masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Thursday, July 4, 2013

ASKOFU AWATAKA WANAOTUMIA JINA LA HAYATI MWALIMU NYERERE KULIENZI HUKU WAKIFANYA MAMBO MACHAFU WABADILIKE

Mhashamu Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa akihubiri wakati wa maadhimisho ya Misa ya Upadrisho na Yubilei ya miaka 75 ya Parokia ya Kaning'ombe.


Padre Victorino Kalinga akiwa amelala kifudifudi akiombewa Roho Mtakatifu kabla ya kuwa Padre.

Mhashamu Baba Askofu akimuweka wakfu Padre Victorino Kalinga

RAIS wa Baraza la Maaskofu Tanzani Mhashamu Tarcisius Ngalalekumtwa amewataka watu wasiwe wasanii kwa kutumia jina la Mwalimu Nyerere kuwa wanamuenzi huku wakifanya mambo ya ajabu ya unyanyasaji na ukandamizaji wa haki za watu.

Aliyasema hayo jana katika maadhimisho ya Misa utoaji wa daraja la Upadre kwa Shemasi Victorino Kalinga iliyokwenda sambamba na maadhimisho ya Yubilei ya Miaka 75 ya Parokia ya Kaning’ombe jimbo Katoliki la Iringa.

Askofu Ngalalekumtwa ambaye pia ni askofu wa Jimbo la Iringa alisema, kutokana na usanii wa watu wanaojifanya wanamuenzi hayati Baba wa Taifa Julius Nyerere huku wakifanya mambo ya kihuni ipo siku uongo wao utawatokea puani.

“Ipo siku mtasema mnamuenzi halafu mmkute ameketi juu ya kaburi sijui mtasema nini? Nyio watu wadanganyifu mnaotumia jina la Mwalimu Nyerere, acheni usanii, uhuni na uongo kuwadanganya watu wenye akili” alisema.

Alisema kuwa si kila mtu amefirisika kifikra na kwamba watu wanajua kila kitu kinachoendele kuwa ni uongo au ukweli.

Alisema binadamu wa leo ametoka nje ya matakwa ya Mungu na kufanya mambo yasiyo stahili kwa kutenda dhambi kwa kujifanya wema huku wakiwaumiza wenzao.

Aliwaasa Wakristo kuwa wajumbe wa habari njema kwa ajili ya kulinda amani ambapo wanatakiwa kumtafuta Mungu kwa ajili ya wokovu.

“Maaskofu na Mapadre wameteuliwa na Mungu kwa ajili ya kufungua mioyo ya watu ili waweze kumtafuta Mungu na kuufifikia wokovu wa wa milele.

“Mungu mwenye upendo, huruma na msamaha ni Yule tunayehitaji kuajikabidhi maisha yetu kwa ajili ya furaha ya milele” alisema askofu Ngalalekumtwa.

Hata hivyo alisema Padre anapasika kuwa na msimamo usio na lawama ili asije akachakachua maagizo ya Mungu na kujitunza nafsi yake kwa ajili ya kuwa muangalizi mwema wa kondoo alioachiwa na Mungu.

“Padre awe na msimamo safi na awe na akili kichwani ili apate kubaini kufichua na kukemea yale ambayo hayastahili yanyowafanya wana wa Mungu kuishi kwa hofu. Padre ni mjumbe wa amani ambaye anatakiwa kuwa mstari wa mbele kwa ajili ya kuishi kwa upendo, mshikamano na kuwahurumia wengine” alisema.

Alisema kuwa pamoja na purukushani zote zilizopo, bianadamu ana kiu ya Mungu ambayo padre anatakiwa kuizima kiu hiyo.

Alisema kuwa wakristo wanatakiwa kukusanyika pamoja na kutoa dua kwa Mungu ili kuliombea Taifa linaloingiliwa na watu wasio na mapenzi mema wanaopenda kuwasambaratisha watu wasio kuwa na hatia.

Miaka 75 ni heshima tuliyopewa na Mungu kwa ajili ya kutangaza uweza wake kwa mataifa ambayo bado hayajamfahamu.

“Miaka 75 iwe ishara ya kuendeleza na utamaduni wetu wa upendo aliotuachia Kristo Mwokozi kwa ajili ya maisha yetu. Lindeni hayo ili Mungu Mwenyezi azidi kutulinda katika ukamilifu wa upendo, mshikamano, huruma, hekima, busara na amani” alisema.

Kanisa lazima litoe lishe kwa watu wake ili miili yao isishambuliwe na magonjwa ya dhambi. Kwa njia ya padre, binadamu watapata faraja ya Mungu kwetu tunaoishi katika bonde la machozi.

Maadhimisho ya upadre yalikwenda sambamba na maadhimisho ya Yubilei ya miaka 75 ya Parokia ya Kaning’ombe ambapo yalihudhuriwa na askofu mstaafu wa jimbo Evrea Italia Mons. Luigi Bettazi pamoja na viongozi mbalimbali wa kiroho na serikali kutoka ndani na nje ya nchi.

No comments:

Post a Comment