masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Tuesday, July 9, 2013

WAANDISHI WA HABARI, WANAHARAKATI NA VIONGOZI WA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI WATAKIWA KUUNGANISHA NGUVU

Onesmo Olengurumwa



WANDISHI wa habari, Wanaharakati na Viongozi wa mashirika yasiyo kuwa  ya Kiserikali wameombwa kuunganisha nguvu zao na kuendelea kuyatetea kwa uhakika makundi yanayohitaji huduma yao.


Wito huo umetokewa na afisa Habari wa Mtandao wa Kutetea haki za Bianadamu Tanzania (Tanzania Human Rights Defenders Coalition-THRDs Coalition) Bw. Elias Mhegera wakati akiongea na waandishi wa habari na viongozi wa mashirika yasiyo kuwa ya Kiserikali Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma.



Mhegera ambaye amefuatana na Mratibu Taifa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (Tanzania Human Rights Defenders Coalition-THRDs Coalition)  katika ziara ya utafiti wa kuangalia vikwazo na changamoto ambazo zimekuwa zikiwakwaza watetezi wa haki za Binadamu  nakuona njisi gani watawasaidia na kufanya shughuli zao zinakwenda vizuri.



Alisema lengo la ziara yetu katika Mikoa ya Tanzania Bara na Visiwani zikiwa ni juhudi za Mtandao huo kufanya utafiti na kuyatambua matatizo, vikwazo na changamoto mbali mbali za ukandamizaji wanavyofanyiwa watetezi hao wa haki za binadamu ambavyo makundi hayo yamekuwa kifanyiwa huku vyombo vilivyo pewa mamlaka na serikali kuwalinda vikiwa havitoi majibu wala kutafuta mwarubaini wa kuvikomesha.



Bw.Mhegera ambaye katika maelezo yake alitolea mfano wamatukio ya kinyama waliyofanyiwa Mwenyekiti wa jukwa la wahariri Tanzania Absalom Kibanda na Dkt. Steven Ulimboka aliendelea kufafanua kuwa hivi sasa Mtandao huo umejipanga kuanza kutoa mafunzo na mbinu za kujikinga kwa wahanga wa vitendo hivyo pamoja na kuandaa mikakati mbalimbali ya kuwatete kwa kuwawekea wanasheri na kuhakikisha kuwa mkono wa Sheria unawanasa maharamia hao.



Akichangia kwa nyakati tofauti Mwenyekiti wa Mtandao wa Asasi za Kiraia Wilayani Tunduru (MATU) ambaye pia  Focal Person wa Mtandao wa watetezi wa Haki za Binadamu Kanda ya Kusini Pwani Bw. John Nginga alisema kwamba changamoto zinazo wakabili kama watetezi wa haki za binadamu ni pamoja na vitisho kutoka kwa viongozi wa serikali,kutopata ushirikiano katika kutekeleza majukumu na kupata taarifa sahihi kama
upatikanaji wa takwimu ikiwemo masuala ya sharia mbali mbali za nchi hususan zinazolengwa haki za binadamu.



Aliendelea kueleza kwamba pamoja na changamoto zinazowakabili kama Mtandao bado hawajakata taa katika kupigania haki za Binadamu hasa katika masuala ya utetezi kwani wananchi waliowengi hususan waishio vijijini wamekuwa wakikwama sana katika upataji wa huduma na haki za msingi za kihuduma kama Wanawake, Wajane, Watoto,Walemavu na WAVIU



Kwa mujibu wa Bw. Mhegera ziara yao ilianzia Unguja, Pemba Tanzania Visiwani na baadae katika Mikoa ya Arusha, Ngorongoro, Serengeti, Musoma,  Bunda, Mwanza, Tabora, Kigoma na Katavi,Rukwa,Mbeya,Iringa na sasa Ruvuma ambako alisema katika msafara huo wamebaini kuwepo kwa Vikwazo na changamoto mbali mbali zinazo hitaji kutolewa kwa elimu ya uhakikwa kwa jamii hapa nchini.



Akitoa neon la shukrani baada ya kufungwa kwa kikao hicho mwakirihi wa asasi ya Kiraia yakitengo cha Kiislam kinacho shughuliki amasuala ya Ukimwi Wilayani Tunduru (BAPRO) Issa Mdaraka alisema kuwa endapo jamii na viongozi wa Mashirika ya kijamii yatapatiwa elimu hiyo upo uwezekano mkubwa wa kupatikana kwa mabadiliko ya kuachana na mila na destuli za aina hiyo.



No comments:

Post a Comment