Mbunge
wa jimbo la Iringa mjini Mch. Peter Msigwa ametoa vifaa vya michezo katika timu
mbalimbali za mpira wa miguu vyenye thamani ya zaidi ya shilingi 6 milioni.
Msigwa
alitoa jezi na mipira juzi katika timu hizo ikiwa ni maandalizi ya shindano la
Msigwa Cup linalotarajiwa kuanza ndani ya Manispaa wiki chache zijazo.
Baadhi
ya timu ambazo zimepewa vifaa hivyo ni pamoja na timu mbalimbali ikiwemo timu
ya mpira ya shule ya sekondari ya Kihesa, timu za vijana wa Kihesa, Mivinjeni
pamoja na timu ya vijana ya Ulonge.
Akikabidhi
vifaa hivyo, Msigwa alisema viongozi wa timu za mpira wanatakiwa kuwa na umoja
na si marumbano.
“Tatizo
la timu zetu hizi ni uongozi. Hatuwezi kusonga mbele kama
kila siku katika timu zetu ni malumbano tu. Tujaribu hata kubadilisha mfumo wa
uongozi wetu ili tusonge mbele” alisema.
Alisema
sababu nyingine ni viongozi kuendekeza ubinafsi na kutafuta maslahi badala ya
kuendeleza soka.
“Tuache
kuweka maslahi mbele na ubinafsi badala ya kuendeleza soka. Mifumo tuliyonayo
ibadilishwe ili tupige hatu mbele” alisema.
No comments:
Post a Comment