| Brian Kikoti akiwahutubia wananchi wa Ng'ang'ange. |
| Mratibu wa Chadema nyanda za juu kusini Frank Mwaisumbe akiwahutubia wananchi wa Ng'ang'ange. |
| Baadhi ya wananchi wa Ng'ang'ange waliofika kwenye mkutano wakisikiliza wahutubiaji. |
| Mratibu wa Chadema kanda ya nyanda za juu kusini Frank Mwaisumbe akifungua ofisi ya Kata ya Ng'ang'ange. |
WAZEE wa kata ya Ng’ang’ange wamelaani vikali
mfumo wa uongozi walio nao na kuwaongoza wananchi kurudisha kadi za CHAMA cha
Mapinduzi (CCM) huku wakitoa shutuma nyingi kwa chama hicho.
Hayo yamefanyika juzi katika Kata hiyo wakati wa
kampeni za kumnadi mgombea wa udiwani kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema) ambapo zaidi ya watu 250 walirudisha kadi za CCM na kujiunga na
Chadema.
Wakiongozwa na mzee Lucian Mahenge mwenye umri wa
miaka 74 waka ti wa kurudisha kadi alisema hakuna sababu ya kuendelea
kuking’ang’ania chama kisicho na msaada na kwamba hakina jipya.
“Baada ya miaka 50 ndani ya CCM nimeona kuna
mateso na siyo uhuru tena tulioahidiwa. Uhuru alioutafuta Baba wa Taifa
umegeuka kuwa mateso kwetu sasa najiuliza imekuwa hivi kwa sababu Baba wa Taifa
hayupo tena duniani? Sasa nawaomba wazee wengu, wanaume na wanawake tuungane na
vijana wetu kuhakikisha mateso haya tunayakimbia ndani ya CCM” alisema Mahenge.
Alisema kumekuwa na ubaguzi uliopindukia katika
utoaji huduma hali inayosababisha watu kupata tabu na kutokujua hatima ya
maisha yao.
“Ndugu zangu, mimi mzee wenu ambaye tangu uhuru
nipo ndani ya CCM nawaambia ukweli kuwa CCM ya Baba wa Taifa siyo hii mnayoiona
leo. Huu ni mzoga. CCM ya wakati huo ilikuwa ni nzuri sana lakitu kwa sasa
nimefikiri sana nikaona chama kinachoweza kutusaidia ni hiki Chadema. Tuungane
kwa pamoja tuiage CCM iliyooza” alisema.
Naye mratibu wa Chadema kanda ya nyanda za juu
Kusini Frank Mwaisume akimnadi mgombea wa udiwani kupitia Chadema alisema miaka
50 imekwisha watu watanzania wakiwa na uchovu kupindukia ambao sasa hakuna
matumaini ya kupata ahueni kupitia serikali yao kwa kuwa nayo ina hali mbaya.
“Baba wa Taifa alilenga kulipeleka Taifa katika
maendeleo na kuyafikia maziwa na asali lakini watu waliopewa dhamana hiyo
wamekuwa hawana weledi ya kusimamia mlengo huo. Sasa ni wakati wa kufanya
maamuzi ya kuwakataa watu wasio na sifa” alisema Mwaisumbe.
Amewataka wananchi kutokufurahia kupewa shilingi
2,000/= kwa ajili ya kumchagua kiongozi kwa sababu pesa hizo zitageuka kuwa
maombolezo kwao.
“Tunamtaka diwani kwa ajili ya maendeleo haila
hatumchagui diwani kwa sababu ya fedha. Ukimchagua mtu kwa sababu ya fedha
unaangamiza familai yako. Usifurahi kwa kuwa unapewa shilingi 2,000/= ili
umchague mtu” alisema.
Alisema mzalendo wa nchi hufanya maamuzi bila
kushawishiwa kwa rushwa na kwamba mwananhi anayesaliti kata, husaliti kijiji, mtaa
au kitongoji hadi familia yake na hivyo kuwataka wananchi wasimsaliti mgombea
wa Chadema kwa ajili ya maendeleo kata hiyo.
Naye mgombea udiwani kwa tiketi ya Chadema Nafred
Lucas Chahe amewataka wananchi wa kata hiyo kumfanya kuwa daraja ili awatumikie
kwa dhati na mwisho maendeleo yaweze kupatikana.
“Tuna mambo mengi sana hapa kwetu hayajawah
kutatuliwa miaka 50 iliyopita hadi leo. Mnifanye kuwa msemaji wa mambo haya ili
yaweze kutatuliwa. Malengo yetu tunayopanga yatatimia tukishirikiana kwa pamoja
ila tu cha msingi kunipa kura yenu ili niweze kuwa msemaji ili tufanikishe
malengo yetu.
Mkutano huo ulikwenda sambamba na ufunguzi wa
ofisi ya Kata ambapo imejengwa kwa jitihada za mgombea udiwani huyo.
Uchaguzi mdogo katika kata hiyo unatarajiwa
kufanyika Juni 16 Mwaka huu.
No comments:
Post a Comment