masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Saturday, March 23, 2013

MAGARI YA SERIKALI YADAIWA KUWA NI CHANZO CHA AJALI

Baraka Frank mwenyekiti wa waendesha bodaboda Mafinga akihojiwa na mtandao huu

Sehemu ya maegesho ya bodaboda Mafinga mbele ya stendi ya mabasi



MAGARI ya serikali yamedaiwa kuwa ni chanzo cha ajali barabarani kwa kukiuka sheria na taratibu za matumizi ya barabara.

Haya yamesemwa mwenyekiti wa waendesha pikipiki (bodaboda) Mafinga Baraka Frank katika mahojiano maalumu na mtandao huu yaliyofanyika katika maegesho ya pikipiki zao maeneo ya stendi.

Frank amesema madereva wa magari hayo wamekuwa wavunjaji makusudi wa sheria za barabarani kutokana na mwendo wao kuwa mkali na kutozingatia alama zilizopo pamoja na kutumia vibaya barabara wakidhani ni wao tu ndio wenye barabara.

“Ajali nyingi zinazotokea zinasababishwa na madereva wa magari ya serikali. Wanatembea hovyo kwenye barabara pamoja na kuwa na mwendo mkali kiasi cha kutowajali waendao kwa miguu, waendesha baiskeli pamoja na sisi waendesha pikipiki” amesema.

Amesema kila inapotokea ajali ikihusisha pikipiki, shutuma nyingi wamekuwa wakibebeshwa waendesha pikipiki kwa kuwa ndio wenye chombo kidogo.

Hata hivyo amesema hata wenye magari makubwa wamekuwa hawawathamini wenye vyombo vidogo kwa kuwa hata ingetokea wanagongana wao hawawezi kupata tatizo jambo ambalo kwa upande mwingine limekuwa ni la unyanyasaji.

“Tunawaomba viongozi wa serikali kila wakati wajaribu kukaa na madereva wao na kuwaelekeza matumizi ya barabara na hata wenye magari makubwa wapewe semina mara kwa mara ili watumie barabara vizuri kwa usalama” amesema.

Hata hivyo amelishauri jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani kutoa semina za mara kwa mara kwa madereva wa magari ya serikali na maroli ili waweze kuzingatia matumizi ya barabara wawapo barabarani.

No comments:

Post a Comment