masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Sunday, March 31, 2013

UCHAGUZI WA WAJUMBE WA MABARAZA YA KATIBA MIZENGWE

UCHAGUZI wa wajumbe wa mabalaza ya Katiba katika Mtaa wa Ngome Kata ya Kihesa katika Manispaa ya Iringa umewashangaza wakazi wa mtaa huo baada ya ofisa Mtendaji kudaiwa kuwaingiza watu wake bila kufanyika uchaguzi.

Imeelezwa kuwa ofisa mtendaji huyo amekuwa na kawaida ya kufanya maamuzi yake bila kuwashirikisha wananchi licha ya kuwa wananchi ndiyo watendaji wa maendeleo.

Wananchi wa mtaa huo wameeleza kuwa katika taratibu za ufanyaji mikutano zimekuwa zikikiukwa mara kwa mara hata ofisa huyo kushirikiana na baadhi ya watu kumpiga vita mwenyekiti wa mtaa huo kutokana na kuwa mkweli na muwazi katika shughuli zake.

Hata hivyo wakazi wa mtaa huo wamesema hawakutangaziwa sehemu ambayo uchaguzi huo utafanyika sambamba na kutoyaona majina ya wagombea wa nafasi hizo ambayo kwa mujibu wa mwongozo wa uundwaji wa mabaraza ya Katiba yalikuwa yabandikwe ili wanamtaa husika waweze kuyaona na kudhiria.

Walisema kuwa zengwe hilo lilianza wakati wa kuwasilisha majina ya kugombea nafasi hizo kwa kile walichokuwa wakiambiwa kuwa anayeandika barua lazima awe anamiliki nyumba.

“Watu tumeandika barua za kugombea nafasi hizo lakini tulipowasilisha kwa mtendaji akasema kama hatumiliki nyumba haturuhusiwi. Ina maana hivyo Katiba ni ya watu wenye nyumba tu? Mtendaji alishindwa kutuambia ukweli kuwa ana watu wake anaowataka awaingize huko kama alivyozoea” alisema mkazi mmoja ambaye alikuwa na hasira.

Na kwamba “mwenyekiti wetu anapofanya vizuri wanampiga vita tena akishirikiana na watu wachache tu ambao anataka kufanya nao wizi. Na sababu ya kumpiga vita ni kwa sababu ni muwazi, hafichi kitu kama wanavyofanya wao”.

Ofisa mtendaji wa mtaa huo Eliques Ngakonda alipotafutwa ili kutoa ufafanuzi juu ya hilo alisema uchaguzi ulifanywa na watu 105 katika viwanja vya soko jipya linaloendelea kujengwa katika mtaa huo.

“Tumefanya uchaguzi katika viwanja vya soko ambapo kulikuwa na watu 105 walioshiriki katika uchguzi huo saa 5 asubuhi na majina yalibandikwa” alisema Ngakonda.

Alipotakiwa kutaja majina ya watu waliochaguliwa alisema majina hayakumbuki kwa kuwa hayupo ofisini.

Hata hivyo alipotakiwa kutoa ufafanuzi wa tuhuma anazotuhumiwa kutumia mabavu katika uongozi wake alishindwa kujieleza kwa kile alichosema hajui lolote.

No comments:

Post a Comment