WAKULIMA
wametakiwa
kufuata ushauri wa wataalam wanaojitolea kutoa mafunzo kwa wakulima mbalimbali
ili kukiwezesha kilimo kuwa bara na chenye manufaa kwa kwa taifa.
Ushauri huo ulitolewa hivi
karibuni na Waziri wa fedha na uchumi William Mgimwa alipotembelea ofisi za
wataalam kupitia mradi wa Muunganisho Ujasiriamali Vijijini (MUVI)
mkoani Iringa kuzungumza na watekelezaji wa mradi huo pamoja na wakulima
wa mazao ya nyanya na alizeti.
Mgimwa alisema nchi nyingi zilizowekeza katika mafunzo na wakaazi wake wayakazingatia ndizo
zilizofanikiwa zaidi duniani.
“Nchi nyingi zilizowekeza katika mafunzo ndizo
zilizofanikiwa zaidi Duniani,ukienda China waliwekeza zaidi katika
mafunzo na wamepiga hatua kiuchumi, zingatieni haya mafunzo mnayopatiwa na
wataalam kutoka mradi wa MUVI” alisema Mgimwa.
Wakulima waliwaasa kufanya kwa
vitendo yale yote wanayofundishwa na wataalam ili waweze kufanikiwa katika kile wanachozalisha.
Ikumbukwe kuwa katika
utekelezaji wa kilimo kama ilivyo katika kaulimbiu ya “kilimo kwanza” serikali
ndiyo yenye jukumu la kusimamia kwa vitendo lakini wanapojitokeza wadau
mbalimbali kusimamia huongeza ufanisi kama
ilivyo kwa utekelezaji wa mradi wa MUVI.
Serikali inapaswa kutambua
mchango wa mashirika yasiyo ya kiserikali hasa yale yanayofanya kazi ambazo
serikali ilipaswa kuwajibika moja kwa moja kwani ushirikiano huo unaonesha
kuleta babadiliko ya kimaendeleo.
Mradi wa MUVI umefanikiwa
kuwaunganisha wakulima katika vikundi mbalimbali katika Mikoa ya Iringa na
Njombe ili kuwawezesha kuboresha kilimo chao kwa ajili ya kuongeza pato lao na
la taif kwa ujumla.
Licha ya juhudi za mradi huo
kushika kasi, serikali ambayo ndiyo yenye jukumu la utekelezaji wa kauli mbiu
ya kilimo kwanza imelalamikiwa kutotekeleza kwa vitendo jambo ambalo bado
linaonesha utekelezaji wa maneo bila vitendo.
Hivi karibuni wananchi
mbalimbali kutoka katika Halmashauri ya Iringa wametoa malalamiko yao kuwa serikali
haiwajibiki ipasavyo kutokana na upatikanaji wa pembe jeo kuwa mgumu licha ya
serikali kuimba wimbo wa kilimo kwanza.
Halmashauri ya iringa ambayo
ina vikundi vingi vilivyoundwa na mradi wa MUVI pembejeo imekuwa ni kitu cha
nadra kwa kile kilichoelezwa kuwa hakuna mpango mzuri wa ugawaji wa ruzuku
hiyo.
Wakulima mbalimbali walitoa
maoni yao kuwa
hakuna haja ya kuzungumzia masuala ya pembejeo wakati upatikanaji wake unakuwa
mgumu na hata zikipatikana gharama yake haifikiwi kiurahisi.
Mradi wa MUVI unaonesha
matumaini kwa wakulima kutokana na wengi ambao wako kwenye vikundi kuonesha
mafanikio ya maendeleo ya kilimo bora.
Mradi wa MUVI unatekelezwa kwa
mfumo wa dhana ya mnyororo wa ongezeko la thamani kwa upande wa zao la
nyanya na alizeti mkoani Iringa.
Licha ya serikali kulalamikiwa
kwa ukosefu wa pembejeo, Wazili Mgimwa, ameendelea na ahadi za mkopo kwa
wakulima wanaozingatia yale yote yanayopaswa katika kufanikisha kilimo bora
hasa kufuata ushauri wa wataalamu mbalimbali hasa MUVI.
Alisema mkulima anayefanya vizuri katika shughuli yake anakopesheka ili alime kitaalam na azingatia kanuni za kilimo bora hapo anaweza kukopesheka.
“Hakuna asiyekopesheka, kila
mtu anayejishughulisha na shughuli
yeyote halali inayeonekana anasifa za kupata
mkopo kutoka kwenye taasisi mbalimbali za kifedha, ila mkopaji lazima aoneshe jitahada na ufanisi wa
hali yajuu utakaomridhisha mkopeshaji; tatizo wakulima wengingi wanalima bila
kuzingatia kanuni za kilimo bora, hawapandi kitaalam, hawatumii mbolea na wala
hawazingatii kile wanachofanya halafu wanasema hawakopesheki, hakuna benki au mtu binafsi anayeweza kukopesha mkulima
wa aina hiyo” alisema.
Wakulima wa nyanya na alizeti wilaya za Iringa, Kilolo na Njombe wana bahati
kubwa kwa kuwepo kwa Mradi wa MUVI unaojihusisha na kuongeza thamani katika
mazao hayo ambapo wamekuwa wakipata mafunzo ya kilimo bora, elimu ya
ujasiriamali, elimu ya biashara na mawasiliano pamoja na elimu ya namna ya kuandaa mpango biashara na sifa za kukopesheka.
Kilimo ni sekta kubwa inayopaswa kuheshimiwa kwa kuwa Taifa na mtu mmoja mmoja wanategemea kilimo
ili waweze kujikimu kimaisha sanjari na kupambana na baa la njaa.
Awali Katibu wa shirikisho la
wakulima wa nyanya na mali mbichi, Magnus
Kimbe akisoma risala kwa niaba ya wenzake, pamoja na mambo mengine alimuomba
Wazir Mgimwa kuwa msimamizi wa shirikisho lao ili waweze kuwa na mshikamano.
Hata hivyo Mgimwa aliwataka
kufanya marekebisho ya katiba yao
ili kuingiza kipengele hicho ili awe tayari kushirikiana nao kwa pale
watakapomhitaji.


No comments:
Post a Comment