| Thomas Lubanga |
Mbabe wa kivita kutoka Congo, Thomas Lubanga, amehukumiwa kifungo cha miaka 14, baada ya kupatikana na hatia ya kuwasajili watoto katika jeshi lake kati ya mwaka wa 2002 na 2003.
Lubanga alipatikana na hatia na mahakama ya kimataifa ya jinai ICC mwezi Machi mwaka huu.
Hukumu hiyo ndiyo ya kwanza kutolewa na mahakama hiyo ya ICC iliyoundwa miaka 10 iliyopita.
Lubanga amekanusha mashtaka yote dhidi yake akisema hakuna kosa alilofanya na kwamba hakuunga mkono watoto kutumiwa kama wanajeshi.
Lakini majaji waliokuwa wakisikiliza kesi hiyo, walikubaliana kwa kauli moja kuwa Lubanga alikuwa na hatia.
Cource: bbc swahili
No comments:
Post a Comment