Uhamasishaji
wa ujenzi huo unakuja baada ya wanakiji kufyatua matofali kwa kushirikiana na
wadau wengine kwa ajili ya kusaidia ukuaji wa elimu vijijini kwa jamii nzima.
Akizungumza
na mtandao huu, mhamasishaji wa mradi huo Bovani Mwakyambiki amesema ili
kufikia malengo ya mradi huo kwa ananchi asasi inategemea michango ya wananchi
wenye kupenda mabadiliko ya kielimu na kwamba kila mmoja anayo nafasi ya kutoa
ushiriki wake.
“Baada
ya kuwaelimisha wanakijiji wa Lugalo na viongozi wa kijiji na kata, uongozi wa
kijiji uliweza kutenga eneo, Uongozi wa kijiji kwa kushirikiana na watendaji wa
Tuwafikie wakahamasisha ushiriki wa wanakijiji katika ufyatuaji wa tofali.
“Nguvu
kubwa ya kukamilisha zoezi hili ilikuwa ni ya wananchi wenyewe kwa kushirikiana
na uongozi wa kijiji cha lugalo, tanuri lilijengwa na tofali zikachomwa. Hivyo
bado tunaendelea kusonga mbele na shughuli iliyopo mbele yetu ili tujenge kwa
haraka maktaba hiyo na baadaye tuendelee mbele” amesema Mwakyambiki.
Ikiwa
sehemu ya kujenga maktaba hiyo imekamilika, Mwakyambiki alisema wadau
mbalimbali wa elimu na wale wanaopenda mabadiliko ya elimu wanayo nafasi ya
kutoa michango yao kwa ajili ya kuendeleza gurudumu la ujenzi huo.
Amesema
baada ya kuonana na kampuni ya interbeton iliyopo Mazombe na kuongea nao kuhusu
uhitaji wa mchanga, mawe na kokoto, na baada ya kuwaeleza umuhimu wa maktaba ya
kijiji kwa wanakijiji cha lugalo, kupitia mkurugenzi mkuu wa mradi wa ujenzi wa
barabara Mr Hans Jorgen Kallehauge waliweza kupata mchanga na kokoto za kutosha
Licha
ya kupata mchanga na kokoto za kutosha pamoja na tofali, asasi hiyo bado ina
uhitaji wa fedha kwa ajili ya kununua saruji na Kukusanya mawe tayari kwa
kuanza ujenzi.
Ameeleza
kuwa harakati hizi zitahusisha wadau wote wa maendeleo ya elimu, kuanzia
Marafiki wa elimu, Taasisi mbalimbali za kiserikari na zile zisizo za
kiserikari, Makampuni na watu binafsi.
Amesema
shughuli zote za Tuwafikie Tanzania ni shughuli zinazotegemea mwamko na
ushirikiano wa wadau wote waliopo katika maeneo au mikoa husika.
“Hii itasaidia kufanikisha maono ya kuhakikisha Maktaba za
Jamii zinajengwa na kupatikana maeneo ya vijijini ili kupunguza ujinga
unaosababishwa na ukosefu wa Taarifa, ukosefu wa ujuzi na Elimu na Jamii
kutokuwa na uwezo wa Kujitambua.
“Kuchangia mfuko wa Tuwafikie Tanzania ni Ishara ya
kutuamini, na kitendo cha sisi kupokea mchango wako ni ishara ya Kujiamini na
kuwa na hakika na kiu ya kutimiza malengo ya kuhamasisha maendeleo ya elimu
vijijini kwa kushirikIana pamoja nawe” amesema.
Tuwafikie
Tanzania ni Asasi iliyoanzishwa kuhamasisha
Usomaji, Ujenzi na Matumizi ya Maktaba vijijini (Community Libraries).

No comments:
Post a Comment