masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Tuesday, August 13, 2013

MAZISHI YA PADRI LIBERATUS MWENDA YALIVYOKUWA

Hawa ni baadhi ya ndugu waombolezaji waliokuwa kando ya kaburi.

Jeneza likuwa limeshafikishwa kando ya kaburi tayari kwa mazishi.


Askofu Evaristo Chengula wa Jimbo la Mbeya mwenye vazi jeupe na askofu Tarcisius Ngalalekumtwa mwenyevazi jeusi wakiwa kando ya kaburi,

Jeneza likiwa limefungwa kamba na kushushwa kaburini.

Jeneza likishushwa kwenye kaburi.

Baada ya jeneza kushushwa kawenye kaburi.



Watu mbalimbali wakiweka udongo kwenye kaburi.

Mapadre Victor Ngalembula akimnong'oneza jambo mwenzake padre Mkalawa.


Hii ni karuri baada ya kuzika.

Mhashamu askofu Tarcisius Ngalalekumtwa akiweka shada juu ya kaburi.

Mhashamu askofu Evaristo Chengula wa jimbo la Mbeya akiweka shada juu ya Kaburi.
Dada wa marehemu akilia baada ya kuweka shada juu ya kaburi.



Watoto wa shirika la Kipapa wakiweka mashada juu ya kaburi baada ya mazishi.



Masista na wawakilishi wa Parokia ya Nyakipambo wakiwasha mishuma katika kaburi.




Mwenyekiti wa umoja wa mapadre jimbo la Iringa (UMWAI) Padre Cephas Mgimwa akitoa pola na shukurani kwa watu mabalimbali.

RAIS wa Baraza la Maaskofu Tanzania Mhashamu Tarcisius Ngalalekumtwa amesema jimbo la iringa limepata pigo kubwa kwa kifo cha Padre Liberatus Mwenda.

Akizungumza wakati wa mahubiri katika Misa ya mazishi iliyofanyika katika Kanisa la Moyo Mtakatifu Parokia ya Tosamaganga Jimbo la Iringa, askofu Nagalalekumtwa alisema pengo alilolicha padre Mwenda ni kubwa na kwamba linaleta simanzi.

“Tuseme nini? Hatuna ugomvi na Mungu lakini yeye ndiye aliyeamua kama alivyomuumba. Tumsindikize kwa sala na maombi ili akapumzike kwa amani” amesema.

Amewaasa wakristo kuishi kwa upendo, haki na uadilifu ili kutendeana mema hapa duniana na kuacha uonezi wa makusudi kwa wengine.

“Kwa kuishi katika upendo, haki, na uadilifu katika injili, tuna uhakika wa kuufikia muunganiko na Mungu. Maombi haya ya leo iwe nguvu ya maisha yetu pamoja na kusindikiza safari ya mwenzetu kwenda kupumzika” amesema.

Hata hivyo amewataka wakristo kukubali mipango ya Mungu na kumshukuru kwa zawadi aliyotoa na kumuomba Mungu ampokee padre Mwenda katika umoja wake wa malaika.

Askofu Ngalalekumtwa ambaye pia ni askofu wa jimbo la Iringa na mlezi wa Jimbo Kuu la Songea amewataka wakristo kuomboleza kwa imani na amani ili kuendeleza utulivu katika nchi.

Amesema padre Mwenda katika uhai wake alishiriki kazi za kichungaji na kimaendeleo katika ustawi wa Kanisa na wake na kwamba alikuwa mhudumu wa kwanza katika nyumba yajimbo Nazareth iliyopo katika Jimbo Kuu la Dar es Salaam.

Padre Liberatus wakati wa uhai wake aliwahi kufanya kazi katika jimbo la Agrigento – Cicilia Italia na aliteuliwa kuwa mlezi wa vyama vyama vya kipapa vya kimisionari.


Alizaliwa Septemba 25, 1955 katika Parokia ya Wasa.

Mazishi hayo yalihudhuriwa na watu mbalimbali akiwemo mhashamu askofu Evaristo Chengula wa jimbo la Mbeya, sekretarieti ya baraza la maaskofu Tanzania, viongozi mbalimbali wa madhehebu na serikali kutoka sehemu mbalimbali.

No comments:

Post a Comment