| Wanchi wa kijiji cha Mkalanga wakisoma magazeti huko kijijini |
Mtandao huu umeshuhudia wananchi wa kijiji cha Mkalanga Kata ya Ukwega Wilaya ya Kilolo wakiwa wamekusanyana kusoma magazeti hayo kujua kinachoendelea nchini.
Wakizungumza na mtandao huu wananchi hao wamesea kuwa licha ya kuwa wanasikia kuwa kuna vyombo vingi vya habari, magaeti yanayowafikia ni hayo tu.
Wakiwa na furaha kuyapata magazeti hayo, wametoa ombi kwa wamiliki wa vyombo vingine kuwa wafanye jitihada kuwafikia wananchi wa vijijini kama wanavyofanya wengine.
Mtandao huu umebaini kuwa Kata za Ukwega, Udekwa, Kimala, Idete, Mtitu, Dabaga, Bomalang'ombe wananchi hawajui vyombo vya habari ni nini pamoja hata redio zinawafikia kwa taabu.
No comments:
Post a Comment