masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Saturday, March 2, 2013

Ulevi siyo ishu!

Mtu ambaye jina halikuweza kufahamika mapema amenaswa akiwa katika usingizi baada ya kile kilichoelezwa kuwa ni ulevi wa ulanzi.




Ulanzi ni aina ya ya pombe yenye kilevi ambao upo kwa mfumo wa maji na ina sukari yenye kumvuta mnywaji kuendelea kunywa.

Licha ya pombe hiyo kuwa n madhara, watumiaji wengi wanajisahau na kujikuta wakishindwa kutembea kutokana na kunywa kupita kiasi.

Pamoja na kuwa pombe hiyo huvutia wanywaji kwa kiwango kikubwa, wapo baadhi ya watu ambao wanajikuta wakiahirisha shughuli zao kwa sababu ya kunywa pombe.

Mtu mmoja ambaye jina lake halikuweza kufahamika kwa haraka amekutwa na mtandao huu leo “akiuchapa” usingizi kando ya barabara ya Dodoma Iringa katika kijiji cha Mgongo baada ya kunywa ulanzi kijijini hapo.

Kwa mujibu wa mashuhuda wamesema mtu huyo alifika kijijini hapo kwa lengo la kuhudhuria msibani lakini akakutana na ulanzi ambao alikunywa kwa fujo kisha kusahau alichofuata.

“Mtu huyo hatumfahamu, alikuja kwenye msiba lakini alipouona ulanzi akachanganyikiwa akaanza kuububuja. Lakini hata hivyo inaonekana alikuwa hajala na ulanzi hautakiwi unapokunywa uwe na njaa. Sasa angalia badala ya msiba amekuwa shida kwake tena” amesema shuhuda mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Kilwabulilo.

Hata hivyo ilikuwa ni vigumu kwa mtu huyo kufanya chochote kwa kuwa amekuwa akiyumba huko na huko na kushindwa kujificha katika kivuli jambo lililomsababisha kujianika kwenye jua.

Wataalamu mbalimbali wa vinywaji vyenye kilevi (alcohol) wanasema hudhuru sehemu mbalimbali katika mwili wa binadamu na kusababisha madhara makubwa na mabaya hasa utumiaji wa  pombe kali.

Wanasema sehemu kubwa zinazopata madhara zaidi katika utumiaji wa pombe ni Ini kuharibika vibaya na kuwa kama kitu kilichoungua kwa moto, Tumbo huweza kuchubuka hasa katika ngozi laini ya tumbo la chakula na kusababisha vidonda vya tumbo.

Sehemu zingine ni Ubongo kuharibika na kusababisha kupungua kwa kumbukumbu kumbukumbu, Mimba kuharibika na kusababisha kuzaliwa kwa mtoto asiyekuwa na akili timamu (mtindio wa ubongo) pamoja na kuleta madhara katika moyo na mapafu ya binadamu.

No comments:

Post a Comment