masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Tuesday, November 12, 2013

WENZI KUAMBATANA KWENDA KLINIKI SI JAMBO LA AIBU: KABIGI

Meneja mawasiliano wa mradi wa TUNAJALI Agnes Kabigi akiongea na waandishi wa habari katika ukumbi wa Green City juu ya kampeni za "tokomeza maambukizi" hii leo.


WANAUME wametakiwa kutowapuuza wenzi wao wanapokuwa katika kipindi cha ujauzito na kuambatana nao kriniki ili kupata ushauri wa pamoja kwa ajili ya kulinda afya zao na afya ya mtoto anayetarajiwa kuzaliwa.

Imeelezwa kuwa kumekuwa na idadi kubwa ya waume wanaopuuza kuambatana na mwenzi wake aendapo kriniki kwa kigezo cha kuona aibu.

Akizungumza waandishi wa habari leo katika ukumbi wa Green City Makambako mkoani Njombe, Meneja mawasiliano wa mradi wa TUNAJALI uliochini ya shirika la kupambana na Ukimwi (USAID) Agnes Kabigi amesema suala la wenzi kuambatana kriniki si jambo la ajabu wala la aibu kwa kuwa linasaidia kuijenga familia na jamii katika suala zima la afya.

Amesema njia hiyo inasaidia kwa kiasi kikubwa kutokomeza maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (VVU) kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto na kusaidia jamii kubadili tabia.

Hata hivyo ameitaka jamii kutambua umuhimu wa kupima afya zao na kuachana na tabia zinazosababisha kuingia katika maambukizi ya VVU ikiwa ni pamoja na kuacha ngono na kutumia nafasi zao kusambaza virusi kwa makusudi.

Amefafanua kuwa huduma zinazotolewa na shirika la Tunajali ni za bure ikiwa ni pamoja na kupata vipimo vyote na ushauri bila gharama na kwamba wahudumu wamepewa mafunzo kwa ajili ya kutoa huduma zilizo bora au zisizowaudhi wa wagonjwa.

Amesema mama mjamzito apatikanapo na maambukizi wakati wa ujauzito huanzishwa dawa za kufubaza nguvu ya virusi hivyo pamoja na kupata huduma ya kumkinga mtoto asiambukizwe na virusi.

Naye Naibu Mkuu wa Mradi TCCP – JHU.CCP chini ya udhamini (ufadhiri wa serikali ya watu wa Marekani Deo Ng'wanansabi amesema elimu inayoendelea kutolewa kwa wanawake na wenzi wao juu ya maambukizi ya VVU yatasaidia katika kutokomeza maambukizi mapya matika familia na jamii.

Amesema jamii ikitoa ushirikiano katika mapambano haya, janga la Ukimwi litakwisha kutokana na jamii kuwa na elimu na mwitikio mkubwa katika kuacha kile kinachoweza kuwa ni chanzo cha maambukizi.

Amesema janga la Ukimwi siyo wimbo wa kuimba na kuusahau bali ni jambo linalopaswa kufanyiwa kazi kwa kila mmoja katika kujikinga na kupambana nalo ili jamii iwe salama katika kizazi kijacho.

“Kwa pamoja tubadilike na kujenge nguvu ya pamoja kwani viongozi pekee yao hawawezi au wahudumu pekee yao hawawezi bali sisi sote tukishirikiana tutatokomeza janga hili” amesema.

Amesema mikakati iliyopo kwa sasa ni kutumia nyenzo zote kwa ajili ya kuihamasisha jamii kujua umuhimu wa kuhudhuria katika vituo vya afya na kupata mwitikio mkubwa wa wanawake na wenzi wao kupata matibabu kwa ajili ya kukinga maambukizi hayo.

Hata hivyo amesema jukumu la kupambana na mimba za utotoni ni la kila mmoja katika familia na jamii nzima kwa ujumla.

“Kila mmoja ana jukumu hilo kwa kushirikiana na serikali kwa kuwa watoto tunaishi nao majumbani mwetu. Vile vile wazazi wanapaswa kuwaeleza watoto wao madhara ya kujihusisha na suala la mapenzi katika umri mdogo” amesema.

Kwa upande wake Dkt. Michael Msangi kutoka Wizara ya Afya Makao Makuu ambaye anafanya kazi katika kitengo cha afya ya Mama na Mtoto alisema hadi sasa utoaji huduma wa kutokomeza maambukizi ya VVU imefikia asilimia 67.

Amesema kutokana na ufadhiri wa watu mbalimbali kutoka nje unasaidia kupanua huduma kwa kiasi kikbwa ambapo hadi sasa kuna vituo 914 nchini vinavyotoa huduma kati ya vituo 5066 vilivyopo.

Amesema lengo ni kupunguza maambukizi kutoka asilimia 50 hadi kufikia asilimia 4 na hatimaye kutokomeza kabisa.

Ameeleza kuwa wanawake wengi wanakufa kutokana na maambukizi VVU na magonjwa nyemelezi kutokana na kutokujitokeza kwa ajili ya kupata ushauri na huduma.

Takwimu zinaonesha kuwa kwa mwaka 2010 vifo vya akina mama wajawazito vinavyotokana na maambukizi vilikuwa ni asilimia 11 na mwaka 2010 – 2012 vilikuwa ni asilimia 18 wakati maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto kwa mwaka 2010 ni asilimia 26 na mwaka 2012 ni asilimia 15.

Tunajali wanatarajia kuzindua mpango wa “tokomeza maambukizi” Mkoa wa Njombe ambapo unatarajia kufanyika leo katika kituo cha afya cha mji mdogo wa Makambako.

No comments:

Post a Comment