![]() |
| Kristie Trup na Katie Gee |
Polisi nchini Zanzibar wameahidi kutoa zawadi ya shilingi
milioni 10 za Tanzania kwa yeyote atakayetoa taarifa zitakazopelekea kukamatwa
kwa watu waliowashambulia wasichana wawili waingereza kwa Tindikali.
Wasichana hao kutoka London,
Kirstie Trup na Katie Gee, walirushiwa Tindikali kwenye nyuso zao walipokuwa
wanatembea mjini Jumatano Jioni.
Serikali ya Zianzibar ndio
itakayotoa zawadi hiyo.
Polisi wanasema kuwa hizo ni
pesa nyingi sana kisiwani Zanzibar.
Kirstie Trup na Katie Gee, wote
wenye umri wa miaka 18 kutoka London, walipelekwa hospitalini nchini Tanzania
baada ya kushambuliwa Mashariki mwa kisiwa hicho.
Inaaminika kuwa walitoka
Tanzania kuelekea Uingereza Alhamisi usiku.
Mama za wasichana hao, Rochelle
Trup na Nicky Gee, walielezea kughadhabishwa mno na shambulizi hilo ambalo
sababu yake haiwezi kujulikana na ambalo halikuchochewa kivyovyote.
Walishambuliwa na wanaume
wawili waliokuwa kwenye pikipiki.
Polisi walisema kuwa
walirushiwa Acid kwenye nyuso zao, kifuani na kwenye mikono yao walipokuwa
wanatembea mjini .
Mwandishi wa BBC anasema kuwa
waliowashambulia walitoroka na polisi hawajui kwa nini wanawake hao walilengwa.
Mama za wasichana hao walisema
kwenye taarifa yao kuwa walighadhabishwa mno na shambulizi hilo na hawaelewi
kwa nini wasichana hao walishambuliwa ili hali walikwenda Zanzibar kwa nia
njema.
''Tunashukuru kwa wale
wanaotaka kujua kinachoendelea lakini tungeomba vyombo vya habari vituwache kwa
sasa hadi tutakapokutana na watoto wetu,'' alisema msemaji wa familia za
wasichana hao.
Wasichana hao walikuwa wamekaa
Zanzibar kwa muda wa wiki mbili ingawa walitarajiwa kuwa huko kwa wiki tatu,
kupitia kwa kampuni ya usafiri ya i-to-i Travel, ambayo ilisema inafanya kila
iwezalo kuwarejesha nyumbani Uingereza.
Chanzo: bbc swahili

No comments:
Post a Comment