masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Tuesday, November 19, 2013

WATU WATANO WANUSURIKA KATIKA AJALI

Gari lenye namba za usajili T 301 AKX linalosadaiwa kusababisha ajali katika barabara ya Kihesa - Chuo Kikuu cha Iringa kwenye maeneo ya Mtaa wa Ngome Kata ya Kihesa katika Manispaa ya Iringa.

Gari linalodaiwa kuwa lilikuwa katika mwendo kasi na kugonga gari lililokuwa likiingia barabarani.

Watu watano wamenusurika kifo baada ya magari walioyokuwa wakisafiria kugongana huku magari hayo yakihribika vibaya.

Ajali hiyo iliyohusisha magari madogo yenye namba za usajili T 301 AKX na T 434 CEL ilitokea jana usiku majira ya saa moja usiku katika barabara ya Kihesa – Chuo Kikuu cha Iringa maeneo ya mtaa wa Ngome mbele ya duka la Ngailo.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo ni kwamba ajali hiyo ilisababishwa na dereva wa taxi T 301 AKX aliyekuwa akiingia barabarani kutoka pale alipokuwa ameegesha kwa nia ya kugeuza bila kuangalia nyumba ya gari lake.

Walisema kuwa dereva huyo aliingia barabarani kwa mbwembwe bila kuangalia pande zote kumbe nyuma yake kulikuwa na gari lililokuwa katika mwendo kasi likielekea katika chuoni kisha kumuingia kwa mbele.


Katika ajali hiyo hakuna aliyekufa wala aliyeripotiwa kujeruhiwa ambapo gari lenye namba za usajili T 434 CEL lilikuwa na watu wa nne kuhu gari lingine likiwa na mtu mmoja aliyekuwa akiliendesha.

No comments:

Post a Comment