![]() |
| Nape Nnauye |
VIONGOZI wa Chama cha
Mapinduzi (CCM) wameonja joto la jiwe baada ya kufukuzwa kwa nyengo na shoka
katika kata ya Ng’ang’ange walipofika kuvamia kiwanja kwa ajili ya mkutano
bila kibali cha mwenye kiwanja.
Hayo yalitokea jana
katika kijiji cha Mdeke ambapo walifika jioni kwa ajili ya kufanya mkutano bila
kuomba kibali cha mwenye kiwanja na kujikuta katika wakati mgumu baada ya
familia inayomiliki kiwanja hicho kutokea wakiwa na silaha na kuwavurumusha.
Dhahama hiyo iliwakuta
viongozi wa CCM akiwemo mwenyekiti wa chama hicho wa Iringa mjini Said
Kiponza na mwenyekiti wa umoja wa vijana (UVCCM) Wilaya ya Kilolo Sifuni
Makongwa.
Akiongea na mtandao huu mmoja wa familia hiyo ambaye ameomba jina lake lisiandikwe gazetini
alisema imefika wakati sasa kukataa kudharaulika na watu wanaotaka kutumia
madaraka yao kwa manufaa yao binafsi.
“Ni kweli tumefanya
hivyo kwa sababu tuliona ni dharau kubwa. Eti mtu anakuja nyumbani kwako bila
kupiga hodi na kuanza kufanya atakacho kana kwamba hakuna mwenye nacho. Hii inaonesha
jinsi walivyo na mabavu kutaka kila kitu kuwa ni chao eti kwa kuwa wapo
madarakani.
“Kwa nafasi hii
napenda kuwaambia kuwa muda wa kunyanyasika umekwisha. Sasa tuheshimiane,
hakuna mtu ambaye yupo usingizini sasa hivi kama walifikiri bado tupo
usingizini wamechemka. Na kibaya zaidi kwa nini waje usiku kama siyo unyang’anyi
huo” kimesema chanzo chetu.
Sifuni Makongwa
alipotafutwa kwa njia ya simu ili kutolea ufafanuzi wa kile kilichodaiwa na
familia hiyo amesema hakuwepo katika tukio hilo na kwamba hajui ni nani yupo
kule ambaye anaweza kutoa maelezo.
“Mimi sikuwepo katika tukio
hilo. Nipo mjini lakini sijajua ni nani yupo kwenye kampeni huko Ng’ang’ange
ambaye anaweza kukupatia majibu!” amesema.
Hata hivyo Kiponza
alipoulizwa kwa njia ya simu alikiri kuwepo na tukio hilo na kwamba hayo ni
mapito tu.
“Si unajua mambo ya
hapa na pale! Ni Bibi kizee mmoja pamoja na wanawe walituletea usumbufu kidogo
lakini tumemalizana nao. Ni kweli hakukuwa na taarifa ya kufanya mkutano hapo
lakini basi yametokea tutarekebisha yasitokee tena” amesema Kiponza.
Alipotakiwa kufafanua
zaidi ni kwa nini kufanya mikutano kwa kuvamia, Kiponza hakuwa na jibu.
Katika hatua nyingine
mikakati ya kutaka kumrubuni mgombea udiwani katika kata hiyo kupitia Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Nafred Lucas Chahe imegundulika.
Taarifa zilizopatika
ndani ya CCM zimeeleza kuwa waameandaliwa watu maalumu kwa ajili ya kuhakikisha
mgombea huyo anarubuniwa kwa gharama yoyote na kwa njia yoyote ili mradi wakati
wa uchaguzi asipite.
Kwa mujibu wa chanzo
chetu taayari mipango ya kuanza kumtafuta mgombea huyo kwa ajili ya kuingia
mkenge imeanza na sasa ameanza kupigiwa simu ili kukutana na watu hao.
Alipotafutwa kwa ajili
ya kuthibitisha, mgombea huyo alikiri kupigiwa simu mara kadhaa na watu tofauti
tofauti kutaka wakutane naye Katika kijiji cha Kidabaga na wakati mwingie
wakitaka kukutana naye mjini.
“Ni kweli napigiwa simu
mara nyingi wakitaka nikutane nao eti kwa madai kuwa wanataka kuniongezea uwezo
wa kupiga kampeni lakini nakataa kila wakati na sehemu wanazotaka nikutane nao
si nzuri kwangu” amesema Chahe.
Namba zinazotumika
kumpigia mgombea huyo ili kukutana yane zimetajwa (tunazo zinahifadhiwa).
Katika utafiti
uliofanywa na mtandao huu umebaini kuwa namba zilizotajwa kutumika wamiliki wake wote ni kada wa CCM

No comments:
Post a Comment