masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Friday, January 25, 2013

CCM walalamikiwa kununua wanafunzi wa vyuo vikuu Iringa


CHAMA cha Mapinduzi (CCM) mkoani Iringa kinalalamikiwa kuwaandaa vijana kwa ajili ya kuhujumu chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ili kudhoofisha harakati za mabadliko.
Taarifa zilizolifikia gazeti hili zinaeleza kuwa CCM imeandaa wanafunzi 200 katika Chuo Kikuu kishiriki cha Mkwawa ili waweze kutumika katika mkutano unatarajiwa kufanyika leo katika viwanja vya Mwembetogwa katika Manispaa ya Iringa.
Taarifa zinasema CCM wametengeneza kadi na fulana zenye nembo ya Chadema ambapo wanafunzi 200 wa Mkwawa wamepewa kadi hizo na shilingi 5,000/= kila mmoja ili wajifanye kama wanachama wa Chadema ili waweze kurudisha katika mkutano huo utakaofanywa na Philip Mangula.
Rais wa serikali ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mkwawa Mtama Joseph amethibitisha kuwepo kwa taarifa hizo ndani ya chuo hicho na kusema kuwa njia inayotumika ni watu waliopoteza mwelekeo.
“Ni kweli kuna taarifa kama hizo zimezagaa hapa chuoni na kama unavyosema ni kweli kwamba kwa mujibu wa taarifa ninazozikia hapa chuoni kuna wanafunzi 200 ambao inasemekana wamepewa shilingi 5000 kila mmoja na kupewa kadi zenye nembo ya Chadema ili warudishe kwenye mkutano wa CCM utakaofanyika kesho 26 Januari mwaka huu katika viwanja vya Mwembetogwa” alisema.
Mtama alisema watu walioshindwa kufikiri na kuwajibika hutumia mbinu chafu kwa kuwa hawana fikra zingine na kwamba wanaotumia rushwa ni wale waliofeli kung’amua wajibu wao na kufiki rushwa ndiyo njia sahihi.
“Watu walioshindwa kung’amua mambo na kuwajibika hutumia rushwa kama njia mbadala kwao kwa kuwa hawana kitu kingine cha kufanya. Lakini ambacho ninaweza kusema ni kwamba watu wanapokubali kununuliwa kwa muda mfupi wafikiri baadaye wataishije. Ila inapofika wakati wa kufanya maamuzi wawatupilie mbali watu wanaotumia njia kama hizo ili liwe fundisho kwao” alisema Mtama.
Awali Katibu wa Chadema katika Manispaa ya Iringa Suzan Mgonukulima alisema kuna mbinu chafu zilizobainika kutumika kuhujumu Chadema ambazo wananchi wanatakiwa kuwa nazo makini.
Alisema kuna baadhi ya watu ambao wametengeneza kadi na fulana (t-shirt) zenye nembo ya Chadema ili kutumika katika mikutano na watu kwa kujivua uanachama wa chama cha Chadema kwa kurudisha kadi hizo kama njia ya kukidhoofisha chama.
Mgonukulima alisema kutokana na hilo itakapotokea mahali popote tendo hilo linafanyika wananchi wanatakiwa kujua kuwa ni mchezo mchafu uliotengenezwa na na watu.
Alisema kwa yoyote atakayefanya hivyo na kubainika kuwa anatumiwa na si mwanachama wa chama cha Chadema atachukuliwa hatua kali za kisheria ili aweze kueleza uanachama wake katika chama cha Chadema ulitoka wapi na kadi aliyoirudisha ilitoka wapi na alipata kwa njia zipi.
Naye Katibu mwenezi wa Chadema katika Wilaya ya Iringa mjini Joseph Mgima alisema kutokana na hujuma wanazofanyiwa Chadema mara kwa mara wamekuwa wakitoa taarifa kwa jeshi la polisi lakini kumekuwa na ukimya hali inayoonesha kupuuzwa na jeshi hilo bila sababu.
“Tumekuwa tukihujumiwa mara kwa mara na kila tunapohujumiwa tumekuwa tukitoa taarifa kwa jeshi la polisi lakini hakuna hatua iliyochukuliwa hadi sasa jambo linaloonesha kusababisha uvunjifu wa amani” alisema.
Alisema baadhi ya wanachama wamekuwa wakitumiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kukihujumu Chadema kwa kuahidiwa kupewa shilingi laki tano kila wanapofanikisha.
Alisema katika mkutano wa CCM uliofanyika katika maeneo ya Soko Kuu katika Manispaa ya Iringa jumapili iliyopita baadhi ya wanachama waliotumika kama wasanii kwa kuihujumu Chadema walitoboa siri hiyo.
Kwa upande wake Kaimu Mwenyekiti wa Chadema katika Manispaa ya Iringa Charles Ndenga alisema mbinu inayotumika kwa kuhujumu chama chake ni watu wasio na fikra ambao wanasubiri kufa na kuzikwa kisiasa.
“Cha ajabi ni kwamba viongozi wa CCM wanatoka katika ofisi zao wakijua kabisa ilani yao haijatekelezwa na kufika kwa wananchi na kunadi uongo wa maneno hali wakijua kabisa wanawahadaa wananchi na badala yake wanaamua kutengeneza mbinu chafu za kuhujumu vya vingine vyenye hoja za msingi” alisema.
Diwani wa Kata ya Mivinjeni Frank Nyalusi (CHADEMA) ambaye pia ni mjumbe wa kamati tendaji ya Wilaya alisema propaganda za CCM ni sawa na mtoto anayekula vumbi bila kujua anakula kitu gani.
“Kila wakati nazishangaa sana propaganda za CCM kwa sababu zinafanana na mtoto anayekula vumbi bila yeye kujua anachokula. Hizo ni dalili za mtu aliyekufa huku akitembea akisubiri kuzikwa. CCM wanatapatapa kwa sababu wanajua kuwa mwaka 2015 wanaachia ngazi na Chadema tunashika dola” alisema.
Katika hatu nyingine mmoja wa vijana wanaosemekana kutumiwa na CCM kwa kukihujumu Chadema amefunguka mbele ya gazeti hili akisema kuwa ameahidiwa shilingi laki tano (500,000/=) na CCM pindi atakapofanikisha hujuma hiyo.
Kijana huyo ambaye aliomba jina lake lisiandikwe kwa ajili ya usalama wake alisema tayari kuna vijana 17 ambao wameandaliwa kwa kazi hiyo na tayari zimekwisha kutengenezwa fulana 200 na kadi 370 na CCM zenye nembo ya Chadema ili ziweze kutumika katika matukio mbalimbali yakiwemo ya kuanzisha fujo katika mikutano ya Chadema ili Chadema iweze kuchafuka pamoja na kadi kutumika katika mikutano ya CCM kawa wanachama kurudisha kadi na kujiunga na CCM.
Akifafua zaidi alisema njia itakayotumika ili kuwachanganya wananchi, CCM wamepanga kusomba wakulima vijijini kwa magari na kuwagawia kadi hizo walizozitengeneza ili watumie majukwa kama kurudisha kadi kwa ajili ya kuwatumainisha wananchi kama Chadema hakifai.
“Nakuomba ndugu mwandishi, nimekwambia hayo yote lakini usiniandike katika gazeti. Yapo mengi lakini kama unavyoona hali ilivyo kwa leo tuishie hapa wasije wakanishtukia. Kwa usalama wangu naomba usiniandike jina” kilisema chanzo chetu.
Wakatika hayo yakizungumzwa katika wa CCM Mkoa wa Iringa Emanuel Mteming’ombe alisema katika mkutano utakaofanyika leo katika viwanja hivyo wanatarajia kupokea wanachama wapya kati ya 400 hadi 500.
Alisema katika mkutano huo ambao utafanywa makamu mwenyekiti wa CCM Philip Mangula, atapokewa na wanafunzi wa vyuo vikuu vya mjini Iringa ambao watakuwa wateja wakubwa wa kuingia katika chama chake.

 “Baada ya mkutano wake wa hadhara siku ya pili atakutana na viongozi wa chama cha Mapinduzi Mkoa wa Iringa kufanya tathimini ya ziara yake kabla ya kurejea jijini Dar es Salaam,hata hivyo ziara hiii ni fupi lakini badaye atakuja kufanya ziara katika Wilaya zote za mkoa wa Iringa”alisema.
Mtemeng’ombe alisema miongoni mwa waanchama wanaotarajia kujiunga na CCM wengi wanatoka katika vyuo vikuu vilivyopo mkoani hapa alivyovitaja kuwa ni Mkwawa, Tumaini, Ruaha (RUCO) na baadhi yao ni vijana walio katika Manispaa ya Iringa Mjini.
“Hawa tunaowaingiza kuwa wanachama wa CCM ni wale tuliofanyia usaili kwa muda mrefu, tumewafundisha katiba ya chama,namna ya kuishi maadidli ya chama na kanuni tunazozitumia,sisis hatuchukua wanachama barabarani bali tunafuata taratibu tulizojiwekea na ndio sababuwanachamwetu ni wa uhakika” alisema Mteming’ombe na kuongeza.

No comments:

Post a Comment