masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Tuesday, February 19, 2013

Nguvu ya umma yamnusuru ofisa kilimo

Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Evarista Kalalu


MKAKATI uliopangwa na ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mufindi wa kumng’oa ofisa kilimo wa Kata ya Itandula wilani humo katika Mkoa wa Iringa ilishindikana baada ya mbinu walizozitumia kuonekana ni za kupangwa.

Katika mkutano uliofanyika katani hapo juzi ulilenga kuchafua na kung’oa ofisa kilimo Ngwalanje Emanuel kwa tuhuma za kujihusisha na siasa kama mwanachama wa chama cha demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Katika Mkutano huo Mkuu wa Wilaya hiyo Evarista Kalalu aliongozana na Ofisa utumishi wa Wilaya Denis Mselema, Afisa Tarafa aliyetambulishwa kwa jina moja la Shirima, Diwani wa Kata ya Itandula Simon Mangula na ofisa Mtendaji wa Kata Francis Ngano.

Kama ilivyoelezwa awali katibu mstaafu wa chama cha Mapinduzi (CCM) Askari Chanda alimtaka ofisa utumishi atolee maelezo juu ya mtumishi wa umma kushiriki siasa jambo ambalo ofisa utumishi huyo alionekana kutoa majibu ya kujichanganya pale aliposema kuwa hairuhusiwi kabisa huku akijua kuwa Mkuu wa Wilaya ni mwanasiasa pia.

Hata hivyo mabalozi wa CCM alionekana kila wakati kutafuta njia za kumtia hatiani ofisa kilimo hali iliojionesha wazi wakizidiwa hoja na wananchi waliokuwepo katika mkutano huo waliokuwa wakipinga vikali kuwa ni mbinu za kutengenezwa.

Mabalozi walionekana kumvaa ofisa kilimo kila wakati ili kumtafutia makosa ni Enabu Nziku, Dickson Kaguo na Brighton Mdendemi.

Kalalu alijiridhisha na majibu yaliyojibiwa na ofisa huyo ambayo yalionesha kuwa tuhuma alizopewa ofisa huyo ni za uongo.

Mabalozi hao walishindwa namna ya kumtia hatianai kwa uongo jambo lililosababisha kuumbuka mbele za mamia ya watu walijitokeza kupinga hoja zao za uongo ndipo ikamlazimu Mkuu wa wilaya kutumia weledi wa kiuongozi baada ya kujiridhisha kuwa uongo umetumika kumtuhumu ofisa huyo.

Katika hali ya kushangaza, mabalozi hao walisikitishwa na kitendo cha Mkuu wa Wilaya kutokutoa tamko la kumfukuza ofisa huyo kazi na badala yake kuwataka viongozi wa umma kutumikia jamii zao bila ubaguzi na kwa kujituma.

Mara baada ya mkutano huo kufungwa chanzo cha habari kilichoomba jina lake kutokuandikwa gazetini kilisema chanzo cha mgogoro huo ni Chadema kuingia kwa akasi katika Kata hiyo jambo linalowapa homa viongozi wa CCM kuanzia mabalozi katika chaguzi za serikali za mitaa zinazokuja mbele yao.

“Unajua chanzo kikubwa cha mgogoro huu ni kuingia kwa Chadema katika Kata hii kwa sababu viongozi wengi wa CCM hadi sasa wana homa kupoteza viti vyao kuanzia katika chaguzi za serikali za mitaa zitakazofanyika mwakani. Sisi hatuna tatizo na ofisa kilimo wetu kwa kuwa ni mtu anayefanya kazi kwa upendo na kwa bidii bila kumbagua mtu yeyote, siyo mtu wa rushwa wala mtu wa kuganganya. Yeye ni mkweli na ni mtu wa ushauri na majadiliano” kilisema chanzo hicho.

Chanzo hicho kilisema tuhuma alizobebeshwa ofisa huyo zilipagwa siku moja kabla ya mkutano uliofanyika na baadhi ya viongozi wa chama cha Mapinduzi na kujipanga namna ya kuwasilisha uongo huo mbele ya Mkuu wa Wilaya.

“Kabla ya kikao walichokaa siku moja kabla ya Mkutano mimi nikiwa miongoni kusikiliza kinachopagwa juu ya ofisa wetu, viongozi hao waliandika barua kwa Mkuu wa Wilaya juu ya tuhuma hizo. Ili kuonesha nguvu ya tuhuma zao ndipo walipokaa na kujipanga namna ya kutetea hoja zao lakini kama ulivyojionea mwenyewe wameshindwa. Kitu cha uongo daima hakina nguvu” kilisema chanzo hicho.

Chanzo hicho kilionesha ushahidi wa sauti zilizo naswa katika kikao hicho kilichodaiwa kililenga kupanga mbinu ya kumchafua na kumtia hatiani ofisa kilimo ili ang’olewe katika nafasi yake.

Hata hivyo imeelezwa kuwa mbinu hiyo itaendelea kufanyika maeneo mengine ikiwamo ya kuwabambika kesi wanachama na wafuasi wa Chadema ili kudhoofisha kasi ya upinzani vijijini.

Wakati mkutano huo ukifungwa Mkuu wa Wilaya aliwataka wananchi kuwaheshimu wataalamu wao ili kuweza kupata ujuzi na utaalam katika utendaji wa shughuli zao na kuachana na mizengwe isiyokuwa na tija katika maendeleo.

No comments:

Post a Comment