masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Monday, November 18, 2013

MTENDAJI WA MTAA AKUMBWA NA KASHFA

Rais Jakaya Kikwete

OFISA mtendaji wa mtaa wa Ngome Eliquis Ngakonda amewatibua wakazi wa mtaa huo kutafuna fedha za michango waliokuwa wakichanga kwa ajili ya ulinzi wa sungusungu na ujenzi wa vyoo vya shule ya Mshingi Tumaini na kudaiwa kuhamishwa kinyemela ili kuficha dhahama inayomkabili.

Hayo yalibainika jana katika mkutanop wa hadhara wa mtaa huo ul;iofanyika katika viwanja vya Soko jipya la mtaa huo linaloendelea kujengwa huku mtuhumiwa huyo akishindwa kuhudhuria mkutano huo.

Katika tuhuma hiyo wamo baadhi ya mabalozi akiwemo mwanamke Prisca Mkusa ambao wanadaiwa kushirikiana na mtendaji huyo kupita mitaani kuchangisha fedha na kuziweka mifukoni mwao huku kusudio la michango hiyo likishindwa kutekelezeka.

Ajenda ya usafi wa mazingira ndiyo iliyoibua hayo baada ya wananchi kutaka kujua taratibu za kuwa na sehemu maalum za kutupa taka ili ziweze kusombwa kwa ajili ya kuyaweka mazingira safi tofauti na sasa ambapo taka zinatupwa hovyo na kuzagaa mitaani.

Wajumbe walitaka ufanyike utaratibu wa kujenga sehemu maalum za kutupa taka ili gari likifika ziweze kupakiliwa ndipo ilipoibuka hoja ya kujua makusanyo ya michango ya sungusungu ili ufanyike utaratibu wa kuona namna sehemu hizo zitakavyo jengwa.

Wajumbe walitaka mabalozi waeleze michango yao walikoiweka kutokana na sungusungu kutofanya kazi na kuwalazimu mabalozi waliokuwepo kuwaeleza wananchi kuwa walimkabidhi Ngakonda na Mkusa ambao walisema ndiyo wasimamiaji.

Hata hivyo ikagundulika baada ya kujua walichokifanya wakaukimbia mkutano huo ikashindikana kupata majibu haraka na wakalazimika kuwaagiza baadhi ya viongozi wa mtaa huo akiwemo mwenyekiti kuhakikisha wanawaita watuhumiwa na kuita mkutano wa dharura mwishoni mwa mwezi huu.

Mabalozi waliokuwepo walitaja fedha walizomkabidhi Ngakonda na Mkusa na kufikia zaidi ya shilingi laki mbili japo kuwa huenda zikaongezeka kutokana na mabalozi wengine kutokuwepo katika mkutano huo wanaodaiwa kukusanya fedha nyingi zaidi.

Ubadhilifu huo ulikuja baada ya ofisa mtendaji huyo akishirikiana na viongozi wa chama cha Mapinduzi (CCM) kumsimamisha uenyekiti Elizabeti Mkayula aliyeonekana kufuatilia kwa ukaribu masuala ya kijamii ambayo yanahusu fedha za wananchi.

Hata hivyo ilielezwa kuwa mtendaji huyo alikuwa anawatumia zaidi vinara wa kuchangisha michango hiyo ambao ni Prisca Mkusa na Abubakari Muumba ambao baada ya kuchangisha fedha hizo kwa kushirikiana na ofisa huyo walizitia kwenye mifukoni mwao huku wananchi wakiambulia patupu.

Baadhi ya wajumbe waliokuwepo kwenye mkutano huo waliongea na mtandao huu baada ya mkutano kuwa tatizo ni kwamba ofisa huyo anafanya kazi za CCM badala ya kazi anayopaswa kufanya ndiyo maana anafanya udanganyifu wa wazi kwa kujidai kuwa hatafanywa chochote kwa kuwa wapo wa kumkingia kifua.

“Unajua tatizo linalokuja hapa! Watendaji wengi wanafanya kazi za chama badala ya kazi wanazotakiwa kuzifanya. Viongozi wa CCM walimsimamisha huyu mama uenyekiti kwa sababu alikuwa kikwazo kwao wanapotaka kuiba maana huyu mama ni mkali na ni muwazi lakini baada ya kufanikisha kuiba walichokusudia sasa ndiyo wanamrudisha madarakani tena. Hata huu ujenzi wa soko haturidhiki nao kwa sababu mambo wanayoyafanya ni uchafu mtupu. Tunaumia sana sisi wanyonge.

“Mimi ni mwanachama wa CCM lakini kwa hili, sipo tayari kulifumbia mamcho. Tatizo la CCM, mtu akiwa mkweli katika chama ni adui lakini mtu mwizi na muongo katika chama ni hazina kwa sababu hiki chama tukubali tu kuwa kimekuwa ni chama cha wezi, mafisadi na wahuni. Chaguzi za miaka ijayo hatuponi maana tumeshaharibu kila kona” kilisema chanzo chetu kilichoomba jina lisiandikwe.

Kuna tetesi kuwa mtendaji huyo alihamishwa na nafasi yake amebadili mtendaji mwingine Gannzan Godson jambo ambalo wqnanchi wanataka kama ni kweli wanataka makabidhiano yao yafanyike mbele yao ili tuhuma zinazomkabili azijibu.

Dodson alipoulizwa juu ya ukweli huo alikiri kuwa ni kweli na kwamba hajakabidhiwa vitendea kazi japo kuwa ameambiwa aendelee kufanya kazi katika mtaa huo.

Wakati huo huo bwana afya wa Kata ya Kihesa Gaudence Haule ameingia katika kashfa ya kuwahadaa wakazi wa mtaa huo huku wananchi wakiahidi kumshughulikia pale atakaposhindwa kutimiza ahadi zake kwenye mtaa.

Katika mkutano huo ambao wananchi walionekana kuwa na jazba juu ya viongozi waongo, bwana afya wa Kata hiyo alikuwa na maswali ya kujibu lakini hakuwepo kwa kile kilichoelezwa na wananchi kuwa amekimbia kujibu uongo aliowadanganya.

Mkutano huo uliazimia kuwa mwishoni mwa mwezi Novemba aletwe ofisa huyo, ofisa mtendaji wa kata, mabalozi ambao hawakuhudhuria mkutano wa juzi ili wawekwe kapuni, diwani wa kata hiyo, mwenyekiti wa Kamati ya Shule ya Msingi Tumaini na Mwalimu Mkiuu wa shule hiyo ili wasaidie kutoa ufafanuazi wa mambo mbalimbali.

Mkutano huo uliahilishwa hadi Desemba Mosi mwaka huu utakapofanyika kwa ajili ya kupata majibu kwa watuhumiwa hao.


No comments:

Post a Comment