masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Saturday, July 13, 2013

VIVUTIO VYA UTALII 67 VYATAMBULIWA MKOA WA IRINGA

Dkt. Christine Ishengoma

VIVUTIO vya 67 vya utalii vimetambuliwa katika Mkoa wa Iringa ambavyo vimeanza kutangazwa kupitia vipeperushi na wasifu (profile) wa utalii.

Pamoja na vivutio hivyo kuanza kutangazwa, uhamasishaji unaendelea kufanyika katika sehemu mbalimbali zikiwemo shule na taasisi mbalimbali ambapo jumla ya shule 12 na Taasisi 4 zimeshakwisha pata uhamasishaji wa utalii katika Mkoa huo.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo Mkuu wa Mkoa wa Iringa Christine Ishengoma alisema kamati ya utalii Mkoa kwa kushirikiana na TANAPA, Taasisi za Elimu ya Juu, Wizara ya Maliasili na Utalii pamoja na wadau mbalimbali wanaendelea kutoa elimu juu ya utalii.

Amesema utangazaji wa vivutio hivyo unakwenda sambamba na utangazaji wa wasifu wa uwekezaji kupitia vikao mbalimbali ambapo vikao vitano vimekwisha kufanyika katika Halmashauri ya Kilolo na Manispaa ya Iringa.

Ishengoma amesema umefanyika uhamasishaji wa usindikaji wa mazao kwa vikundi vitatu kwa msaada wa Shirika la MUVI juu ya umuhimu wa kusindika mazao kabla ya kuyauza kwa kufuata viwango vinavyokubalika na shirika la viwango Tanzania (TBS) ili kuongeza thamani ya zao.

Hata hivyo amesema jumla ya maeneo 159 yametengwa na kuendelezwa katika halmashauri kwa ajili ya kuendeleza viwanda vidogo vidogo.

Kwa upande wa biashara Ishengoma amesema jumla ya vikundi 8 vya wajasiriamali vimepatiwa mafunzo kuhusu mbinu za kuyafikia masoko ya nje katika halmashauri ya Iringa vijijini na Manispaa.

“Uhamasishaji katika Halmashauri zote umefanyika kupitia Idara za kililo, mifugo na biashara kwa kuwaelimisha wananchi kutumia bidhaa za ndani ambapo vijiji 100 vimefikiwa. Halmashauri zimeendelea kuboresha mazingira ya kufanya biashara kwa kutekeleza sheria za usajili wa shughuli za biashara (BRELA) kwa kuhakikisha biashara mbalimbali zinasajiliwa katika vijiji” amesema.

Katika ujenzi wa miundombinu amesema jumla ya Km 720.04 za barabara zimefanyiwa matengenezo ya aina mbalimbali ikiwa Km 236.0 zimefanyiwa matengenezo ya kawaida, Km 299.1 za maeneo korofi na km 184.14 zimefanyiwa matengenezo maalum.


Hata hivyo ujenzi wa barabara ya Iringa – Mafinga umekamilika kwa asilimia 95 wakati barabara ya Iringa – Dodoma ujenzi wake umefikia asilimia 65.

No comments:

Post a Comment