masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Friday, March 29, 2013

MUNGAI AICHAMBUA TUME YA WAZIRI MKUU PINDA

Joseph Mungai akifafanua zaidi barua yake aliyoiandika kwa tume ya kuchunguza anguko la elimu kwa mwaka 2012 kwa waandishi wa habari.

Joseph Mungai akijibu swali aliloulizwa na Katibu wa chama cha waandishi wa habari Mkoa wa Iringa (IPC) Francis Godwin (kulia).

Joseph Mungai akiwashukuru waandishi wa habari mara baada ya kumaliza mazungumzo naye.

WAZIRI wa zamani wa elimu Joseph Mungai, ameipa somo Tume  ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda iliyoundwa kwa ajili ya kuchunguza matokeo mabaya kuliko yote ya mitihani ya kidato cha nne yaliyowahi  kutokea hapa nchini, akiitaka kuzitolea uvivu taasisi mbili za umma ambazo ni Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) na Taasisi ya Elimu nchini (TIE).

Mungai aliyeiongoza Wizara ya Elimu wakati wa serikali ya awamu ya tatu mwaka 2000-2005 sambamba na kuwa Mbunge wa Mufindi Kaskazini,amesema inafaa matokeo ya mitihani yawe yanatangazwa kwa uwazi hata kama ni mabaya tofauti na ilivyo sasa.

Katika barua yake ya wazi ya Machi 29 mwaka huu yenye kumbukumbu namba JJM/2013/ELIMU/19 iliyoandikwa kwenda kwa Mwenyekiti wa Tume ya Elimu iliyoundwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuchunguza kufeli kwa wanafunzi wa kidato cha nne mwaka 2012,

Mungai ameitaka tume hiyo irejee utafiti uliofanywa na Wizara ya Elimu na Ofisi ya Waziri Mkuu,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) mwaka 2010 ambayo ilifanya utafiti kudadidi sababu za ufaulu mbaya ambayo pia serikali ilishindwa kuusoma bungeni.

Katika barua yake kwa tume hiyo, Mungai anahoji kwa nini ukweli ulifichwa licha ya taarifa hiyo ya utafiti  kuwapo kwenye maktaba za Wizara na kwamba anayoyasema hivi sasa ameyapata kutoka taarifa moja isiyo ya siri ndani ya Wizara ya Elimu.

Hata hivyo, Mungai ameitaka tume hiyo ieleze wazi wazi kwamba Taasisi ya Elimu (TIE) iagizwe na iachiwe kutekeleza wajibu wake wa kisheria chini ya sheria ya elimu ya mwaka 1995 ya kuandaa na kuboresha mitaala.

“Tume ya Waziri Mkuu (Pinda) ifanye kwanza rejea ya maandiko ya Wizara ya Elimu ambayo ni Nyaraka za Elimu za mwaka 1999 hadi 2005 na Sheria ndogo za Elimu au kanuni za elimu zilizotungwa kuyapa maboresho hayo uzito wa kisheria yamepelekwa nyaraka za kale kabla ya wakati wake…Hii itasaidia badala ya kutumia muda mwingi na fedha nyingi kugundua upya gurudumu,” inasema sehemu ya barua hiyo ya wazi kwenda kwa Tume ya Waziri Mkuu.

MITAALA YA ELIMU IPO
Waziri huyo wa zamani wa Elimu  amemkejeli pia Mbunge wa kuteuliwa na Rais, James Mbatia kuhusu kauli yake aliyoitoa Bungeni miezi michache iliyopita kwamba nchi inaongozwa bila mitaala ya elimu kwamba haina ukweli kwa kuwa mitaala hiyo ipo isipokuwa kuna ‘madudu’ katika taasisi za umma zinazohusina na elimu.

Alisema Mbatia aliitoa kauli yake bungeni pasipo kufanya utafiti wa kina na kwamba hata wapinzani wa serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM) wanajua kwamba wanasiasa huamua bila kuzingatia ipasavyo utafiti na ushauri wa kitaaluma kuhusu elimu ya taifa letu.

“Kwa hiyo mimi ninaimbia tume ya Waziri Mkuu kwamba utaratibu sahihi wa kupanda madarasa kwa kufaulu uliowekwa na Waraka wa Elimu namba moja na namba mbili wa mwaka 2002 urejeshwe na uimarishwebila kuchelewa ambayo mwalimu mkuu siku zote anayo madaraka ya kukaririsha kama mwanafunzi hajazijua zile ‘K’ 3 yaani kusoma,kuandika na kuhesabu,”Alisema Mungai.

 =========================================
Joseph J.Mungai MB (mstf0
P.O.BOX 34 Mafinga
S: 0753 192999 BP: jjmungai@tatepa.com



BARUA YA WAZI KWA TUME YA ELIMU
YA KUFELI 60% MTIHANI WA KVI 12012
ILIYOTEULIWA NA MHE WAZIRI MKUU


                                                          29/03/2013


Kumb Na. JJM/2013/ELIMU/19



Kwa Mwenyekiti

Tume ya Elimu  ya Kufeli KIV

Ofisi ya Waziri Mkuu

DAR ES SALAAM



Ndugu Mwenyekiti

KUONGEZEKA WANAOFELI KIV KUTOKA 9.7% MWKA 2007 HADI 60% 2012

1.1   Nnawapongeza kwa kuteuliwa na ahsante kutupa fursa wadau fwa elimu kuwaletea maoni na  au/ushauri.

2.0  Mimi ni mdau wa elimu, niliyewahi kuwa Mwenyekiti mwanzilishi wa Mufindi Education Trust (MET) iliyoanzisha katika wilaya ya Mufindi        na kuziendesha  kwa mika      zaidi    ya 10 Sekondari  9 za: (1) JJ Mungai (2) Sadani ( 3) Itengule  ( 4) Igowole ( 5) Itandula ( 6) Mgololo ( 7 ) Kibengu ( 8) Mdabulo na ( 9) Nyololo; ambazo sasa ni za serikali. Aidha nimewahi kuwa waziri wa Elimu na Utamaduni  mwaka 2000 hadi 2005.

3.0 Kabla ya kutoa ushauri naoba kuipa Tume yako ufahamu  wa ukweli ufuatao:

3.1 Kufeli mwaka 2012 kidato cha Nne (KIV) kwa asilimia 60 halikuwa tukio lililoibuka ghafla bali waliofeli ( Division 0) mtihani huo waliongezeka kutoka mwaka 2007:9.7% ; 2008:16.3%; 2009:27.5%; 2010:49.6%; 2011:46.4% na sasa 2012:60%!!!!!

3.2 Kabla ya hapo waliofeli kidato cha Nne (KIV) WALIPUNGUA kutoak mawka 1998:24:3%:; 1999:20.0% 2000:21.6% 2001:22.6%, 2002:12.7%; 2003:12.2%, 2004:8.7%, 2005:10.7%, 2006:10.9%, na 2007:9.7% wastani wa kufeli 2004 hadi 2007 ni 10%. Tazama hotuba ya bajeti ya Waziri wa Elimu na Utamaduni ya mwaka 2005/2006 kielelezo Na. 75.4 ukurasa wa 100; na BEST ( Basic Statics in Education, National Data) ya miaka  husika.

3.3 Kati ya 2004 na 2007 waliofeli kidato cha Nne  walikuwa wastani wa 10% ambayo   inavumilika. Kwa nini kati ya 2007 na 2008 kulikuwa na mruko kutoka 9.7% hadi 16.3%? Huo ukawa ndio mwanzo wa kuonge zeka  kila    mwaka    hadi kufikia 60%       ya mwaka huu!!!!! Wizara ya Elimu na OWM-TAMISEMI baada   ya  matokeo mabaya ya mwaka 2010 walifanya  “utafiti kudadisi sababu   za ufaulu huo mbaya” na taarifa yake ipo kwenye maktaba a Wizara” na iliandaliwa kauli ya waziri isomwe Bungeni”, lakini  hadi leo haikusomwa.   Ukweli ulifichwa; na mficha ugonjwa kifo kitamuumbua. Nukuu zangu kutoka Taarifa moja     isiyo   ya siri ya ndani    ya wizara ya Elimu.

4.0 Kwa maoni yangu maboresho ya Elimu ya Serikali ya Awamu ya Tatu ambayo  yanaweza kusomwa katika maandiko   mawili    ya Wizara   ya Elimu     yaitwayo: (a) Nyaraka za Elimu 1999 hadi 2005, na ( b) Sheria ndogo za Elimu au kanuni za Elimu zilizotungwa kuyapa maboresho   hayo uzito w akisheria yamepelekwa NYARAKA ZA KALE (ACHIVES) kabla  ya wakati wake. Maboresho yamewekwa kando moja     baada ya jingine  au  hayakusimamiwa ipasavyo na Elimu yetu imerudi  ilivyokuwa kabla  ya mwaka 2000.

USHAURI:

5.0 Kwa kuwa Elimu ni nyenzo muhimu   sana kuliko zote katika kuboresha nguvu kazi ya Taifa na kucho cchea  maendeleo  ya nchi nimeamua kutonyamaza na kuwa muwazi kabisa, ingawaje mimi ni mwanasiasa  niliyestaafu. Kwa hiyo NASHAURI mambo yafuatayo:

5.1 Utaratibu  sahihi wa kupanda madarasa kwa ufaulu ( achievement based progression)  uliowekwa na waraka wa Elimu Na. 1& 2 wa 2002 urejeshwe na uimarishwe   bila  kuchelewa kuasnzia Darasa la kwanza,  la pili na la Tatu ambayo      Mwalimu Mkuu siku zote anayo madaraka    ya kukalilisha, kama mwanafunzi   hajazijua “K” 3: kusoma, kuandika na kuhesabu.

5.2 Tume ya Mhe. Waziri Mkuu ifanye kwanza REJEA ya maandiko ya Wizara ya Elimu  niliyoyataja akatika 4(a) na (b) hapo  juu yaliyomo maboresho ya         elimu ya 2002-2005 yaliyofanikisha kufaulu vizuri  katika   Elimu ya Msingi na Sekondari miaka       ya 2004-2007; badala ya kutumia muda mwingi na fedha n=yingi kugundua upya gurudumu.

5.3 Taasisi  ya Elimu   Tanzania ( Tanzania  Institute of   Education –TIE) iagizwe na iachiwe  kutekeleza wajibu  wake wa kisheria chini ya Sheria ya Elimu ya 1995 wa kuandaa na kuboresha mitala.

5.4 Wanasiasa tuache kuamua bila  kuzingatia ipasavyo utafiti na ushauri w kitaaluma kuhusu Elimu ya Taifa letu.



Kutokana  na uamuzi mbaya na kuchelewa kuchukua  hatua ya marekebisho kila inapobidi; Elimu yetu imerudi ilikokuwa  kabla ya mwaka 2000. Rika zima la kielimu limepotea!!!sasa tunavuna kilichopandwa vibaya. Kwa hiyo TUJISAHIHISHE kwa kuacha kuingilia na kuamua bila kuzingatia  utafiti na ushauri fwa kitaaluma ili tusije kuumbuliwa tena na matokeo mabaya kama    hayo ya kidato cha Nne   ya mwaka 2012. Aidha inafaa matokeo ya mitihani    yawe yanatangazwa kwa uwazi hata kama ni mabaya kwa sababu, narudia “ anayeficha maradhi       kifo kitamuumbua”



Wasalamu



Joseph J Mungai MB mstf

MDAU WA ELIMU
 


No comments:

Post a Comment