masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Tuesday, November 6, 2012

Mhashamu Askofu Aloysius Balina afariki

Mhashamu askofu Aloysius Balina  wa Jimbo Katoliki la Shinyanga amefariki dunia akiwa katika hospitali ya rufaa ya Bugando jijini Mwanza alipokuwa akitibiwa.

Mauti hayo yamemkuta leo majira ya saa 5 asubuhi katika hospitali hiyo wakati madaktari na wauguzi mbalimbali walipokuwa wakifanya juhudi za kuiokoa uhai wake


Mhashamu Askofu Aloysius Balina alizaliwa Juni 21, 1945 katika kijiji cha Isoso Ntuzu wilayani Bariadi mkoani Shinyanga akwekwa wakfu na Papa Yohane Paulo II mwaka 1984 kuwa Askofu wa Geita na kusimikwa Machi 10, 1985.
 
Septemba 23, 1997 alihamishiwa Jimbo la Shinyanga na kuwa Askofu wa tatu wa Jimbo la Shinyanga hadi mauti yalipomkuta, huku watangulizi wake wakiwa Askofu Edward A. Mc Gurkin, aliyetumikia cheo hicho toka mwaka 1956 hadi 1975, alifariki Agosti 28, 1983 huko Marekani, wa pili ni Askofu Castor Sekwa, aliyetumikiwa kuanzia mwaka 1975  hadi  Juzi 6, 1996 alipofariki na askofu Balina kushika nafasi yake.
 
Mpango wa wazishi unaendelea kufanyika na taarifa zaidi tutaendea kupata.
 
Mungu aiweke roho yake mahala pema ............ Amina.

No comments:

Post a Comment