| Mtuhumiwa wa mauaji ya aliyekuwa Mwandishi wa kituo cha Runinga cha Channel Ten katikati aliyevaa jaketi jeupe akifikishwa mahakamani leo. |
| Aliyejifunika kofia ya jaketi jeupe ni mtuhumiwa wa mauaji ya aliyekuwa mwandishi wa kituo cha runinga cha Channel Ten alipokuwa mahakamani leo. |
MTUHUMIWA wa mauaji ya aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo cha
runinga cha Channel Ten Daud Mwangosi amefikishwa mahakamani leo katika ulinzi
mkali huku waandishi wa habari wakizuiwa kupiga picha.
Askari
wa kikosi cha kuzuia ghasia wengine wakiwa na virungu, silaha za moto huku
wengine wakivaa kiraia walitandaa mahakamani hapo kuhakikisha waandishi wa
habari hawapati mwanya wa kupiga picha.
Wakili
wa serikali ambaye pia aliendesha mashtaka ya mtuhumiwa huyo Lilian Ngilangwa
aliambia mahakama mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Dyness Lyimo kuwa upelelezia
wa kesi hiyo haujakamilia.
Pasificus
Cleophace Simon (23) alifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi kwa tuhuma ya
kumuua kwa makusudi mwandishi huyo katika ufunguzi wa matawi ya Chama cha
Demokrasia na Maendeleo CHADEMA katika kijiji cha Nyololo Wilaya ya Mufindi
Mkoa wa Iringa uliofanyika Septemba 2 mwaka huu.
Mtuhumiwa
huyo mwenye namba G 2573 alifikishwa mahakamani hapo kwa gari la polisi lenye
namba PT 1467 likiwa na ulinzi mkali.
Siku
ya kwanza mtuhumiwa huyo alifikishwa mahakamani hapo kwa gari la kifahari lenye
namba za kiraia T 320 ARC linalosadikiwa kuwa ni la RCO huku kwa mara ya
pili akifikishwa kwa miguu na kuondolewa mahakamani hapo kwa gari namba DFP
2175 pic up akiwa katika ulinzi mkali huku waandishi wa habari wakidhibitiwa na
polisi na mmoja wao kunusurika kupigwa jambo lililozusha hisia tofauti miongoni
mwa wananchi wengi mkoani hapa.
Kwa
mujibu wa wakili huyo, upelelezi haujakamilika na kesi imeahirishwa hadi
Novemba 07 mwaka huu itakapotajwa tena.
Wakati
waandishi wahabari wakiwajibika mahakamani hapo kutafuta uwezekano wa kumpiga
mtuhumiwa huyo picha, mwandhishi wa habari wa gazeti Majira Eliasa Ally
amepigwa na askari akizuiliwa kupiga picha.
Askari
aliyempiga mwandishi huyo ametambuliwa kwa jina moja la Idirisa jambo
ambalo limezua hisia mbalimbali miongoni mwa waandishi hao pamoja na wananchi
waliokuwepo katika tukio hilo.
Mwangosi
aliuawa kwa bomu Septemba 2 mwaka huu katika kijiji cha Nyololo alipokuwa
akiwajibika kwa kazi za kihabari wakati wa ufunguzi wa matawi hayo.
No comments:
Post a Comment