![]() |
| Rais Jakaya Kikwete |
WATU watatu ambao ni wanachama wa
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wamepigwa na kujeruhiwa na watu wanaoaminika kuwa
ni wafuasi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) katika kijiji cha Mdeke Kata ta Ng’ang’ange
jimbo la Kilolo.
Kipigo hicho kimetokea leo mita 50
kutoka ofisi ya Chadema ambapo wanchma wa Chadema walikuwa wamekaa kufanya
maongezi yao nyuma ya ofisi.
Wakati vurugu hizo zikianza mwanachama mmoja wa Chadema alikuwa akipita barabarani jirani na uwanja walipokuwa
wakifanyia mkutano CCM ambao hutumiwa na Chadema kufanyia mkutano.
Wakati mwanachama huyo akipita
alijikuta akivamiwa na kundi la vijana wa CCM na kuanza kukimbia kuelekea
ofisini kwao ambako wenzake walikuwa wakifanya maongezi hali iliyosababisha wengine kupigwa bila
kutegemea.
Wakati tukio hilo likitukia
viongozi wa CCM walitumia mgambo kwenda kuwadhibiti wanachama wa Chadema kwa hofu
kuwa wangerudisha mashambulizi jambo ambalo mgambo walijikuta wakiwa na hofu
kuwakamata bila sababu na kulazimika kupiga simu kituo cha Polisi Kilolo kwenda
kutoa msaada.
Watu waliopigwa ni Fahamu Mgata
ambaye alikutwa na dhahama hiyo wakati akijiandaa kutoka na pikipiki ya
matangazo kwenda kutangaza mkutano wa Chadema huku ambapo aliyekuwa akipita
jirani na mkutano huo kwenda kujumuika na wenzake katika maongezi ofisini na
kuanza kupata kichapo ni Tomasi Msuva.
Chagua Lwisa ni majeruhi wa tatu
ambaye pia alikuwa ameumizwa wakati akijaribu kumuokoa Msuva aliyekuwa
akiwakaribia huku akipokea kichapo.
Kada mmoja wa CCM aliyehojiwa na mtandao huu na kuomba jina lake lisiandikwe amesema kuwa mpango huo
umepangwa kwa kufanyika hivyo kila wakati kwa lengo la kuwakatisha tamaa
wananchi kukipigia kura Chadema.
“Kwanza naomba unilinde, mimi nipo
ndani ya CCM lakini kwa mipango ya kampeni inayopangwa sasa si mizuri kwa
sababu ni kutumia fujo. Watu wa leo hawahitaji siasa za fujo bali wanataka
siasa za hoja lakini tulipofikia ninalaani kabisa kitendo hiki.
“Mlengwa mkuu katika hili ni Baraka
Mfilinge na Tomasi Msuva wa Chadema kwa kuwa ndio wanaosadikiwa kuwa wanafanya
siasa za kuwabadilisha wananchi kuhamia Chadema. Kiukweli huu siyo uungwana.
Ifike mahali tukishindwa tukubali kuwa tumeshindwa kuliko kutumia mabavu”
kilisema chanzo chetu.
Hata hivyo mtandao huu ulifanikiwa
kuongea na baadhi ya maaskari wa Kilolo ambao majina yao tunayo (yanahifadhiwa)
wallisema walipigiwa simu kwa ajili ya kwenda kuwakamata wafuasi na wanachama
wa Chadema jambo ambalo walipofika wakaona ni la uonezi.
Hata hivyo chanzo hicho kimeeleza
kuwa hayo yanatokea baada ya kuona mbinu za kumrubuni mgombea wa Chadema
zinagonga mwamba baada ya kushtikiwa.
“Mtu mmoja mkubwa tu wa CCM
alitupigia simu kuwa tukifika kule tumkamate Baraka Mfilinge, Tomasi Msuva na
mwandishi wao lakini kiukweli baada ya kufika pale tuligundua kuwa CCM ndio
wachokozi.
“Uchokozi wa CCM unakuja pale
walipokwenda kufanyia mkutano nje ya ofisi ya Chadema lakini hata hivyo
wamefanya makosa kuwapiga wanachama wa Chadema kwa kuwa walikuwa katika maeneo
yao sahihi” kilisema chanzo chetu.
Chanzo hicho kilipoombwa kutaja
jina la mwandishi wa habari ambaye alitakiwa kukamatwa, kilisema “mwandishi wa
gazeti la Tanzan Daima" bila kutaja jina lake.
Vurugu hizo zinatokea siku chache
baada ya kuwa na taarifa kutoka ndani ya CCM kuwa kuna watu maalumu
kutoka ndani ya chama hicho wameandaliwa
kuhakikisha mgombea wa Chadema Nafred Lucas Chahe anarubuniwa kwa njia yoyote
na kwa gharama yoyote ili mradi tu asishiriki uchaguzi kwa kuwa ndiye anayependwa
na wananchi.
Hata hivyo mtandao huu umebaini
watu ambao wanafanya mipango ya kumrubuni mgombea huyo ambao namba za simu zao
zinahifadhiwa na majina yao.
Hata hivyo wananchi walioshuhudia tukio hilo wamelaani vikali
na kulazimika kuondoka katika viwanja hivyo huku wakisemezana kuwa CCM imekosa
mvuto.
“Kila wakati wanasema Chadema ndio wenye fujo kumbe tulikuwa
hatuelewi. Leo tumejionea kwa macho yetu CCM wakianza kumpiga mtu bila sababu.
Mbona watu wa Chadema tunao hapa kila siku hatuoni wakianza kumpiga mtu lakini
kwa macho yetu tumewaona CCM wakiwapiga. Kama hawakutaka apite hapa barabarani
walitaka akapite wapi? Kumbe tumegungua njama zao” zilisikika sauti za wananchi hao wakisemezana.

No comments:
Post a Comment