![]() |
| Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere enzi za uhai wake. |
| Waziri Stiphen Wassira akiwa kanisani hii leo. |
| Baadhi ya Mapadre wakiwa kanisani wakati wa maadhimisho ya Misa ya Kumkumbuka Baba wa Taifa. |
| Mkuu wa Mkoa wa Iringa Dkt. Christine Ishengoma pamoja na viongozi wengine wakiwa kanisani wakati wa maadhimisho ya Misa ya kumkumbuka Baba wa Taifu Mwalimu Nyerere. |
| Mhashamu askofu Tarcisius Ngalalekumtwa akipokea matoleo kanisani. |
| Shemasi Paul akisoma somo la Injili kanisani. |
| Waziri wa Serikiali za Mitaa (TAMISEMI) William Lukuvi na nyuma yake Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini Peter Msigwa (CHADEMA) wakifuatilia Misa Takatifu kanisani. |
![]() |
| Hayati Baba wa Taifa Julius Kambarage Nyerere enzi za uhai wake. |
RAIS wa Baraza la Maaskofu
Tanzania Mhashamu Tarcisius Ngalalekumtwa amesema Watanzania tuna deni kubwa
ambalo ni jukumu la kila mmoja kulipa.
Ameyasema hayo leo wakati wa
maadhimisho ya Misa Takatifu iliyokuwa ni kwa ajili ya kumkumbuka Baba wa Taifa
Hayati Julius Kambarage Nyerere iliyofanyika kitaifa mkoani Iringa katika
Kanisa la Moyo Mtakatifu wa Yesu Parokia ya Kihesa (Kanisa Kuu la kiaskofu).
Askofu Ngalalekumtwa ambaye pia
ni askofu wa Jimbo la Iringa na msimamizi wa Jimbo Kuu la Songea amesema deni
linalopaswa kulipwa ni kufuata maadili na matendo ya haki.
“Tuna deni kubwa kwa Hayati Baba
yetu wa Taifa na deni hilo
lazima lilipwe. Deni hilo
ni kuishi kwa pamoja kwa umoja na kuheshimiana pia” amesema.
Amesema watanzania walipewa zawadi
kubwa ambayo kwayo amani ya nchi ilijengeka na heshima ya nchi ilipatikana
ambapo kila mmoja anawajibu wa kulinda tunu hizo.
“Maisha yake yalikuwa zawadi
kwetu; si kwa watanzania pekee bali kwa waafrika na dunia nzima” amesema.
Amesema Mwalimu alijitahidi
kutunza roho ya mcha Mungu huku kazi zake akizifanya kwa hofu ya Mungu.
Pia amesema Mwalimu alijitahidi
kukusanya watanzania katika kaki na kuwajengea moyo wa kumtegemea Mungu jambo
lililosaidia kulinda heshima ya nchi.
“Tusivunje matumaini kwa Mungu.
Tuzitoe nafsi zetu katika kujali Mungu na wenzetu. Tuishi kwa uchaji ili Mungu
atushushishie Baraka zake. Tukiishi kwa uchaji, hata wale hata wale tunaoishi
nao watatunza kumbukumbu tamu, nzuri na nono katika mioyo yao ” amesema.
Hata hivyo akofu Ngalalekumtwa
amewataka watanzania kuishi kwa kuheshimia katika imani ili kuendeleza
utamaduni wa kuishi kwa pamoja bila kutofautiana kwa kwa kigezo cha imani na
kwamba binadamu anahitaji huruma, ya Mungu, faraja na utakaso kwa yale machafu
anayoyafanya au kuwafanyia binadamu wenzake.
Aidha amewataka viongozi wa ngazi
zote kuwa na roho ya huruma, upendo na kuwatendea raia wake haki inayostahili.
“Kupitia Misa hii tuliombee Taifa
letu, viongozi wetu ili wawe na roho ya huruma, upendo, upole na haki. Haya
yakiwepo tukawa na viongozi wa namna hiyo, nchi itabaki kuwa ya amani.
“Tunapenda nchi iwe ya amani.
Zifike nyakati za amani, za kutulia na nyakati za kutazamana kwa raha. Uhuru wa
kuabudu uheshimiwe. Anayeviruga uhuru huu si mwenzetu na huyi ndiye anayeingiza
machafuko kwa watu wanaopenda amani” amesema


No comments:
Post a Comment