mbali katika utumishi na ndiyo maana amekuwa
akiwachekea wale wote ambao wamekuwa wakitajwa kuwa ni mafisadi wakubwa na
kuwasababishia watanzania wasijue hata maisha yao yatakuwaje” alisema Profesa
Lipumba.
Alisema kutokana na hali hiyo ndiyo maana serikali wamekuwa
maharamia kwa kutaka kuteka mchakato wa katiba na kufanya kila njia ili katiba
mpya isipatikane.
Mbali na hilo alisema kuwa anashangazwa na Rais Kikwete
kutokuwa tayari kuona haki za binadamu zinaingizwa katika katiba mpya na kuwa
sheria inayojitegemea na badala yake amekuwa akitaka haki za binadamu kiwe
kipengele tu ndani ya katiba.
Kwa upande wake mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa
(Chadema) inasikitisha kuona viogozi wa serikali ya CCM wanaendesha siasa
uchwala na zenye vitisho.
Wakati huo huo, Shekh Rajab Katimba kutoka katika Shura ya
Maimum alisema Rais Kikwete alipoteua tume ya Katiba alikonekana kufanya jambo
la maana na la haki lakini cha kushangaza amekuja kuitukana tume aliyoiteua
mwenyewe.
Alisema maoni yaliyomo kwenye Katiba si ya Jaji Warioba kama
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na chama chake bali ni maoni ya wananchi
ambayo yanatakiwa kuheshimiwa.
Alisema haiwezekani hata siku moja kukawa na amani kama
hakuna haki na kwamba CCM haitaki uwazi na kuwatukana waasisi wa Muungano jambo
ambalo walianza kuwatukana katika kulivunja Azimio la Arusha.
“Cha kushangaza baada ya wananchi kutoa maoni rais Kikwete
ameonesha usanii waziwazi na kuitukana tume ya Katiba pamoja na kuwatukana
wananchi ambao wametoa maoni hayo. Ulimwengu tunaokwenda nao si ulimwengu wa
kudanganyana bali ni ulimwengu wa uwazi. Tusahau utofauti wetu wa vyama, huu ni
wakati wa kutafuta maendeleo ya wananchi.
“Kiongozi yeyote anayesimama na kuchochea eti tukiwa na
serikali tatu kutakuwa na udini ni muongo mkubwa tena ni mchochezi wa
machafuko. Hiyo ndiyo tabia ya CCM kutuchonganisha sisi wananchi tulioishi kwa
kuheshimiana katika imani zetu kwa zaidi ya miaka hamsini” alisema.
Naye Bamba Juju Mjumbe wa Kamati Kuu Taifa ya NCCR Mageuzi
alisema CCM wanatapeli wananchi kwa maneno mepesi mepesi kwa hoja zisizo na
msingi huku wakishindwa kujenga hoja ya kuwa na Serikali mbili kama
wanavyotaka.
Alisema nia ya CCM ni kuendelea kuwatengenezea wananchi
umasikini kwa kuendeleza ubabe na ufisadi wao uliokithiri katika chama chao cha
kwa kutaka kuendelea kuwaficha wananchi ukweli kuhusu tunu za Taifa.
“Umasikini si kitu kinachokuja kama ajali bali ni kitu
kinachotengenezwa. Umasikini tulio nao Watanzania umetengenezwa na CCM. Hoja na
misingi ambao CCM wanashindwa uielewa ni umoja wetu.
“Kitu ambacho hatuji ni kwamba, ukishakuwa mtumishi wa
serikali hutakiwi kufungua akaunti nje ya nchi lakini hawa wenzetu CCM wanataka
waendelee kuwaibia wananchi ili wakafungue akaunti zao nje kama wanavyofanya
sasa.
“Tujadiliane kujenga hoja pale bungni lakini siyo kukataa
maoni ya wananchi. Ukosefu wa amani na haki havifungamani hata siku moja”
alisema.
No comments:
Post a Comment