masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Saturday, March 8, 2014

WANAWAKE WASITUMIE UTANDAWAZI KAMA KIGEZIO CHA MMOMONYOKO WA MAADILI: MKUU WA WILAY

 Vikundi mbalimbali vikipeleka zawadi kwa ajili ya kusaidia watoto yatima.




WANAWAKE wametakiwa kutotumia utandawazi kama kigezo cha mmomonyoko wa maadili katika jamii nchini.

Haya yamezungumzwa na Mkuu wa Wilaya ya Iringa Dkt. Letisia Warioba kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa Christine Ishengoma katika maadhimisho ya siku ya wanawak duniani iliyofanyika jana katika viwanja vya Mwembtogwa katika Manispaa ya Iringa.

Amesema wanawake wanakumbushwa wajibu zao katika jamii ili kulea familia zenye mwenendo mzuri na kutoruhusu utandawazi kuvuruga maadili hasa tamaduni za kiafrika.

Akisoma hotuba hiyo Warioba amesema wanawake wasiwaruhusu watoto wao kufanyishwa kazi kwa kunyanyasika sambamba na kulipwa ujira mdogo.

Ameikumbusha jamii kushiriki shughuli za haki katika usawa bila kumbagua mwanamke na kuhakikisha kuwa hakuna unynyasaji wa kijinsia unaofanyika katika familia.

“Kina mama tutoe maamuzi ya busara pale inapobidi. Wazazi tusibague watoto wetu katika fursa bila kumbagua mtoto wa kike kama hawezi chochote bali wapeni nafasi sawa” amesema.

Wakisoma risala mbele ya mgeni rasmi, wanawake wamesema wanaiomba jamii itambue mchango unaotolewa na wanawake mahali popote duniani.

Wamesema ndoa ndoa nyingi zimekuwa zikiathiria na janga la UKIMWI ambalo husababisha vifo kwa wenza na kuongezeka kwa kazi ya idadi ya wajane au wagane na watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi na yatima.

Hata hivyo wamesema katika Manispaa ya Iringa wamekuwa wakipeana mbalimbali kwa pupiga vita kujiingiza katika ngono, kujiepusha na mila na desturi, imani potofu na mazoea hatarisi kuhusu uhusiano wa unyumba na mambo ya uzazi.

“Elimu juu ya UKIMWI imetolewa kwa wanandoa na wafanyabiashara kutoka makundi mbalimbali ili kuwawezesha wanawake ambao ndio wanaahirika zaidi na kubeba mzigo mkubwa kwa kulea watoto yatima na wagonjwa wa UKIMWI” wamesoma kwenye risala.

Katika kutekeleza kwa vitendo msemo wa lugha ya Kiswahili usemwao “mtoto wa mwenzaio ni wako”, kupitia mfuko wa wanawake wa Manispaa ya Iringa wameweza kusaidia familia zenye kulipa karo ya shule kwa watoto 18 waliochaguliwa kujiunga na shule za sekondari jumla ya sh. 400,000/= ambapo watoto 98 walipewa mahitaji mbalimbali kama vile sukari, unga wa sembe, sabuni, madaftari na mafuta ya kupikia ambavyo vilitokana na michango ya siku ya mwanamke duniani ya mwaka 2013.

Vile vile sh. 500,000/= zilitolewa kwa ajili ya kugharamia matibabu na huduma mbalimbali ya vipimo katika hospitali ya Rufaa ya Taifa Mhimbili kwa kijana mwenye mazingira magumu mwenye tatizo la kibofu cha mkojo anayetoka katika Kata ya Ruaha katika Manispaa ya Iringa.

Katika ufumbuzi wa kudumu wa tatizo la familia zenye mazingira magumu, wanawake wamefungua akaunti ambayo itatumika kuhifadhi fedha ambazo zinatokana na michango ya watu mbalimbali ambayo hadi sasa ina jumla ya kiasi cha sh. 1,145,500/=.

Wakati wa maadhimisho hayo watumishi wa ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa walitoa msaada wa chakula wenye thamani ya Sh. 181,000/= kwa kituo cha watoto yatima cha FARAJA HOUSE Mgongo kilichopo Kata ya Nduli ambapo vikundi mbalimbali vimetoa zawadi kwa ajili ya kuwasaidia vituo vya watoto yatima.

Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yalianza kuadhimishwa tangu mwaka 1945 huku Tanzania ikianza kuadhmisha rasmi mwaka 1995 ambapo siku hii huadhimishwa 8 Machi kila mwaka.

No comments:

Post a Comment