| Mbunge wa Iringa mjini Peter Msigwa (Chadema) akihutubia wakazi wa Kihesa katika Manispaa ya Iringa. |
MBUNGE wa Iringa mjini Peter Msigwa (CHADEMA) ameendelea kusisitiza kuwa pamoja na kuwa suala la wafanyabiashara ndogo (machinga) wa mashinetatu liko mahakamani, ataendelea kupigania ili kuhakikisha hawaondolewi nje ya mji.
Msigwa amesema hayo leo
katika mkutano wa hadhara wa kiserikali uliofanyika katika uwanja wa Kihesa
katika Manispaa ya Iringa na kuwataka wananchi kuwa wavumilivu na ili wakati
akiendelea kufanya taratibu za kisheria kuwapigania haki zao.
Amesema machinga ni
watu wanaopaswa hithaminiwa kwa kuwa wanalipa kodi zao kama kawadi sawa tu na
watu wengine na kwamba inapofika mahala wananyanyaswa familia zao zinadorora.
“Pamoja na kuwa suala
la Machinga pale mashinetatu lipo mahakamani, mpango wangu kuhakikisha
hawatolewi nje ya mji upo palepale” alisema Msigwa.
Amesema watu wengi
wanafikiri kuwa cheo kinabadilisha akili ya mtu jambo ambalo wengine wamegeuka
kuwa miungu wangu kwa kutaka waheshimiwe na kupigiwa saluti hata wanapofanya
viba.
Amesema licha ya kuwa
watu huchagua viongozi wao kwa kusudi la kuwawakilisha, wapo ambao baada ya
kupata vyeo wamekuwa tofauti na matarajio ya wananchi na kugeuka kuwa kikwako
kikubwa kwa maisha ya wananchi.
“Kuna watu tumewapatia
vyeo lakini ni wapumbavu. Cheo hakibadilishi akili. Kama huna akili ukipata
cheo utabaki kuwa mpumbavu tu” amesema.
Pia amesema ikiwa mtu
anajua kusoma na asijishughulishe na kujisomea atakuwa hana utofauti na mtu
ambaye hakusoma kabisa na kwamba wajibu wa viongozi ni kutatua shida za
wananchi wake lakini wengi wamekuwa wababaishaji tu.
Naye Dady Igogo kutoka jimbo
la Rorya amesema kiongozi anayechaguliwa na watu kuwa muwakilishi na kugeuka
kuwa bubu ni hatari katika ustawi wa jamii na maendeleo kwa ujumla.
“Ukiona una muwakilishi
ambaye hawezi kuzungumzia kero za watu wake ni hatari. Kiongozi wa namna hiyo
hafai kuendelea kuwa muwakilishi na pia anakuwa ametudharau tuliyempa dhamana
hiyo.
“Msigwa ni nyuki ambaye
hakumbatiwi na watu wahuni. Wote wanaombeza Msigwa ni wahuni ambao wanataka
kufanya mambo yao kihuni. Tusikubali kuendelea kuwa na wahuni. Tuwakatae watu
wa mtindo huo” alisema Igogo.
No comments:
Post a Comment