| Baadhi ya watu mbalimbali wakisikiliza mjadala wa amani katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo jana. |
Amir na Mbashiri Mkuu wa Jumuiya
ya Waislamu Waahmadiyya Tanzania Sheikh Tahir Mahmood Chaudhry amesema Dunia
inapita katika ghasia na migogoro ambavyo sababu zake ni uchumi, tofauti za
kisiasa na kidini.
Alisema hayo jana katika mkutano
wa kujadili amani uliofanyika mkoani
hapa katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo uliojumuisha dini na madhehebu
mbalimbali pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali.
Alisema kuwa kumekuwa na
kutafsiriwa vibaya na watu mbalimbali wakiwamo waislam wenyewe kwa neno jihadi
ambalo wengi wanalitafsiri kama ni kuingia vitani.
“Kwa bahati mbaya inapotajwa
jihadi ndani ya vichwa vya waislam wengi na wengi wasio waislamu wanachokidhani
wao ni vita tu, kwamba jihadi maana yake ni waislamu kuwa tayari muda wowote na
kwa njia yoyote kupambana kwa vita na wasio waislamu” alisema.
Alisema uelewa huu umezua tatizo
kubwa miongoni mwa matatizo ya dunia ya leo ambapo baadhi ya makundi ya
waislamu hutumia njia zisizo halali kama za wale wanaojilipua mabomu,
wakiyalipua mabomu kwa jina la dini katika kuwaua na kuwajeruhi wasio waislamu.
Amekemea vikali vitendo hivyo
kuwa ni ukatili usiokubali popote ndani ya waislamu na wote kwa ujumla na
kwamba kutokana na mwenendo huu wa hovyo wa baadhi ya waislamu kufanya vitendo
hivyo kwa jina la dini, wanaleta taswira potofu na sasa imejengeka ndani ya
nchi zisizo za kiislamu na matokeo yake baadhi ya sehemu za jamii zinaongea kwa
uwazi.
Alisema vitendo hivi vimeunda hali ya kutokuwa na imani ndani ya
mioyo ya watu na kujenga chuki miongoni mwa watu wasio waislamu kwa waislamu na
kwamba kutokana na mwenendo huu wa waislamu wachache, badala ya mambo kuboreka
, athari hasi za wasio waislamu zinazidi kuwa mbaya siku hadi siku.
“Kwa vile leo kwa fadhili za
mwenyezi Mungu takribani sehemu kubwa ya dunia kuna uhuru wa kuabudu, zikiwemo
sheria za umoja wa mataifa na hata hapa nchini petu, basi sababu ya kufikiriwa
jihadi kwamba ni vita tu inakuwa haipo.
“Leo jihadi kubwa kwa waislamu ni
kujaribu kuyaelewa na kuyatekeleza mafundisho ya dini pamoja na kuyafikisha kwa
wengine yaani kufanya mahubiri kwa hekima na mawaidha mema na kujadiliana na
wasio waislamu kwa wema” alisema.
Alifafanua kuwa ili dunia iwe na
amani ni lazima watu wafanye uadilifu; viongozi wanatakiwa kuwa waadilifu kwa
wanaowaongoza na wananchi wenyewe wanatakiwa kuwa waadilifu kwa mamlaka za nchi
zao na baina yao wenyewe kwa wenyewe bila kuwekeana fitina, kinyongo au hasira.
Alisema uhuAlisema matukio haya yanaonu wa kuabudu udumishwe ili
watu waweze kuchagua kile wanachokitaka kwa kuwa mara kadhaa kuwanyima watu
uhuru wa kuabudu kumekuwa ni kikwazo kikubwa cha kuwepo amani duniani.
Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa
Iringa Ramadhani Mungi alisema amani itapatikana pale watu watakapo hakikisha
hakuna vurugu, hakuna migogoro, hakuna hofu ya vurugu, kukosekana maadui au
uadui, endapo hakuna chuki na kutokuwepo ugomvi.
Wakati Mku wa Mkoa wa Iringa
Christine Ishengoma akifungua mkutano huo alisema kuna matukio yaimu siyo ya
kawaida ya uvunjifu wa amani ambayo ni dalili mbaya kuwaenzi waasisi wa amani
duniani.
Alisema ili kuwa na amani watu
wanapaswa kuwa watulivu kuanzi kwenye familia zao ili kuwaheshimu wengine bila
kujali tofauti za kiitikadi za kisiana na kidini.
“Tudumishe amani ili kizazi
kijacho kiweze kufurahia amani na upendo na kudumisha amani. Viongozi
mbalimbali wa dini na madhehebu hubirini amani” alisema.
No comments:
Post a Comment