| Mgunge wa Iringa mjini Peter Msigwa (CHADEMA) aliyevaa kofia akiongea na waandishi wa habari katika ofisi ya Chadema Wilaya na kulia kwake ni Katibu wa chama hicho Wilaya Suzan Mgonukulima. |
| Diwani wa Kata ya Mivinjeni Frank Nyalusi (CHADEMA) akiongea na waandishi wa habari katika ofisi ya Chadema Wilaya na kulia kwake ni Katibu wa Wilaya Chadema Suzan Mgonukulima. |
MBUNGE wa Iringa mjini
Peter Msigwa (CHADEMA) amekemea vikali vitendo vya kupiga wananchi na kung’oa
bendera za Chadema vinavyofanywa na vijana wa Chama cha Mapinduzi (Green guard)
wakati wa ukimbizaji wa bendera ya chama hicho na picha ya Rais Kikwete.
Msigwa ametoa rai kwa
jeshi la polisi Mkoa wa Iringa kutofumbia macho vitendo hivyo na badala yake
waongeze ulinzi ili kuepusha vitendo vinavyoweza kusababisha uvunjifu wa amani.
Amesema kuijiunga na
chama ni hiari ambapo kila mtu yupo huru kuchagua chama anachopenda kujiunga na
kwamba siasa chafu zinazofanywa na CCM ni zisifumbiwe macho kwani ni chanzo
kikubwa cha uvunjifu wa amani.
Akiongea na waandishi
wa habari katika ofisi ya Chadema Wilaya leo, Msigwa amesema kukaa kimya
hakumaanishi kuwa Chadema imeshindwa la kufanya ila ni ustaarabu tu ambao
wameamua kuufanya ili kutoa nafasi kwa vyombo vya ulinzi na usalama kuthibiti
vitendo hivyo.
“Mimi napenda kuwaasa
ndugu zetu wa chama cha mapinduzi kuwa tufanye siasa za ustaarabu. Kila
wanakokwenda wakikimbiza bendera na picha wanapiga watu. Huo ni utarataibu
gani? Tusingependa kujibu kwa vitendo hivyo wanavyovifanya bali tunaomba
wajirekebishe” amesema.
Amesema vijana
wanaotumika na chama cha mapinduzi kupiga watu na kung’oa bendera za Chadema
waache mara moja vitendo hivyo bila kulazimishwa.
Amesema vitendo vinavyofanywa
na vijana hao huku viongozi wao wakikaa kimya vinaamaanisha ni mipango mikakati
walio nayo katika chama kufanya fujo kwa watanzania wasio na hatia.
“Uwezo wa kujirudishia
tunao lakini tumeamua kunyamaza kimya si kwa sababu tunawaogopa bali ni
ustaarabu tu. Ila vitendo hivi vikiendelea hatutasita kujilinda na kulinda
bendera zetu ambazo zinaharibiwa bila sababu” amesema.
Wakati wa ukimbizaji wa
bendera katika halmashauri ya Iringa, vijana wa CCM walipiga watu katika
vjijiji vya Ifunda na Ihemi jana wakati Nduli na Isimani nako watu wakipigwa
kwa madai kuwa wamevaa nembo za Chadema huku wakiong’oa bendera za Chadema
katika Wilaya ya Kilolo ambapo mwenyekiti wa vijana (UVCCM) Wilaya ya Kilolo
Sifuni Makongwa akituhumiwa kuratibu mpango huo.
Makongwa alikamatwa
katika Kata ya Ilole aking’oa bendera za Chadema jambo alilolazimika kuomba
msamaha kwa vijana waliokerwa na vitendo hivyo na kuachiwa huku akiahidi kuwa
atalipa gharama za bendea hizo.
Sambamba na hilo Msigwa
amesema michango ya Mwenge inayoendelea mjini hapa ni ya wizi kwa kuwa haina
tija yoyote kwa wananchi na kuwataka wananchi wasilazimishwe kutoa mchngo bali
waamue wenyewe.
“Mwenge hauna tija
yoyote; wananchi msilazimishwe kutoa mchango huo kwa sababu kuna watu
wamejitengenezea ulaji. Tumieni hela zenu katika shughuli za msingi, changieni
shughuli za maana tu. Si kwamba tunakataa michango lakini mchango wa Mwenge
hauna maana. Tutasimama na kuvalia njuga pale tunapoona kuna tija ili wananchi
tuchangie lakini michango isiyo na maana hatutaki iwaumize.
“Na ieleweke kuwa
shughuli za kuchangia au kutokuchangia siyo za wanasiasa bali ni za viongozi serikalini.
Ipo michango inayohidhinishwa na serikali Kuu na ipo michango ambayo watu
wachache wanaianzisha kwa maslahi yao wenyewe. Epukeni michango ya unafiki kwa
kuwa itawaumiza” amesema.
Hivi karibuni
wafanyakazi wa taasisi mbalimbali katika Manispaa ya Iringa na halmashauri ya
Kilolo wamelalamika vikali juu ya michango ya Mwenge wanayolazimishwa
kuchangia.
Pamoja na malalamiko
hayo, wameeleza kuwa japo kuwa kila mwaka huchangia, kwa mwaka huu imekuwa
tishio kwa kutakiwa kuchangia sare kwa shilingi elfu 25 huku mchango wa Mwenge
Pekee ukiwa ni shilingi 1,000/=.
Vyanzo vyetu mbalimbali
vimeeleza kuwa kuna kiongozi ambaye amebuni kufanya biashara hiyo na kushawishi
wakuu wa idara kupitisha ili waweze kuwakamua wafanyakazi kinguvu huku wakijua kuwa kipato chao bado hakikidhi
mahitaji.
Taarifa zinasema kuwa
wapo baadhi ya wakuu wa idara ambao wamekuwa wakitumika kwa ajili ya kuwaumiza
wafanyakazai wenzao kwa kutaka kusifiwa na kupandishwa vyeo jambo ambalo
limekuwa likiwaumiza wafanya kwa kiwango kikubwa.
Wakati wafanyakazi
waliopo ndani ya Manispaa ya wakilalamika na kulaani, wafanyakazi waliopo ndani
ya Halmashaur ya Kilolo wamesikitishwa na kitendo cha kukatwa mshahara kwa
madai ni michango ya Mwenge.
Vyanzo mbalimbali
kutoka Kilolo vimeeleza kuwa wafanyakazi hawakushirikishwa juu ya michango hiyo
lakini wameshangazwa kuona mshahara wao ukiwa pungufu.
“Watu wana mambo ya
ajabu kweli, wamekata mshahara lakini tulipokwenda kuhoji mishahara imekatwa
kwa sababu gani eti wanatwambia michango ya Mwenge! Mbona huu ni unyonyaji
mkubwa sana? Watu wanatumia mwenge kuiba mishahara ya watu.
“Tukiendelea kwa mtindo
huu sijui tutafika wapi! Mbona nchi hii imekuwa kama ya watu waigizaji wasio na
ubinadamu? Mwalimu atakumbukwa kwa mengi” kilisema chanzo chetu.
Wakati wafanyakazi wa
Manispaa wakitakiwa kuchanga kiasi cha shilingi 26,000/= kwa ajili ya Mwenge,
wafanyakazi wa Kilolo wamekatwa 10,000/= katika mishahara yao kila mmoja.
Hata hivyo mtandao huu umefanikiwa kunasa barua ambayo imeandikwa na kusambazwa kwenye taasisi mbalimbali na
kusainiwa na Christina Nyato kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa yenye
Kumbukumbu namba IME/E.10/34/VOL.IV/27 kuwata watumishi kutoa michango hiyo.
Oktoba 14 mwaka huu Mwenge
wa Uhuru unatarajiwa kuzimwa kitaifa katika Mkoa wa Iringa.
No comments:
Post a Comment