masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Monday, November 5, 2012

MAMLAKA YA MAPATO (TRA) MKOA WA IRINGA YAVUKA MALENGO UKUSANYAJI KODI > WALIPAKODI 24 KUTUNUKIWA VYETI > YADAI BILIONI 1 KWA WALIPAKODI

Meneja wa Mamlaka ya Mapato (TRA) Mkoa wa Iringa Rosalia Mwenda akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo.

Meneja wa TRA Mkoa wa Iringa katikati, Meneja Msaidizi Swalehe Byarugaba kulia na Meneja Msaidizi - Madeni na Ulipaji kodi kwa ridhaa Salehe Kiluwa kushoto.

Mr. Hilly mfanyakazi wa TRA kushoto na Mr. Ipyana Mwakalinga mhasibu wa TRA Mkoa wa Iringa kulia.

Godfrey Mushi mwandishi wa Nipashe akimsikiliza meneja wa TRA.

Laurian Mkumbata mwandishi wa ITV na Radio One akiandika habari katika ofisi ya meneja wa TRA.

Zulfa Shomari mwandishi wa Mwananchi akiandika habari katika ofisi ya meneja wa TRA.

Mamlaka ya mapato Mkoa wa Iringa imekusanya zaidi ya shilingi 24 bilioni zaidi ya kiwango walichopangiwa na serikali kukikusanya kwa mwaka wa fedha wa 2011/2012.

Taarifa hiyo imetolewa leo na meneja wa mamlaka ya mapato katika Mkoa huo Rosalia Mwenda alipokuwa akiongea na vyombo vya habari ofisini kwake.

Kiasi hicho ni zaidi ya kile kilichopangwa na serikali kukusanywa kwa muda huo ambapo jumla ya shilingi 23 bilioni zilitakiwa kukusanywa.

Kodi hizo zilizopangwa kukusanywa ni pamoja na ushuru wa forodha pamoja na kodi za ndani.

Taarifa hiyo imetolewa wakati mamlaka ya mapato inaadhimisha siku ya mlipa kodi ambayo kilele chake kinatarajia kufanyika Novemba 7, mwaka huu ambayo katika Mkoa wa Iringa itafanyika katika ukumbi wa Chuo Kikuu Huria.

Wakati wa maadhimisho ya siku ya mlipa kodi, mamlaka ya mapato katika Mkoa huo, jumla ya shilingi 877,000, zimekusanywa kwa ajili ya kutoa msaada wa kibinadamu katika kituo cha kulelea watoto yatima cha kiislamu cha Dhinurayn kilichopo Ilala mkoa ni humo.

Wakati akitoa taarifa hiyo, Mwenda amewataka wananchi kutoa maoni juu ya huduma zinazotolewa na mamlaka hiyo ili palipo na mapungufu yafanyike marekebisho kwa ajili ya kusimamia haki pamoja na kutoa mafunzo kwa wanafunzi mbalimbali juu ya masuala ya kodi.

“Katika maadhimisho hayo, tutatumia fursa hii kupokea maoni ya wateja na wadau mbalimbali juu ya huduma zetu ili pale ambapo panakuwa na mapungufu tuweze kurekebisha ili kutoa huduma kwa haki na pia tutatoa semina kwa wanafunzi kuhusu masuala ya kodi ili wawe wasambazaji wetu wa taarifa na watoaji wa elimu kwa watu mbalimbali” amesema Mwenda.

Ikiwa maadhimisho ya siku ya mlipa kodi huambatana na kauli mbiu, mwaka huu maadhimisho hayo yanabebwa na kaulimbiu inayosema “Ulipaji Kodi wa Hiari kwa Taifa Lenye Mafanikio”.

Katika kufanikisha ukusanyaji wa mapato hayo kwa mwaka 2011/2012 njia mbalimbali zilitumika ikiwemo ya kutoa semina kwa walipakodi, kutoa huduma bora kwa wateja, kutoa mafunzo ya kodi kwa wanafunzi pamoja na kuhamasisha walipakodi kwa njia ya redio na matangazo.

Amesema kuna sababu ambazo zinaweza kukwamisha ukusanyaji wa kodi kwa wateja ikiwemo ja kudorora kwa hali ya uchumi duniani ambako huchangia kwa kiawango kikubwa kupotea kwa pato la serikali pamoja na kushuka kwa makusanyo ya kodi ya ongezeko la Thamani (VAT).

Lengo la maadhimisho ya siku ya mlipakodi ni kutambua ushiriki wa walipakodo katika kuhakikisha kuwa na ulipaji kodi wa hiari kwa Taifa.

Ikiwa Novemba 7 yatakuwa ni maadhimisho ya sita, Mamlaka ya Mapato Mkoa wa Iringa watawatunuku vyeti jumla ya walipakodi 24 ambao wapo mstari wa mbele katika kuweka kumbukumbu za za biashara kwa usahili, kulipa kodi zinazolingana na biashara zao, kujituma kulipa kodi kwa wakati kisheria na wale wanaolipa kodi zao kwa hiari.

Hata hivyo Mwenda amesema wanaendelea kufuatilia madeni kutoka kwa walipakodi ambapo kiashi cha shilingi 1 bilioni hazijalipwa kutoka kwa wafanyabiashara mbalimbali.

“Pamoja na kuvuka malengo, wapo walipakodi mbalimbali ambao wanadaiwa bado hawajalipa kodi zao. Madeni hayo ni ya muda mfupi nay ale ya muda mrefu ambapo hivi sasa kiasi ambacho walipakodi wetu wanaodaiwa ni shilingi bilioni 1. Tutahakikisha kuwa wanalipa kwa kutumia njia mbalimbali pamoja na wadau wengine wanaokusanya kodi hizo” amesema.

Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) ilianza kusherehekea siku ya mlipakodi mwaka 2006 ilipotimiza miaka 10 tangu kuundwa mwaka 1997.

No comments:

Post a Comment