masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Friday, November 2, 2012

Safari ya kumsindikiza Padre Salutaris Lello Massawe ndivyo ilivokuwa. Matukio haya ni sehemu ya mwisho.

Asko wa Jimbo la Iringa Mhashamu Tarcisius J.M. Ngalalekumtwa akiweka shada juu ya kaburi la marehemu Pd. Massawe.

Asko wa Jimbo la Singida Mhashamu Desderius Rwoma akiweka shada juu ya kaburi la marehemu Pd. Massawe.

Asko wa Jimbo la Njombe Mhashamu Alfred Maluma akiweka shada juu ya kaburi la marehemu Pd. Massawe.

Asko wa Jimbo la Mbeya Mhashamu Evaristo Chengula akiweka shada juu ya kaburi la marehemu Pd. Massawe.


Kaka wa Marehemu Pd. Massawe akiweka shada juu ya Kaburi.

Mama wa marehemu Pd. Massawe Maria Illuminata akiweka shada juu ya kaburi la mwanawe.

Sr. Pascalina Mkolomi wa Consolata akiweka shada juu ya kaburi akisaidiwa na Mhashamu askofi Ngalalekumtwa.


Add caption

Wanafamilia ya Pd. Massawe wakiwa mbele ya kaburi baada ya mazishi.

Wanafamilia ya Pd. Massawe wakiwa mbele ya kaburi.

Wanafamilia wakiwa mbele ya kaburi.


 Padre Salutaris Lello Massawe alizikwa kichifu kwa kupigiwa mizinga hewani kutambua uwajibikaji enzi za uhai wake.

Pd. Massawe ameitwa na Mungu wakati ambao shirika lilikuwa bado linamhitaji kwa ajili ya uwajibikaji wake hasa katika kulitumikia shirika, Mungu na kuchunga kondoo wa Bwana aliokabidhiwa.

Bado ni kama ndoto kwa waamini hasa jimboni Iringa ambako makao makuu ya shirika la Consolata Tanzania yapo japo kuwa hawana budi kuyapokea mapenzi ya Bwana aliye muumbaji.

Padre Salutaris Lukas Massawe Lello alizaliwa Moshi Julai 8, 1962. Baba yake ni Lukas Victor na Mama, Maria Illuminata Manka.

Alisoma katika shule ya msingi ya Singachini kati mwka 1971 – 1978, akajiunga katika seminari ya Maua ambapo alisoma mpaka 1985, alipohitimu masomo ya sekondari.

Mwaka 1985 alianza masomo ya falsafa na teolojia katika seminari ya Consolata ya Nairobi na kuhitimu mwaka 1988 alipoanza unovisi. Alimaliza unovisi mwaka 1989 na akafunga nadhiri za kwanza 21 Julai 1989 Sagana (Kenya).

23 Oktoba 1992 alifunga nadhiri za milele Nairobi na 28 Novemba 1992 akapewa daraja la ushemasi.

Julai 27, 1993 alipewa daraja la upadre Moshi kwa kuwekewa mikono na Mhashamu Baba Askofu A. Msarika.

Pd. Massawe alifanya kazi ya umisionari katika nchi ya Ethiopia kutoaka 1995 hadi mwaka 2000 baada ya hapo akatumwa Italia akifanya kazi ya uhamasishaji wa roho ya umisionari hadi mwaka 2007 aliporudi Tanzania.

Baada ya kusoma katika Chuo Kikuu cha Mt. Augustino Mwanza, akatumwa Bunju, Dar es Salaam kwa ajili ya shughuli za gazeti la wamisionari wa Consolata “Enendeni. Kutoka Septemba 7, 2011 alikuwa Baba Mkuu wa Shirika la Wamisionari wa Consolata nchini Tanzania.

Pd. Massawe alifariki Oktoba 25, 2012 Bagamoyo kwa ajali ya Maji na kuzikwa Oktoba 30, 2012 katika makaburi ya Jimbo yaliyopo Tosamaganga.

Mazishi hayo yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali na madhehebu ya kidini kutoka ndani na nje ya nchi ambapo jumla maaskofu wanne walihudhuria mazishi hayo.

Maaskofu hao ni pamoja na Mhashamu Desderius Rwoma wa Jimbo Katoliki la Singida, Mhashamu Alfred Maluma wa Njombe, Mhashamu Evaristo Chengula wa Mbeya pamoja na Mhashamu Tarcisius Ngalalekumtwa wa Iringa ambaye pia ni Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania.

Mungu aiweke roho yake mahala pema ……. Amina



Hapa ndipo tunakomea kwa matukio ya Mazishi ya Pd. Salutaris Lelllo Massawe. Mungu akubariki kwa kufuatilia matukio haya mpaka mwisho. Samahani kwa usumbufu uliojitokeza.

No comments:

Post a Comment