masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Sunday, September 8, 2013

SEKONDARI HATARINI KUANGUKA

Mistari inayoonekana katika picha ni nyufa za jengi hilo ambapo kiti kinatengana na ukuta hali inayoweza kusababisha jengo hilo kuporomoka wakati wowote.



JENGO la sekondari ya Kata ya Kimala Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa lipo hatarini kuanguka kabla ya kumalizika kujengwa kutokana na kile kinachodaiwa kujengwa chini ya kiwango huku viongozi wa Kata akiwemo Diwani wa kata hiyo wakibebeshwa lawama za matumizi mabovu ya michango ya wananchi.

Wakizungumza na mtandao huu kijijini hapo kwa nyakati tofauti, wananchi hao wameonesha kusikitishwa na michango yao kutumika vibaya huku wakikosa ufafanuzi wa njia zilizotumika kumpata mkandalazi wa jengo hilo.

Telaki Ndenga mwananchi wa kijiji cha Kimala ameliambia gazeti hili kijijini hapo kuwa wananchi wamekuwa wakipuuzwa na viongozi pale wanapohitaji ufafanuzi juu ya jengo hilo kuonesha dalili za kuanguka huku wakisukumiwa matusi.

Alisema kila wakati wamekuwa wakitoa malalamiko yao kwa ofisa Mtendaji wa Kata hiyo na kwa diwani wao lakini wamekuwa na kigugumizi cha kutoa ufafanuzi juu ya suala hilo na badala yake kuitwa wajinga.

“Suala hili ni la muda mrefu tu kwani tuliliona mapema kabisa kuwa jengo linalojengwa kwa ajili ya shule ni bomu kwa watoto wetu watakaosoma hapo; tumetoa malalamiko yetu kwa mtendaji wa Kata na diwani lakini majibu hatupewi.

“Tatizo linaloonekana hapa diwani na mtendaji wao ndiyo kila kitu. Hawashirikishi kamati ya ujenzi ila wao wanachokiamua ndicho wanachotaka kifanyike. Baada ya kuona hali inazidi kuwa mbaya tulichukua hatua ya kutoa malalamiko yetu kwa Mkuu wa Wilaya ila mengine alitujibu na mengine akatuambia kuwa anayafanyia kazi” alisema.

Rudio Mtenga mmoja wa wanakamati ya ujenzi wa shule hiyo alisema kuwa wanankamati wamedharauliwa na viongozi hao ambapo wanafanya kazi kwa kujinufaisha badala ya maendeleo ya wananchi wote wanaotoa michango yao kwa ajili ya ujenzia wa shule hiyo.

Alisema wakati mwingine vikao vya kamati ya ujenzi vinavyofanyika ni vya kihuni kwa kile alichoeleza kuwa vimekuwa vikiitishwa na ofisa mtendaji wa Kata na diwani ambao wanajihusha moja kwa moja na matumizi machafu ya pesa za wananchi.

Alieleza kuwa wakati vikao hivyo vikiitishwa, wanakamati wamekuwa hawana hoja kwa kile walichokuwa wakielezwa kuwa hawajapewa semina na kutakiwa kukaa kimya.

“Tulipohoji diwani alitujibu kuwa hatujapewa semina kwa hiyo tutapata nafasi ya kuhoji tutakapopata semina. Tangu hapo wamekuwa wakichukua michango kwa wananchi bila kutushirikisha sisi wanakamati.

“Desemba 25, 2012 tulikubaliana kuwa kamati ipewe majukumu yake tukianza na utafutaji mbao lakini tulipotafuta mbao na kurudisha majibu ili tupewe fedha ya kulipa tukaambiwa mbao zimeshanunuliwa. Tulipouliza ni nani kanunua wakati kazi hiyo ni ya kwetu, diwani alisema juu ya mbao tusiulize ila tuendelee na mambo mengine japo kuwa kamati walisema bila kujulikana mnunuzi wa mbao hizo kamati haiwezi kuendelea kufanya lolote” alisema.

Alisema kutoka hapo diwani na ofisa mtendaji wakatumia nguvu kujengea mbao hizo japo kuwa zilikuwa chini ya kiwango kwa mujibu wa ujenzi wa jengo hilo na kwamba tangu hapo hawajawahi kushirikisha kamati shughuli yoyote inayoendelea.

Boniface Kasuga mwanakamati wa ujenzi wa shule hiyo alisema michango ya wanachi inatumiwa na watu wachache kwa manufaa ya familia zao bila kujali kuwa ni kuwaumiza wananchi wanaojitoa kwa ajili ya maendeleo ya elimu.

Alisema kuwa fedha zinazotolewa na wananchi kwa ajili ya ujenzi hazifikishwi kwenye kamati kwa ajili ya kupangia bajeti na badala yake diwani na ofisa mtendaji wa kata wamekuwa wao ndio wanakamati na ndio watendaji.

“Pia fedha inayotoka halmashauri sisi wanakamati tunatakiwa tuandikie bajeti lakini wao hawafanyi hivyo na tunaambiwa tu kuwa hela hizo wanazichukua na kwamba zikichukuliwa zitafanya kazi gani hatuambiwi wala hatujui na pia hatujui wanatumia muhtasari gani kuchukua fedha hizo. Hapo ndipo tunapoona mtendaji  wa kata na diwani hawatutendei haki” alisema Kasuga.

Naye mjumbe wa Kamati hiyo Sadick Kasuga alisema kuwa mafundi wanaojenga jengo hilo linabomoka ni ndugu zake na diwani.

Alisema waliligundua hilo mapema tu kwenye kikao cha kwanza kwa ajili ya kuanza kujenga jengo hilo na kwamba walitilia shaka juu ya uhalali wa jengo hilo kutokana na mafundi hao kuwa ndugu wa diwani.

“Sisi wanakamati tunaulizwa na wananchi juu ya maendeleo ya jengo hilo na kwamba ni kwa nini linabomoka lakini tunashindwa kuwajibu kwa sababu kila kitu wamejihodhisha viongozi bila kutushirikisha sisi wanakamati.

“Tunachopenda kama wataalamu wa majengo wangefika hapa ili waone hali halisi na wathaminishe kwa jengo lenyewe na gharama zilizotumika wangejua kabisa kuwa tunachokizungumza sisi siyo uzushi bali nikitu cha kweli” alisema.

Hata hivyo alisema kuwa waliandika barua kwa ofisa mtendaji wa kata kuomba maandamano ya amani kuelekea sehemu ya jengo ili wananchi watoe kero na hisia zao lakini mtendaji huyo hakuwa tayari kuruhusu maandamano.

“Wananchi waliandika barua ya kuishtaki kamati ya ujenzi ambayo nayo haikujibiwa hadi leo. Tukihoji matumizi wanatuambia kuwa Mkurugenzi amesema hana fungu la kuendesha semina. Chakushangaza vifaa vya ujenzi vinaanza kukarabati jengo ambalo halijaisha badala ya kuendelea kujenga majengo mengine. Hii ni aibu kubwa hata kwa wenzetu wanaoliona jengo hili” alisema.

Mtandao huu umefanikiwa kufika katika eneo la jengo hilo na kushuhudia jengo hilo likiwa na nyufa nyingi kala sehemu pamoja na kuwa linaendelea kujengwa huku nyufa zingine zikiwa zimezibwa na kupasuka tena na kulazimika kujengwa nguzo nyuma ya jengo ili kuzuia lisiporomoke.

Hata hivyo, Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Gerald Guninita alipoelezwa na wananchi katika mkutano uliofanyika Agosti 28, mwaka huu alisema atalifanyika kazi na kwamba majibu yatatolewa ambapo alitoa mifuko 50 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa shule hiyo.

Ofisa mtendaji wa Kata hiyo Richard Ngungulu alipotafutwa ofisini hapo hakuweza kupatikana licha ya ofisi kuwa wazi na kutokuwepo mtu yeyote na lakini alipotafutwa kwa simufua.

“Huo ni uongo tena ni uzushi. Usiamini maneno ya watu, hao waliokuambia hivyo ni waongo tu” alisema


Naye diwani wa kata hiyo Mejusi Mgeveke alipotafutwa hakuweza kupatikana kwa kile kilichoelezwa kuwa yupo kijijini kwake Idunda ambako hakuna mawasiliano ya simu.

No comments:

Post a Comment