masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Friday, June 27, 2014

WAANDISHI WAACHILIWA SYRIA NA WAPIGANAJI

Waandishi wa habari na wapiga picha wanaofanya kazi na gazeti la Times wameachiliwa baada ya kutekwa nyara na kundi la waasi nchini Syria.

Wote wawili, Anthony Lyod na Jack Hill, ambao wana ujuzi wa muda mrefu wa kuandika na kupiga picha za habari, walikuwa wakirudi kutoka eneo la Aleppo, Syria, walipotekwa nyara na kundi la wapiganaji karibu na mpaka wa Uturuki.

Bwana Hill alijaribu kutoroka lakini alikamatwa na kupigwa vibaya.

Bwana Lyod pia alipigwa risasi miguuni mara mbili kumzuia kutoroka na pia akapigwa vibaya.
Waandishi hao wa habari walisema kuwa waliachiliwa baada ya kuingilia kwa kundi kubwa la waasi nchini Syria la, Islamic Front.

Chanzo: bbc shwahili

No comments:

Post a Comment