| Wanafunzi wa shule ya sekondari ya wasichana Iringa wakitumia teknolojia ya mtandao kusoma katika maktaba ya Global Outreach. |
| Wanafunzi wa shule mbalimbali za sekondari wakisoma katika maktaba ya kidijitali. |
Jimbo Katoliki la Iringa
limedhamiria kuwajibika katika kuboresha elimu kwa njia ya mtandao wa kidigitali
katika shule mbalimbali pamoja na watu binafsi wenye nia ya kujiendeleza.
Kupitia maktaba ya kidijitali ya
Global Outreach iliyopo Kichangani, wenye ulemavu wa kuona na kusikia
watanufaika kwa kuwa na teknolojia ambayo itawawezesha kupata kile
wanachokitaka kupitia teknolojia hiyo.
Akizungumza na mwandishi wa
makala haya, Mkurugenzi wa Global Outreach Tanzania Sixtus Kanyama anasema licha
ya changamoto mbalimbali wanazozipata, mwitikio wa waalimu na wanafunzi
unaridhisha kwa kuitumia maktaba hiyo.
Anafafanua kuwa matumizi ya
maktaba ya kidigitali inarahisisha kupata masomo kwa muda mwafaka bila kusubiri
vitabu vilivyochapwa kwa kuwa kitabu ambacho kingepatikana darasani na kutumiwa
na wanafunzi watatu au wanne kinapatikana kwenye mtandao na kutumika na
mwanafunzi mmoja kwa muda mwafaka ikiwa ni pamoja na vitabu vipya ambavyo vinakuwa
havijamfikia mwanafunzi na mwalimu.
“Nianze kwa kuwapongeza wanafunzi
na walimu ambao wametambua umuhimu wa maktaba hii. Muamko wao ni mkubwa kwa
pande zote mbili kwa maana ya waalimu na wanafunzi. Muamko wa wanafunzi hadi
sasa unafikia asilimia 50 (50%) wakati walimu ni asilimia 25 (25%)” anasema
Kanyama.
Licha ya muamko huo anasema wapo
baadhi ya walimu na wanafunzi ambao wanaamini kutumia machapisho pekeke (had
materials) ndiyo njia sahihi zaidi.
Anakwenda mbali zaidi na kusema
kuwa, pamoja na vitendea kazi kuwepo bado watu wengi hawajaichangamkia
teknolojia mpya ambayo jibu la maswali magumu yanayoikabili sekta ya elimu.
“Inaonesha kuwa wanafunzi wengi
na waalimu wangekuwa na muamko mkubwa zaidi wa kuitumia teknolojia hii mpya,
sekta ya elimu inaweza kukua kwa kiwango kikubwa kwa sababu teknolojia yetu
inajibu na kutatua matatizo manne likiwemo la uhaba wa vitabu, uhaba wa walimu,
mbinu mbovu za ufundishaji na wanafunzi kubaki kama wapokeaji tu wa kile kinachofundishwa darasani kwani
sasa wanapata nafasi ya kujitegemea” anasema.
Mradi huo ambao uko chini ya
Kanisa Katoliki jimbo la Iringa unadhamiria kusambaa kote nchini kutokana na
mwitikio na mapokeo ya wengi wanaoonekana kuwa na uhitaji wa kutumia teknolojia
hiyo kielimu.
Kanyama anamueleza askofu wa
jimbo la Iringa Mhashamu Tarcisius Ngalalekumtwa kuwa ni wa aina yake katika
kupigania elimu kwa kujitoa kwa kila namna.
“Baba askofu Ngalalekumtwa ni mtu
wa aina yake. Hili halina mpinzani kwa wale wanaomfahamu. Ni mtu anayependa elimu
na anatumia muda wake mwingi kwa ajili ya kuhakikisha elimu inasonga mbele hasa
katika jimbo hili” anasema.
Anatoa mfano wa shule wanachama
wa kutumia maktaba ya kidigitali ya Global outreach katika mitihani kuwa ni
Mafinga Seminari iliyopo katika Wilaya ya Mufindi, Shule ya Sekondari ya
Bomalang’ombe, Image zilizopo katika Wilaya ya Kilolo, shule ya Wasichana
Iringa (Iringa girls) na shule ya sekondari ya Lugalo zilizopo katika Manispaa
ya Iringa.
“Kupitia shule hizo, zimekuwa
kipimo kwetu kwa kuwa na matokeo mazuri. Kipimo chetu kingine ni kwamba,
wanafunzi ambao wamekuwa kama viongozi wa wenzao wapo vyuo vikuu” anasema.
Kanyama anasema hivi sasa kuna
utaratibu wa kupanua wigo wa utoaji elimu kwa watu mbalimbali wenye ulemavu ili
kuwawezesha kupata kile ambacho wengine wanakipata ambapo kwa sasa wenye ulema
wa kuona wananufaika kwa kusikiliza kitu kile kile ambacho wengine wanakisoma.
Anabainisha kuwa baadhi ya wadau
wa elimu wameridhika na huduma hiyo na kuamua kutoa msaada kwa ajili ya
kuwawezesha wenye ulemavu kupata elimu kwa njia ya mtandao.
“Kuna asasi moja inaitwa “Iringa
Living Lab” ambayo iko chini ya shirika la Tanza ICT tunafanya nao kazi kwa kwa
ajili ya kuboresha maktaba ya kidigitali kwa matumizi ya wenye ulemavu ambapo
kila siku ya ijumaa tunatoa mafunzo kwa wenye ulemavu wa wasiosikia ili waweze
kupata ujuzi wa kutafuta kile wanachokihitaji kwenye mtandalo.
“Kwa wasioona tunawatengenezea
masomo kwa njia ya sauti ili waweze kusikiliza na kujua nini kinaelezwa”
anasema.
Pia anasema kuwa wapo katika
mpango wa haraka kuwatengenezea utaratibu wenye ulemavu wa kuona na kusikia wa
kuwawezesha kufanya mitihani ya maarifa (QT) kama wengine wanavyo fanya ili
wasijione wanyinge na watu waliosahaulika.
Akieleza changamoto wanazokumbana
nazo, Kanyama anasema walimu wa Wakuu wa shule wameelewa umuhimu wa maktaba ya
hiyo lakini bado kuna hawajawajibika kwa kiasi kikubwa kuwahamasisha walimu wao
katika shule zao na kwamba asilimia 75 (75%) ya walimu bado wanaamini vitabu.
Pia anasema wapo baadhi wanafunzi
ambao wanatumia vibaya teknolojia hii kwa kuwa wengi wanapoingia wanakuwa na
lengo la kuangali mambo machafu kwenye mtandao badala ya masomo japo kuwa
katika upande wa maktaba ya kidigitali wamefanikiwa kufunga mambo hayo na
kumsaidia mwanafunzi kujikita katika masomo tu na si vinginevyo.
| Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Lugalo wakiwa katika maktaba ndogo ilipo shuleni hapo inayosimamiwa na Global Outreach wakijisomea kwa njia ya mtandao. |
Mary Lugusi ni miongoni mwa
wanafunzi ambao wamenufaika na maktaba hiyo na sasa anasoma katika Chuo cha
usimamizi wa fedha (IFM)licha ya wanafunzi watano walionufaika na maktaba hiyo
kuwa vyuo vikuu hapa nchini.
Anazungumza na mwandishi kuwa
ukaribu wake na Global Outreach ndio ulimuwezesha kupata nafasi ya kujiunga na
chuo hicho kwa kuwa alikuwa akipenda sana kusoma kwa kutumia kompyuta.
“Mwaka 2010 nilijiunga na maktaba
ya Global Outreach na kutumia maktaba ya kidigitali kusoma masomo mbalimbali.
Nilipata upeo mkubwa kwa kuwa kila nilichokuwa ninakitafuta nilikuwa nakipata
pamoja na rejea zake ambapo nilipata hamu kubwa ya kufungua kujisomea.
“Maktaba ya kidigitali ina vitabu
ambavyo ni msaada mkubwa. Kuna mfumo mzuri wa vitabu vya hesabu na lugha nah ii
makta inasaidia kwa wale wanaopenda kufanya mambo yasiyo na maana wasifanye kwa
sababu ni ya kisasa zaidi ni maalum kwa taaluma tu ” anasema Lugusi.
Anasema upekee wa maktaba hiyo
unaonekana pale wanapokuwa wanajihusisha na wanafunzi kwa kiwango kikubwa bila
malipo na kwamba maisha yake kwa sasa ni teknohama.
“Kila kitu kikitumika ipasavyo
kina faida lakini sisi watu huwa tunatumia kwa ulimbukeni na kusababisha kitu
ambacho kinakuwa msaada kugeuka kuwa ni kitu cha anasa. Haya ni matumizi mabaya
ya akili zetu na fikra zetu” anasema.
Anasema kuna haja ya watu
wanaotoa huduma za mtandao kuhakikisha wanakuwa na usimamizi kwa watu wanaopata
huduma ili kuhakikisha wanafanya kile ambacho kinajenga maadili na akili ya mtu
badala ya watu kutumia kwa upuuzi na mambo ya aibu.
Anafafanua kuwa ni jambo la aibu
na la kufedhehesha kuona hata wasomi wa vyuo vikuu ambao wanatakiwa kuwa kioo
kwa watu wengine wanatumia mitandao vibaya badala ya kutumia katika elimu na
maendeleo.
Anasema taasisi na mashirika
mbalimbali yanayotoa huduma za kimtandao wawe na mipaka katika utoaji huduma
kwa jamii ili kulinda maadili.
“Kutokana na Global Outreach
nilianza kujifunza mawasiliano na teknolojia (IT) ndiyo maana nilifanikiwa
lakini usije ukafikiri kuangalia picha chafu na takataka zingine unaweza
ukapata akili. Hata siku moja! Huo utakuwa ujinga wa kudumu” anasema.
No comments:
Post a Comment