masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Thursday, April 4, 2013

KUFELI KWA WANAFUNZI NI DALILI YA KUFELI KWA JAMII NZIMA



KUSHUKA kwa kiwango cha ufaulu wa wanafaunzi nchini kumeelezwa kwamba ni dalili ya jamii kushindwa kuwajibika katika elimu.

Haya yamezungumzwa na Mkurugenzi wa asasi isiyo ya kiserikali ya Tuwafikie Bovan Mwakyambiki katika mahojiano maalum na mtandao huu leo.

Mwakyambiki amesema ili mwanafunzi aweze kufanya vizuri ni lazima jamii inayomzunguka iwe inafanya vizuri pia ambapo jamii ya watanzania kwa asilimia kubwa ni jamii ambayo haijaipa sekta ya elimu umuhimu wa kutosha.

“Jamii ya watanznia ni jamii ya watu ambao wapo bize kiasi cha kusahau kufuatilia hata maendeleo ya watoto, ni jamii ya watu waliojengwa katika mfumo wa kujifunza wakiwa shule na baada ya kumaliza shule hawaoni umuhimu wowote wa kuendelea kujifunza na kujiendeleza” amesema Mwakyambiki.

Amesema kila jamii ya watanzania ni jamii ya watu wasiopenda kujisomea na kuboresha fikra zao na ni rahisi kumkuta mzazi ukipita zaidi ya mwaka mmoja bila kugusa kitabu chochote ambacho kinaweza kumuongezea ujuzi katika mambo mbalimbali

“kila mkoa niliopita, nje ya Dar es salaam ni vigumu sana kuyakuta maduka ya vitabu vya kijamii, na mikoa mingine hakuna kabisa maduka ya vitabu vya kijamii. Hii ni dalili kubwa sana kwamba jamii yetu sio ya wasomaji, ni jamii ambayo inaona suala la elimu ni anasa. Hakuna maendeleo yatakayoweza kupatikana kama jamii haitaweza kubadilika. Wanafunzi ni watoto wetu, ni matunda ya jamii yetu. Kama jamii ilivyobize kufanya mambo mengine na kuona hakuna mda wa kuendelea kujifunza, vivyo hivyo hata kwa wanafunzi ambao ni watoto wetu. Nao wanaona kuna mambo mengine ambayo wanapenda kuyafanya zaidi ya kusoma kwa sababu hata wazazi nao wanatabia hizo” amesema.

Amesema suala la kufeli kwa wanafunzi si la kuilaumu sekta moja bali ni jambo linalotokana na mmomonyoko wa maadili kwa jamii nzima kwani kila jamii ina wajibu wake.

“Watu wengi wameshangazwa sana na matokeo ya kidato cha nne kwa wanafunzi waliofanya mtihani wa taifa mwaka jana, jamii imekua ikilaumu sana serikari na wasimamizi wa masuala ya elimu nchini na kusahau kuwa jamii bora hujengwa na jamii husika” amesema.

Amesema kufeli kwa wanafunzi ni urithi kutoka kwa wazazi na jamii inayowazunguka na kwamba kila mti huzaa matunda ya aina yake, jamii ya watu wasiopenda elimu huendelea kuambukiza tabia hizo hata kwa vizazi.

“Kufeli kwa wanafunzi ni dalili ya kufeli kwa mzazi, kufeli kwa mwalimu, kufeli kwa viongozi wa ngazi zote, ni kufeli kwa wasimamizi wa masuala ya elimu nchini, kufeli kwa wanafunzi ni kufeli kwa jamii nzima. Kwa hali hii ninaamini kama tungeweza kutafuta kipimo cha kupima uelewa wa Watanzania kwa mambo mbali mbali pia ninaamini kiwango cha kufeli kingekuwa ni kikubwa kuliko hata hiki cha wanafunzi” amesema.

Ameitaka jamii kubadilika na kujua ya kwamba, hakuna maendeleo yoyote kama hakutakua na juhudi za msingi kuthamini na kuboresha utoaji na upokeaji wa elimu pamoja na kuona uzito uliopo katika elimu na kutambua kutambua kwamba ni kioo na picha yake halisi huonekana kwa uraisi kwa uzao wetu ambao ni wanafunzi.

“Ninapozungumzia jamii ninagusa kila mmoja kwa nafasi yake, hata rais wa nchi
hii yumo ndani ya jamii” amesema.

Ameongeza kuwa jamii itakapochukua hatua ya kubadilika na kuthamini elimu pindi itakapojitambua na kujua wajibu wake itawawawezesha vijana kuwatengeneza na kuwasimamia katika kuwaongoza na kuwaonesha njia ikiwa ni pamoja na kushirikiana na wadau wote wa masuala ya elimu

“Kama jamii itaweza kuwajibika na kujua kwamba ni wajibu wa kila mmoja wetu kuweza kusimamia maendeleo ya elimu nchini, tutaweza kuwa na elimu bora na hakika hatutaweza kuwapoteza wanafunzi kama ilivyo sasa. Wanafunzi wengi wanadharau elimu kwa kuwa hata wazazi au jamii wanaidharau pia. Mabadiliko ni lazima yaanze na wewe, mimi mabadiliko ni sisi” amesema.

Ufaulu wa wanafunzi wa kidato cha nne kwa mwaka 2012 umeshuka kwa 60% kulinganishwa na mwaka 2011 walifeli kwa 46.4%, mwaka 2010 walikuwa 49.6%, mwaka 2009 walikuwa 27.5%, mwaka 2008 ilikuwa 16.3% na mwaka 2007 ilikuwa 9.7%.

No comments:

Post a Comment