masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Wednesday, May 8, 2013

WAZIRI CHIKAWE AWADANGANYA WATANZANIA KUHUSU KUKAMILIKA KWA UPELELEZI WA KESI YA MTUHUMIWA WA MAUAJI YA MWANGOSI





Huyu ndie mtuhumiwa wa mauawaji ya Mwangosi (kulia)

WAZIRI wa sheria na katiba Mathias Chikawe awadanganya watanzania kuhusu upelelezi  wa kesi ya mtuhumiwa wa mauwaji ya aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo cha runinga cha Channel Ten Daud Mwangosi baada ya mtuhumiwa  huyo  kufikishwa leo  mahakamani na mahakama  hiyo kuelezwa  kuwa upelelezi bado kukamilika.
 
Waziri Chikawe alilidanganya  bunge hivi karibuni  wakati akijibu maswali ya wabunge kuhusu ucheleweshaji  wa usikilizaji  wa kesi hiyo ya mtuhumiwa huyo wa mauwaji ya Mwangosi , askari wa FFU mwenye namba G2573 Pasificus Cleophace Simoni ambapo waziri  alisema  kuwa upelelezi  wake umekamilika.
 
Katika hali  iliyowashtua wengi leo mahakamani hapo ni baada ya mtuhumiwa  huyo  kufikishwa kwa mara nyingine mahakamani hapo na wakili  upande wa jamhuri Adolph Maganda kuomba mahakama  hiyo  kutoa tarehe nyingine ya  kesi hiyo kutajwa  kutokana na upelelezi  wake kutokamilika.
 
Mtuhumiwa  huyo  alifikishwa mahakamani hapo ghafla  leo   baada ya kumbukumbu  za  awali kuonyesha  kuwa kesi hiyo ingetajwa May 9 ila jana alifikishwa  mbele hakimu mkazi, mwandamizi mfawidhi wa mahakama ya mkoa wa Iringa Juma Hasan  kiasi cha hakimu  huyo  kulazimika kumuuliza  mtuhumiwa huyo kama ni  yeye kweli ama la.

Baada ya  kesi  hiyo  namba 1/2012  ya mauwaji inayomkabili  askari  huyo  wa FFU  kutajwa  mbele ya mahakama  hiyo  kwa mtuhumiwa  kuitwa kizimbani hakimu  huyo alionyesha shaka  na kulazimika  kumhoji mtuhumiwa kwa mshangao kama ni kweli jina hilo ni lake na  yeye ndio mhusika ama vipi.
 
“Eti  ni  kweli  wewe  ndio mwenye jina  hili na mhusika na kesi hii iliyotajwa?" alihoji hakimu  huyo na mtuhumiwa   huyo  kuthibitisha  kwa  sauti kuwa ni kweli  mheshimiwa hakimu.

Hata  hivyo  wakili wa serikali Adolph Maganda aliiomba mahakama  hiyo  kutaja  tarehe nyingine ya kutajwa  tena  na kudai kuwa  upelelezi  wa kesi hiyo bado  kukamilika.

Kesi  hiyo  itatajwa  tena May  22 mwaka  huu  na mtuhumumiwa  amerudishwa mahabusu kutokana na kesi  hiyo  kukosa  dhamana kisheria.



No comments:

Post a Comment