masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Friday, March 8, 2013

Wakulima watumia mbao za matangazo

Nelson Mbimbi mkazi wa kijiji cha Kising’a Mkoani Iringa akihojiwa na mwandishi juu ya mafanikio yake kutokana na kilimo cha alizeti. Pikipiki ni mali yake ambayo ni mafanikio ya kilimo.

Ubao wa matangazo kwa wajasiriamali uliojengwa katika kijiji cha Kising’a kata ya Kising’ tarafa ya Isimani ulivyowakomboa wanakijiji. Baadhi ya watekelezaji wa mradi wa MUVI wakijadili jambo na meneja wa ubao wa matangazo Rehema Msalilwa (wa pili kulia).



MBAO za matangazo kwa wajasiriamali zimemkomboa kimaisha Nelson Mbimbi mkazi wa kijiji cha Kising’a Kata ya Kisinga tarafa ya Isimani Wilaya ya Iringa katika Mkoa wa Iringa.

Akiongea na mtandao huu Mbimbi amesema mbao za matangazo zilizobandikwa na Muunganisho Ujasiriamali Vijijini (MUVI) juu ya bei za mazo zimemfanya kujikomboa na umasikini aliokuwa nao.

“Niliona matangazo ya MUVI yamebandikwa kwenye mbao za matangazo katika kijiji changu yaliyokuwa yakihusu wajasiriamali, bei za mazao yote yanayozalishwa hapa kijijini, wanakijiji tulipewa elimu ya matumizi ya  ubao wa matangazo japo kuwa sikuona umuhimu” alisema Mbimbi.

Amesema mara kwa mara alikuwa akijiuliza, ni mara ngapi ubao uandikwe na kuundiwa kamati ya kuusimamia ubao hali ambayo alisema aliona ni ya kipuuzi hadi hapo alipoeleweshwa kuutumia.

Amesema kwa muda mrefu wakulima wa kijiji hicho wamekuwa wakilima bila mafanikio kutokana na elimu ndogo waliyokuwa nayo na kubaki gizani kutokujua nini cha kufanya.

Hata hivyo amesema “licha ya kulima bila mafanikio, hatukuwahi kufikiri kuhusu suala la mawasiliano, kupashana habari juu ya kile tulichokuwa tukizalisha. Kila mtu aliuza kwa bei yake hata walanguzi walitumia ukosekanaji wa taarifa kama njia ya kutunyonya kwa kuwa hatukujua kama tunadhulumiwa”.

Amesema ubao huo uligawanyika katika sehemu kuu mbili ambapo sehemu ya kwanza ilihusu taarifa za bei na masoko na hehemu ya pili ilihusu taarifa kijamii.

Anaainisha kuwa “Sehemu ya kwanza, taarifa za bei inayotembea kijijini hapa pamoja na mikoa ya jirani. Sehemu ya pili taarifa zinazohusu jamii husika”.

Pamoja na kwamba mradi wa MUVI unajihusisha na kuendeleza mnyororo wa thamani wa zao la alizeti na nyanya katika mbao za matangazo hizo mazao mengine pia yamepewa nafasi katika ubao huo kuonesha bei.

“Wanakijiji wapatao 60-150 huweza kupata taarifa za bei kupitia ubao wa matangazo kila wiki. Mimi ni mmoja kati yao, kila siku bei zinavyoandikwa  huwa naenda kujisomea  na kufahamu bei inayotembea sokoni” anasema.

Anasema kuwa walanguzi wengi hufika vijijini kununua mazao kwa mazoea kuwa watu wa vijijini hawajui bei za matangazo lakini leo ni tofauti kwani wakulima wengi wameshapata elimu

“Anakuja mlanguzi anataka kununua alizeti gunia moja lenye ujazo wa kilo 60 kwa shilingi elfu (30) thelathini…wakati huo ubao wamatangazo umendikwa gunia la kilo 60 ni shilingi elfu 50 hamsini” anasema.

Anasema wakati mwingine walanguzi wanakuwa wanaifahamu bei ya mazao lakini kwa makusudi wanataka kumgandamiza mkulima; wanajaribu kushawishi ili wanunue bei zao lakini kwa kuwa bei zimeandikwa katika mbao za matangazo, inakuwa ni vigumu kushawishika kirahisi.

“Mlanguzi akija na kuanza kutushawishi kwa bei zake, swali la kwanza huwa tunamuuliza hivi: umesoma ubao wa matangazo? Mlanguzi anajibu hapana halafu tunamwambia: Kasome halafu  urudi… halafu anaondoka kwa aibu” anasema Mbimbi.

Ubao wa matangazo kwa wajasiriamali vijijini  huandikwa taarifa za bei kila  baada ya siku tatu, yaani jumatatu, jumatano na ijumaa.

Mbimbi anaeleza kuwa baada ya kuweza kutumia vizuri mbao za matangazo kujihabarisha, amefanikiwa kununua pikipiki aina ya SunLug na pia ameweza kulipia gharama za kuunganishiwa umeme kwenye nyumba yake hapo kijijini.

Kijiji cha Kising’a kipo katika umbali wa takribani kiometa  25 kutoka mjini Iringa. Ni kijiji ambacho wakazi wake hujishughulisha na kilimo cha alizeti  pamoja na mazao mengine kama vile mahindi, kunde, mtama  na mazao ya mboga mboga.

No comments:

Post a Comment