| Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania Mhashamu askofu Tarcisius Ngalalekumtwa akihubiri katika Kanisa la Bikira Maria Consolata - Mshindo. |
| Mhashamu askofu Evaristo Chengula wa jimbo Katoliki la Mbeya akimuwekea mikono Shemasi Deogratias Lyimo Mtika. |
| Shemasi Deogratias Lyimo Mtika akiwa amelala kifudifudi wakati wa kusali litania ya watakatibu wakati wa kuwekwa daraja la upadre. |
| Pd. Deogratias Lyimo Mtika mara baada ya kupata daraja Takatifu la upadre. |
MAKUHANI wametakiwa kudumisha heshima ya wazee kwa kufuata mongozo wa
uchungaji katika kazi zao za kiroho ili waweze kuwa watumishi waaminifu katika
kutekeleza kazi waliyokabidhiwa.
Haya yamezungumzwa na Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania Mhashamu
askofu Tarcisius Ngalalekumtwa katika Misha ya daraja la upadre iliyofanyika
leo katika Kanisa la Bikira Maria Consolata Parokia ya Mshindo katika jimbo la
Iringa.
Mhashamu askofu Ngalalekumtwa ambaye pia ni askofu wa jimbo hilo amesema
kazi ya kuhani ni kuelekeza na kufundish ayaliyomema pamoja na kuwashauri
waliopoteza mwelekeo wa amani kurudi katika kutenda haki.
Amesema kuhani anapoacha kazi anayotakiwa kufanya na kujiingiza katika
upotoshaji ni hatari kwani huwa ni chanzo cha amani kupotea na kujipotezea
imani kwa watu wanaomtegemea kimawazo na kimtazamo kwa kufuata njia iliyo
sahihi.
Amesema kazi ya utume si ya mzaha na hivyo kila wakati lazima Mungu
apewe nafasi ya kwanza kwa kila anachotaka kukifanya ili kiwe na baraka kwa
ajili ya watu.
“Bidii ya kusali iwe mbele ili Mungu azidishe nguvu katika utendaji na
kutoa maamuzi yaliyosahihi kwa ajili ya kupatanisha na kufundisha; kulegea
kusali ni kukaribisha udhaifu wa mafundisho ya kweli nay a haki” amesema.
Amewataka kutoona aibu katika kukiri imani na kusimamia imani popote
kwani kufifia kiimani ni kukaribisha mvurugano katika uadilifu na utumishi.
“Hubirini kwa bidii bila kuionea aibu imani yenu kwani mkilegea tu
mtakuwa mmekaribisha kupotea kwa maadili yenu na utumishi wenu utakuwa ni wa
mashaka” alisema.
Amesema kuwa popote wanapofanya kazi wanatakiwa kuwa na mahusiano mazuri
na watu wanaowatumikia ili amani na upendo viendelee kuwepo kwa ajili ya
kulijenga taifa la Mungu.
“Watumikieni watu wote bila kubagua kwa kuwa na mahusiano mazuri
mkihubiri amani, upendo na mshikamano ili taifa la Mungu liendelee kuwa na
upendo. Mkiwa kinyume na hayo mtatowesha amani na kusambaratisha watu kwa
kuwagawa katika matabaka na makundi yasiyo na sababu” amesema.
Hata hivyo amewataka wasitawaliwe na mambo ya kidunia yaliyo kinyume na
maadili ya utumishi wao ili kuendeleza heshima ya uadilifu na upendo.
“Kumbuka unapowekewa mikono na wazee, heshima yao iendelee kupitia tabia
na maadili yako unapokuwa kwenye huduma. Usiwe mtu mwepesi kiasi cha kudharaulika
kitabia na kiuadilifu” amesema.
Misa hiyi ilikwenda sambamba na utoaji wa daraja takatifu la upadri kwa
Shemasi Deogratias Lyimo Mtika wa shirika la wamisionari wa Biokira Maria
Consolata huku ikihudhuriwa na Mhashamu askofu Evaristo Chengula wa jimbo la Mbeya pamoja na viongozi
mbalimbali wa dini na serikali.
No comments:
Post a Comment